Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Hua mnaoverestimate uwezo wa timu kiasi kwamba hua mnaandika kwa kuzingatia overestimation. Katika mashabiki wote ni mmoja tu niliona ameaddress ishu ya kweli juu ya mabeki.

Alikua Kimbukiko wengine wote ilikua ni kuishi historia.
 
Kenge kama kenge .... mmmbanduliwe tu mtolewe, goli 5 nyingi sana kuchomoa ngumu sana, washambuliaji wenyewe ndio kina Delap ? Hata ukimpa pasi nzuri hawezi kupokea mali ikakaa mguuni vizuri !!!

J Pedro nae takataka....ana upepo tu, sio mchezaji wa level ya Timu kubwa ya champions league. .....
Msisahau kwenye ligi big 4 mmpambane, vinginevyo mwakani mtashiriki conference league
 
Huyu kipa kiazi alichofanya leo n Sawa na alichofanya Loris Karius akiwa Liverpool Kwenye fainali ya uefa dhidi ya Madrid
Wewe uliona alichokifanya kipa wa Tottenham juzi wakicheza dhidi ya Atletico Madrid?
Bora hata huyu wenu
 
Delap akiwa uwanjani ni kama mpo 10 tu .... hana msaada wowote, sio link up play, sio kusumbua mabeki wa timu pinzani, wala pasi nzuri..... lijamaa ni hewa,,,, kocha nae kiazi kila siku anapambana anampa minutes
 
Leo nimeamka nikiwa mnyonge, nimekata tamaa, sina nguvu wala hamu ya kufanya hata yale mambo ninayoyapenda. Sikuelewa tatizo ni nini mpaka baadaye nikakumbuka kuwa jana Chelsea walicheza… na wakafungwa na wale legelege PSG. Sasa sisi mashabiki furaha yetu itatoka wapi kama hata PSG tunashindwa kuwapiga. Tunarudi Stamford Bridge tukihitaji ushindi wa 4–0 ili kuwatoa kwenye UCL. Kwa hali hii, Chelsea inabaki na tofauti gani na Tottenham au Man City.
 
Sikuweza kufuatilia mechi yote jana, lakini kwa kweli, kama wamiliki hawataziba mapengo haya kwenye dirisha lijalo la usajili, basi wanapaswa kuachia ngazi.

Tunahitaji mjadala mzito kuhusu nafasi ya golikipa. Huwezi kushindania mataji kama EPL au UCL ukiwa na makipa kama Sánchez na Jørgensen. Tofauti kubwa kati ya Jørgensen na Sánchez iko kwenye uwezo wa kuokoa mashuti—ni kama Jørgensen haoni kabisa mashuti yakipigwa. Sitaki tena kumuona Jørgensen akianza kwenye mechi kubwa za ligi au UCL. Mungu apishe mbali. Amina.

Tunapaswa kumsajili beki ambaye si wa kubahatisha—kiongozi wa kweli wa kuja kushirikiana na Colwill. Waliobaki wabaki kuwa backups au waondoke.

Chelsea walikuwa bora kuliko PSG kwenye karibu kila idara jana, lakini makosa ya makipa na mabeki ndiyo yametufikisha hapa tulipo.

Gameplan ya Rosenior pia haujakaa imara kama wa Maresca, hasa kwenye mechi kubwa kama hizi. Sikuona mkakati wowote wa kuwapress PSG hadi washindwe kucheza mpira wao. Hakukuwa na mpango wa kuwadhibiti wachezaji hatari wa PSG kama Dembélé au Kvaratskhelia.

Kama tungeweza kudhibiti uzembe wa jana, matokeo yangekuwa 2–2, au hata kama tungefungwa, labda 3–2. Baadhi ya yale magoli yalikuwa yanazuilika kabisa kama mabeki wangekuwa imara.

Sasa tunadaiwa magoli matatu, tuna chini ya siku sita kujiandaa kwa mchezo wa marudiano Stamford Bridge—na bado tuna Newcastle wikiendi hii kwenye mechi kubwa ya PL ya kupigania nafasi ya top 4.
1773304201463.png
 
Naona hapa kuna come back kama moja au mbili
  1. Tottenham Hotspur 2-5
  2. Chelsea 2-5
  3. Man City 0-3
Aidha mji wa Manchester au London wiki ijayo tutegemee comeback kama ile ya:
  1. Liverpool 4–0 Barcelona (2019)
  2. Chelsea vs Napoli (2012)
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom