Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Attachments

  • 20260315_133547.jpg
    20260315_133547.jpg
    117.1 KB · Views: 14
Narudi tena kusema kumfukuza Maresca na kumleta kocha aliye chini yake kiuwezo ni kosa kubwa.

Matatizo ya hii hii yanajulikana ila kwakiwa wale masporting director wako pale na wamiliki wanaendelea kuziba maskio acha tuendelee kuisoma namba.

Huwez spend zaidi ya 1+BN kwenye usajili na bado team yako haiko sawa.


Umetoka kuchukua club world cup sajili wachezaj wa maana watakao kutoa level uliyopo na kwenda juu ndio kwanza unasajili squad player.

Siku wale SD watakapoondoka ndio siku hii team inaweza endelea kwa sasa acha waendeleze connection maana sidhan kama wanaweza pata nafasi kama hiyo
 
Team yetu imeharibika baada ya kuuzwa, kwa hawa matajiri wa sasa. Maana wao wapo kibiashara zaidi, wamefanya sajili nyingi ambazo hazijatupa matokeo bora zaidi. Mfano msimu huu wachezaji tuliosajili na wakafanya vizuri ni mmoja tu Joao Pedro. Wachezaji wengi waliosajiliwa hawana sifa za kucheza Chelsea. Mchezaji kama Tosin, Badiashile, Hato, Esugo, Neto, Delap, Andre Santos, Marc, Gerlach, Gitten na Jorgensen. Hawa ni hasara tu
 
Hakuna mtu aliyewahi kudai kwamba Chelsea ni timu nzuri. Matatizo ya hii timu tunayajua, na tumekuwa tukiyasema kila siku. Kuwa na imani na timu yako haimaanishi kujifanya kwamba ni timu bora. Msimu huu karibu kila timu iliyo juu ya table ina mapungufu, lakini Chelsea ina matatizo makubwa zaidi — na tunajua sababu. Wamiliki hawataki kusajili wachezaji wenye ushindani wa kweli.

Arsenal wamesajili Gyökeres, sisi tukaleta Delap mchezaji wa kiwango cha Championship kama mshambuliaji.
Manchester City wamemsajili Marc Guehi, sisi tukachukua Mamadou Sarr na Tosin bure.
Manchester United wamemsajili Cunha na Mbeumo, sisi tukaleta Gittens na Garnacho.

Hii ndiyo hatima tuliyolazimishwa kuikubali chini ya hawa Wamarekani wasio na akili ya uongozi. Hata huo utajiri wanaodaiwa kuwa nao sijui wamaupataje? labda wameiba, maana uwezo wa kufanya maamuzi ya maana kwenye soka hauonekani kabisa.
NItaandika hivyo mara nyingi kwakua mmekua mkisema mara nyingi kwamba mna wachezaji wazuri na world class kuliko waongoza ligi Arsenal.

Mlisajili wachezaji karibu 25, huwezi taja wanne kwamba ndiyo chanzo.
 
NItaandika hivyo mara nyingi kwakua mmekua mkisema mara nyingi kwamba mna wachezaji wazuri na world class kuliko waongoza ligi Arsenal.

Mlisajili wachezaji karibu 25, huwezi taja wanne kwamba ndiyo chanzo.
Sasa mkuu unataka tukwambie akina Saka na Martinell ni world class?!!
 
NItaandika hivyo mara nyingi kwakua mmekua mkisema mara nyingi kwamba mna wachezaji wazuri na world class kuliko waongoza ligi Arsenal.

Mlisajili wachezaji karibu 25, huwezi taja wanne kwamba ndiyo chanzo.
Wachezaji wazuri kuliko Arsenal wapo, ila kuna pia matakataka.
Bati imara na mpya haiwezi kufanya nyumba isivuje kama kuna bati mbovu na kuukuu katikati
Chelsea tuna shida ya Defense na winga wachanga
Chelsea tuna shida ya kubadilisha badilisha makocha na hata anayeletwa bado nao ni wacganga kama wachezaji
Bado nyufa zipo na hawa wamarekani naona wanajitahidi kuziba kwa udongo badala ya zege
 
Team yetu imeharibika baada ya kuuzwa, kwa hawa matajiri wa sasa. Maana wao wapo kibiashara zaidi, wamefanya sajili nyingi ambazo hazijatupa matokeo bora zaidi. Mfano msimu huu wachezaji tuliosajili na wakafanya vizuri ni mmoja tu Joao Pedro. Wachezaji wengi waliosajiliwa hawana sifa za kucheza Chelsea. Mchezaji kama Tosin, Badiashile, Hato, Esugo, Neto, Delap, Andre Santos, Marc, Gerlach, Gitten na Jorgensen. Hawa ni hasara tu
Kwa Pedro Neto nakataa, huyu ana hadhi kabisa ya kucheza Chelsea ni vile tumekosa structure nzuri ya team kwa style hii hata Palmer itafika hatua utamuona mbaya hivi nikuulize nafasi gani ya maana Joao Pedro alitengenezewa kwa mechi ya juzi?
 
