Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Diamond Platnumz: Mdee ni Mzigo Jimbo la Kawe

Hizo pesa za kununua masinki ya dhahabu, na vitanda vya watoto walio tumboni vya dhahabu alitakiwa Diamond kama msanii mwenye mafanikio makubwa afanyie kazi za kijamii kama hizo. Halima Mdee hana fungu, lazima aombe ombe na serikali kwa kuonyesha mabavu itamnyima hela ili yatokee malalamiko kama hayo.

Haisaidii kuwa na ghorofa pekee yako kijiji kizima.
 
Last edited by a moderator:
kama hana mbona aliahidi atajenga?chadema kama ccm tu

alisema ataihamasisha serikali, ijenge barabara hiyo, lakin si kutoa pesa zake mfuk0ni ili ajenge barabara

source. -mi mwenyewe nilikuwkovkipindi cha kampeni zake.
 
Upinzani na Alikiba umemshinda anaanza upinzani na mdee
 
Hizo pesa za kununua masinki ya dhahabu, na vitanda vya watoto walio tumboni vya dhahabu alitakiwa Diamond kama msanii mwenye mafanikio makubwa afanyie kazi za kijamii kama hizo. Halima Mdee hana fungu, lazima aombe ombe na serikali kwa kuonyesha mabavu itamnyima hela ili yatokee malalamiko kama hayo.

Haisaidii kuwa na ghorofa pekee yako kijiji kizima.

Acheni wivu mbaya. Kuweni na wivu wa maendeleo. Diamond ni haki yake kumiliki chochote kutokana na jasho lake. Na Watanzania na dunia nzima ni mashahidi jinsi bwana mdogo huyo anavyochakarika. Tumtie moyo awe mfano mwema kwa vijana wenzake badala ya kumkatisha tamaa. Yeye ni msanii wa muziki. Halima ni mwanasiasa. Halima ndiye mwenye wajibu wa 'moja kwa moja' wa kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo lake. Huo ni wajibu wake, asikwepe wajibu wake! Na ninyi msijifanye kama vile hamwelewi kuwa huo ndio wajibu wake Halima! Atawaleteaje maendeleo wananchi hao? Hiyo ndio changamoto inayomkabili Halima. Kwani alijitutumua kuomba kura akifikiri wananchi wa Kawe walimpa ili apite akilalamika tu? Acheni hizo banaa!! Kuweni wakweli. Ni WAJIBU wa Halima kuhakikisha barabara hiyo inajengwa. Sivyo, akiache kiti cha ubunge wa Kawe mara moja akafanye shughuli nyingine!! Acheni kutetea ujinga!!!
 
Acheni wivu mbaya. Kuweni na wivu wa maendeleo. Diamond ni haki yake kumiliki chochote kutokana na jasho lake. Na Watanzania na dunia nzima ni mashahidi jinsi bwana mdogo huyo anavyochakarika. Tumtie moyo awe mfano mwema kwa vijana wenzake badala ya kumkatisha tamaa. Yeye ni msanii wa muziki. Halima ni mwanasiasa. Halima ndiye mwenye wajibu wa 'moja kwa moja' wa kuwaletea maendeleo wananchi wa jimbo lake. Huo ni wajibu wake, asikwepe wajibu wake! Na ninyi msijifanye kama vile hamwelewi kuwa huo ndio wajibu wake Halima! Atawaleteaje maendeleo wananchi hao? Hiyo ndio changamoto inayomkabili Halima. Kwani alijitutumua kuomba kura akifikiri wananchi wa Kawe walimpa ili apite akilalamika tu? Acheni hizo banaa!! Kuweni wakweli. Ni WAJIBU wa Halima kuhakikisha barabara hiyo inajengwa. Sivyo, akiache kiti cha ubunge wa Kawe mara moja akafanye shughuli nyingine!! Acheni kutetea ujinga!!!

You're a great thinker!
 
wana ukumbi,

msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, diamond platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo madale ambayo ipo kwenye jimbo la kawe chini ya halima mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya chadema kwa kuwa halima mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha clouds tv pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge halima mdee.

huyu dangote wa makaratasi nae vipi ? Kumbe muziki wa bongo haulipi, dangote anaomba lami kwa mbunge ?
 
Kwanini alitoa ahadi kwa wananchi kuwa katika ubunge wake huu atahakikisha barabara inajengwa? Ikiwa alijua yeye sio serikali in the first place!

Mbona rais alisema "maisha bora kwa kila mtanzania" na leo 1USD inakaribia 2000...achilia mbali hali mbovu ya maisha kwa wa tanzania!!
 
Dont ask what America have done to you! Ask what have you done to America. J F K

That is America. Not Tz.

By the way, do you think someone should not ask/condemn the representative just because he/she is CDM or CCM?

Rubbish!
 
Barabara za jimbo la kawe aibu kashalewa hata hivyo asahau kawe labda kigoma kaskazini
 
Diamond ni mfano wakuigwa ktk kutoa na ndio maana anazidi kufanikiwa huyo mbunge wenu kazi yake ni hiyo
 
Halima Mdee ana kampuni ya ujenzi wa barabara?
Siku tukijua nani wa kumwajibisha nchi yetu itasonga mbele.
Kwa sasa adui ujinga bado anatutesa
Na ndio maana wabunge wengi wanatumia gia ya kuomba kura kwa kutoa ahadi ya kuleta maji, umeme na huduma ya simu utasema wakichukua ubunge wanakabidhiwa fedha za halmashauri, siku ambayo wananchi wa Tz tutapotambua kazi ya mbunge nadhani ndio tutachagua wabunge wazuri maana imekuwa kawaida barabara ikiwa mbovu anaangaliwa mbunge kumbe barabara zingine zipo chini ya halmashauri ya wilaya na inashughulikiwa na baraza la madiwani tu
 
Jonh mnyika ; naye ni mzigo ; ziara utadhani vasco dagama tanzania wkt anahijua
 
Wana Ukumbi,

Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.

Huyu Diamond akili zake km Kepten Komba. Ndo mana amenukuliwa akisema Kikwete anajua mengi kuhusu mziki kuliko yeye!
 
Wana Ukumbi,

Msanii maarufu nchini mwenye mafanikio makubwa katika sanaa ya mziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, amevunja ukimya wake juu ya ubovu wa barabara iendayo Madale ambayo ipo kwenye jimbo la Kawe chini ya Halima Mdee.

Msanii huyo ameelekeza lawama zake kwa mbunge huyo wa kupitia tiketi ya CHADEMA kwa kuwa Halima Mdee aliahidi wananchi wa jimbo hilo kuwa katika kipindi chake cha ubunge atahakikisha barabara hiyo inajengwa kwa kiwango cha lami, lakini hadi hii leo barabara imejaa tope tu!

Diamond alieleza masikitiko yake huyo kupitia katika kituo cha Clouds TV pale alipoulizwa swali kuhusu makazi yake mapya yaliyopo katika jimbo la Kawe na ndipo hapo akafunguka kuhusu suala hilo la kero ya barabara ambalo lina muda mrefu alijashughulikiwa na mbunge Halima Mdee.

Kwa akili hizi za Diamond ipo siku atamlalamikia mama yake kwanini sio mzuri kama Zari, The Boss Lady!
 
dimond kama watu wa moro wanakuita,so madale ni wewe tu
au madale ni ya kina madale
 
Back
Top Bottom