Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Delap akiwa uwanjani ni kama mpo 10 tu .... hana msaada wowote, sio link up play, sio kusumbua mabeki wa timu pinzani, wala pasi nzuri..... lijamaa ni hewa,,,, kocha nae kiazi kila siku anapambana anampa minutes
 
Leo nimeamka nikiwa mnyonge, nimekata tamaa, sina nguvu wala hamu ya kufanya hata yale mambo ninayoyapenda. Sikuelewa tatizo ni nini mpaka baadaye nikakumbuka kuwa jana Chelsea walicheza… na wakafungwa na wale legelege PSG. Sasa sisi mashabiki furaha yetu itatoka wapi kama hata PSG tunashindwa kuwapiga. Tunarudi Stamford Bridge tukihitaji ushindi wa 4–0 ili kuwatoa kwenye UCL. Kwa hali hii, Chelsea inabaki na tofauti gani na Tottenham au Man City.
 
Sikuweza kufuatilia mechi yote jana, lakini kwa kweli, kama wamiliki hawataziba mapengo haya kwenye dirisha lijalo la usajili, basi wanapaswa kuachia ngazi.

Tunahitaji mjadala mzito kuhusu nafasi ya golikipa. Huwezi kushindania mataji kama EPL au UCL ukiwa na makipa kama Sánchez na Jørgensen. Tofauti kubwa kati ya Jørgensen na Sánchez iko kwenye uwezo wa kuokoa mashuti—ni kama Jørgensen haoni kabisa mashuti yakipigwa. Sitaki tena kumuona Jørgensen akianza kwenye mechi kubwa za ligi au UCL. Mungu apishe mbali. Amina.

Tunapaswa kumsajili beki ambaye si wa kubahatisha—kiongozi wa kweli wa kuja kushirikiana na Colwill. Waliobaki wabaki kuwa backups au waondoke.

Chelsea walikuwa bora kuliko PSG kwenye karibu kila idara jana, lakini makosa ya makipa na mabeki ndiyo yametufikisha hapa tulipo.

Gameplan ya Rosenior pia haujakaa imara kama wa Maresca, hasa kwenye mechi kubwa kama hizi. Sikuona mkakati wowote wa kuwapress PSG hadi washindwe kucheza mpira wao. Hakukuwa na mpango wa kuwadhibiti wachezaji hatari wa PSG kama Dembélé au Kvaratskhelia.

Kama tungeweza kudhibiti uzembe wa jana, matokeo yangekuwa 2–2, au hata kama tungefungwa, labda 3–2. Baadhi ya yale magoli yalikuwa yanazuilika kabisa kama mabeki wangekuwa imara.

Sasa tunadaiwa magoli matatu, tuna chini ya siku sita kujiandaa kwa mchezo wa marudiano Stamford Bridge—na bado tuna Newcastle wikiendi hii kwenye mechi kubwa ya PL ya kupigania nafasi ya top 4.
1773304201463.png
 
Naona hapa kuna come back kama moja au mbili
  1. Tottenham Hotspur 2-5
  2. Chelsea 2-5
  3. Man City 0-3
Aidha mji wa Manchester au London wiki ijayo tutegemee comeback kama ile ya:
  1. Liverpool 4–0 Barcelona (2019)
  2. Chelsea vs Napoli (2012)
 
Rosemary jana UCL imemuexpose uwezo wake kama kocha kaja na mbinu nzuri mwanzoni ila uwezo wa kusoma mchezo ndani ya mchezo ndio umemuexpose

Yule kipara mwenda zake mechi kama hii alikuwa anawabamiza tena
hawa PSG
Game management na playing style inayoendana na resource bado ni mtihani kwa kocha na SD

Playing from back kwa kipa na mabeki wasio na uwezo wa kucarry mpira ni red flag kwa kocha lazima mmoja ampishe mwenzake
 
Rosemary jana UCL imemuexpose uwezo wake kama kocha kaja na mbinu nzuri mwanzoni ila uwezo wa kusoma mchezo ndani ya mchezo ndio umemuexpose

Yule kipara mwenda zake mechi kama hii alikuwa anawabamiza tena
hawa PSG
Game management na playing style inayoendana na resource bado ni mtihani kwa kocha na SD

Playing from back kwa kipa na mabeki wasio na uwezo wa kucarry mpira ni red flag kwa kocha lazima mmoja ampishe mwenzake
Umesema ukweli uwezo wa beki zetu ni mdogo sana, beki hawezi hata kupga pasi hata moja ya mbele kwa zote dk.90. Beki kichwani inajua back pass tu, beki hawezi hata kujitaftia nafasi ya kupga pasi kwa kusogea na mpira pale anapoishiwa na option. Sasa hii mibeki kama miroboti hapo hapo aliposimama anapga back pass.

Unaweza ukamlaumu kipa ila lawama zirudi kwanza kwa beki kwa kusababisha kipa kuwa kwenye presha mara kwa mara kwa kumrudishia mipira kila mara.

Sina uelewa wa ukocha ila Yaani kocha hakuona kabisa mechi ya jana iliwahitaji zaid Garnacho na Neto, mana beki zao zilikuawa zinakuja juu na kushambulia, mipira mirefu kwa kina Garnacho ingehusika. Cha kushangaza anaingia Delap!!! halafu nje alikua anapasha Mjomba Tosin na shoga ake Badiashile, tungekua bado mbili mbili wangeingia hao wajomba pia. Bora Maresca aisee dah!!
 
Timu za Uingereza Bana, yani timu sita hakuna hata moja iliyoshinda...Timu ambazo unaweza kusema zina nafasi kusonga mbele kwenye makaratasi ni timu mbili Tu ambazo ni Liverpool na Arsenal, nahisi Newcastle, Man City, Chelsea kuna mmoja anaweza kufanya comeback hapa na mechi kuamuliwa na Extra time au matuta....
 
Timu za Uingereza Bana, yani timu sita hakuna hata moja iliyoshinda...Timu ambazo unaweza kusema zina nafasi kusonga mbele kwenye makaratasi ni timu mbili Tu ambazo ni Liverpool na Arsenal, nahisi Newcastle, Man City, Chelsea kuna mmoja anaweza kufanya comeback hapa na mechi kuamuliwa na Extra time au matuta....
Muondoe THE BLUES hapo hawezi fanya come back. Ameshatolewa
 
Rosemary jana UCL imemuexpose uwezo wake kama kocha kaja na mbinu nzuri mwanzoni ila uwezo wa kusoma mchezo ndani ya mchezo ndio umemuexpose

Yule kipara mwenda zake mechi kama hii alikuwa anawabamiza tena
hawa PSG
Game management na playing style inayoendana na resource bado ni mtihani kwa kocha na SD

Playing from back kwa kipa na mabeki wasio na uwezo wa kucarry mpira ni red flag kwa kocha lazima mmoja ampishe mwenzake
Mechi ilikuwa nzuri kwa Chelsea, kama kuna kosa kumuweka Jorgensen golini
 
Muondoe THE BLUES hapo hawezi fanya come back. Ameshatolewa
Chelsea na Rosenior watawashangaza sana, tusubiri tuone.
Naona hapa kuna come back kama moja au mbili
  1. Tottenham Hotspur 2-5
  2. Chelsea 2-5
  3. Man City 0-3
Aidha mji wa Manchester au London wiki ijayo tutegemee comeback kama ile ya:
  1. Liverpool 4–0 Barcelona (2019)
  2. Chelsea vs Napoli (2012)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom