Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Kwa nini aliahidi kuwaletea wananchi wa madale barabara ya lami ikiwa anajua kuwa hana kampuni ya ujenzi?

Unauhakika aliahidi hio barabara?. Diomond mwenyewe kahamia juzi tu. Hayo mambo anayajua wapi?. Aache kujikombakomba.
 
Kwa hadhi yake hatakiwi kulialia tena afanye kama yulee mbunge wa bunge la africa mashariki jina limenitoka somebody Bhanji
 
Kwa hiyo Mdee ndio serikali? Nahisi huyu jamaa nyimbo za ngono anazoimba zinamponza. Kwa nini asijjenge yeye si ana hela?
 
Halima Mdee ana kampuni ya ujenzi wa barabara?
Siku tukijua nani wa kumwajibisha nchi yeru itasonga mbele.
Kwa sasa adui ujinga bado anatutesa

Sasa alivyotoa hiyo ahadi alitegemea zitajijenga zenyewe au!????

CDM + CCM = Ukoo Wa Panya
 
Usipanik please, kanunue bidhaa kutoka kwenye duka lenye EFD hata kama ni penseli utaona kodi unayolipa. Kajifunze aina za kodi kwanza ndio uje hapa. Mdee lazima ajifunze..kuna haki na wajibu, sie tumemchagua yeye awakikishe matatizo yetu. Wanaowakilishwa vizuri wamefanikiwa
 
Kuwa star kwenye mziki haimaniishi kuwa Diamond kichwani anaakili ,... Toka lini Mdee akakusanya kodi? Mdee ndo waziri wa Ujenzi? Hawa wanamuziki wanatakiwa wajiendeleze kielimu kwa manufaa yao badala ya kuropoka kudhihirisha utupu kwenye mbongo zao ...
 
Matokeo ya kufikiri kwa masaburi. Halima anawaahidi kuwajengea barabara yeye ni serikali? Tangu lini wabunge wakajenga barabara. Serikali ndiyo ya kulaumiwa na si HM.

Kwahiyo Halima Mdee aligeuka kuwa msemaji Wa serikali alivokua anatoa ahadi 2010 au!???
 
Kwa hiyo ninyi mkiahidiwa na yeyote hamna akili ya kuhoji?

watu wengine hujifunza ujinga shuleni ( FaizaFoxy )
Watu wa Kg bwana! Kama anataka kupoteza his music fame ajaribu kujiingiza kwenye siasa. Kawe si jimbo la wajinga kiasi hicho!
 
Last edited by a moderator:
wana ukumbi,

msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, diamond platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo madale ambayo ipo kwenye jimbo la kawe chini ya halima mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya chadema kwa kuwa halima mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha clouds tv pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge halima mdee.

ahadi ni deni
 
Wana Ukumbi,

Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.

yeye si mbeba sembe.ajenge
 
Domoli nae so hata hili nalo hajui muhusika ni nan?
 
Huyu nae kujipendekeza gani huku??? Hivi andhani kujenga barabara ni sawa na kumtia mimba zari? nonsense.
 
Kama wewe ni mbunge na katika jimbo lako kero hazitatuliwi, ujue tu hauna ushawishi.

Katika hali hiyo ya kukosa ushawishi, basi hufai kuwa mwakilishi wa wananchi husika. It's simple as that.

Halima, time to go!

Tunasubiri Ujiji iwe kama Dubai, Uwanja wa ndege Misenyi,Meli mpya ziwa Victoria,........
 
Back
Top Bottom