Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Wana Ukumbi,

Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.
Ila afahamu kwenye tatizo wilaya ya kinondoni sio huko madale tu, pia Halima mdee hana kampuni ya ujenzi yeye anategema mipango thabiti ya halmashauri ya kinondoni ambayo ndiyo ina vipaumbele vyote vya barabara mezani, badala ya kumlaumu moja kwa moja aende kwanza kwenye Ofisi ya mtendaji kata wa eneo lenye tatizo aelezwe tatizo ni nani? pamoja na hayo kwa kuwa yeye amefanikiwa sana kwenye medan ya music basi aeleze kama mwananchi aliyeguswa na kero hiyo anasaidiaje japo vifusi tu?
 
Huyo diamond aendelee kukata viuno tu sie watu wa kawe hatuwezi chagua muimba taarabu


Si bure huyo domo atakuwa anawashwa
 
Unamsemea Diamond huyu makapelo kufunika???bwai..chizi hilo linajua kitu kwani,Mdee ana kusanya kodi kwani
 
Hizo pesa za kununua masinki ya dhahabu, na vitanda vya watoto walio tumboni vya dhahabu alitakiwa Diamond kama msanii mwenye mafanikio makubwa afanyie kazi za kijamii kama hizo. Halima Mdee hana fungu, lazima aombe ombe na serikali kwa kuonyesha mabavu itamnyima hela ili yatokee malalamiko kama hayo.

Haisaidii kuwa na ghorofa pekee yako kijiji kizima.
Afadhali uwaambie na manyinyiem ya humu
 
Last edited by a moderator:
Diamond gan? ni yule mtembea nusu uchi mpenda kushika sehemu zake za mbele akiwa manukwaani? Ikiwa ni yule bc ktk watu mapoyoyo tz yule ni mmoja wapo na yy pia ni ninamfananisha na gari lililobeba taka likipeleka dampo, bendela fuata upepo ndio watamuelewa anachosema chiz yule watu makini hawawez kumckiliza mpuuz yule
 
Wana Ukumbi,

Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.


Thread ya April 2015 hii.
 
Kwanini alitoa ahadi kwa wananchi kuwa katika ubunge wake huu atahakikisha barabara inajengwa? Ikiwa alijua yeye sio serikali in the first place!
Milioni 50 kila kijiji His excellence kushindwa! Unashangaa nini kwa mbunge??? TENA wa Upinzani!!
 
Back
Top Bottom