Sikuweza kufuatilia mechi yote jana, lakini kwa kweli, kama wamiliki hawataziba mapengo haya kwenye dirisha lijalo la usajili, basi wanapaswa kuachia ngazi.
Tunahitaji mjadala mzito kuhusu nafasi ya golikipa. Huwezi kushindania mataji kama EPL au UCL ukiwa na makipa kama Sánchez na Jørgensen. Tofauti kubwa kati ya Jørgensen na Sánchez iko kwenye uwezo wa kuokoa mashuti—ni kama Jørgensen haoni kabisa mashuti yakipigwa. Sitaki tena kumuona Jørgensen akianza kwenye mechi kubwa za ligi au UCL. Mungu apishe mbali. Amina.
Tunapaswa kumsajili beki ambaye si wa kubahatisha—kiongozi wa kweli wa kuja kushirikiana na Colwill. Waliobaki wabaki kuwa backups au waondoke.
Chelsea walikuwa bora kuliko PSG kwenye karibu kila idara jana, lakini makosa ya makipa na mabeki ndiyo yametufikisha hapa tulipo.
Gameplan ya Rosenior pia haujakaa imara kama wa Maresca, hasa kwenye mechi kubwa kama hizi. Sikuona mkakati wowote wa kuwapress PSG hadi washindwe kucheza mpira wao. Hakukuwa na mpango wa kuwadhibiti wachezaji hatari wa PSG kama Dembélé au Kvaratskhelia.
Kama tungeweza kudhibiti uzembe wa jana, matokeo yangekuwa 2–2, au hata kama tungefungwa, labda 3–2. Baadhi ya yale magoli yalikuwa yanazuilika kabisa kama mabeki wangekuwa imara.
Sasa tunadaiwa magoli matatu, tuna chini ya siku sita kujiandaa kwa mchezo wa marudiano Stamford Bridge—na bado tuna Newcastle wikiendi hii kwenye mechi kubwa ya PL ya kupigania nafasi ya top 4.