Wachezaji wazuri kuliko Arsenal wapo, ila kuna pia matakataka.
Bati imara na mpya haiwezi kufanya nyumba isivuje kama kuna bati mbovu na kuukuu katikati
Chelsea tuna shida ya Defense na winga wachanga
Chelsea tuna shida ya kubadilisha badilisha makocha na hata anayeletwa bado nao ni wacganga kama wachezaji
Bado nyufa zipo na hawa wamarekani naona wanajitahidi kuziba kwa udongo badala ya zege
Wachezaji wa Arsenal wanaonekana ni wazuri ni kwasababu Wanamfumo mzuri wa kiuchezaji unaoeleweka kwa kila mchezaji kwasababu wachezaji wamekaa kwa pamoja kwa muda mrefu plus morali ya team but Wana wachezaji wengi tu wa kawaida kina martinell, Jesus, Kai, tossard, Zubimend, Eze, Madueke n.k hawa wote niliyo wamention hawana muendelezo mzuri wa viwango vyao
 
Ndg, tukipata Conference league tutashukuru sana kwa sababu tutabeba kikombe. Cha kushangaza hata hiyo Conference tunaweza kuikosa
Usijikatie tamaa mastA, lolote linawezekana EpL ni ngumu mno .......... katimu kapo mkiani kamaweza kumshikisha adabu muongoza ligi.... ndio maana ni ligi bora ulimwenguni
 
BREAKING NEWS:
Chelsea imepigwa ban ya kusajili na kuandikisha wachezaji wa Timu ya kwanza kwa mwaka mmoja halafu ikafanyiwa suspension. Sijawahi kuiona adhabu ya jinsi hiij lakini ngoja nijaribu kuielezea.

Kimsingi Ligi Kuu Ya Uingereza imeipa Chelsea adhabu ya kutosajili wachezaji kwa mwaka mmoja halafu hiyo adhabu ikahairishwa hadi Machi 2028 kwa masharti yafuatayo:
  1. Adhabu imesitishwa kwa miaka 2 hadi takriban Machi 2028.
  2. Chelsea inaweza kusajili wachezaji wapya kawaida ndani ya miaka hiyo 2.
  3. Kifungo cha mwaka 1 kitaanza tu ikiwa Chelsea itafanya makosa mengine ndani ya kipindi hicho.
  4. Makosa yanayohusika ni ya ukaguzi wa fedha, uwekezaji wa watu wa tatu, na maendeleo ya vijana (kutoka malipo yasiyoripotiwa 2011–2018).
  5. Hii ni tofauti na kifungo cha miezi 9 cha usajili wa akademi, ambacho kinaendelea hadi takriban Desemba 2026.
Uhamisho wa Abramovivh wa kuanzia 2011 - 2018 ulihusisha uhamisho wa Eden Hazard, David Luiz, Andre Schurrle, Ramires, Matic, Willian, Eto'o nk.

1773670652345.png
 
Miracles happen — and when they do, mambo yanakuwa hivi.

Chelsea vs PSG – Second Leg at Stamford Bridge

00' – Kick‑off
20' – João Pedro scores → Chelsea 1–0 PSG
23' – Rúben Neves sent off (red card)
24' – Cole Palmer converts a penalty → Chelsea 2–0 PSG
44+2' – João Pedro strikes again in added time of first half→ Chelsea 3–0 PSG

45' – Half‑time

50' – Dembélé pulls one back → Chelsea 3–1 PSG
55' – Enzo restores the three lead → Chelsea 4–1 PSG
56' – Cucurella booked (yellow card)
74' – Andrey Santos finishes it → Chelsea 5–1 PSG
87' – Kvaratskhelia hits the post
90+7' – Full‑time → Chelsea 5–1 PSG

Aggregate: Chelsea 7–6 PSG

Chelsea march into the quarter‑finals against Liverpool.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom