Ila sijawahi kuona mchezaji mbinafsi na asiye na maamuzi sahihi kama Nicolas Jackson. Chelsea haijawahi kumkataa. Amepewa miaka miwili akiwa boss wa nafasi yake, akicheza kila wiki bila presha. Sasa timu imesajili washindani wa kumpa changamoto, badala ya kupambana, amekasirika na kutaka kuondoka.
Chelsea ikamkubalia, ikamwekea bei kubwa—lakini badala ya kuonyesha shukrani, amejiona kama Messi, akaongeza kiburi juu. Timu inazama, tunahitaji msaada, lakini yeye anafurahia kuzama kwa jahazi. Kagoma kurudi, wakati hata ule ulikuwa ni mkopo tu bila obligation ya kumnunua.
Chelsea wako sahihi. Kama ni hivyo, Bayern Munich walipe hiyo milioni 80 tuachane na huyu mwoga na mbinafsi. Nasema hivi kwa hasira, kwa sababu wakati mashabiki wengine walimuita “takataka,” sisi tulimtetea kwa nguvu zote. Tulimwamini. Tulimpenda.
A real coward. Sijui kama angekuwa kwenye nafasi ya Trevoh Chalobah, angefanyeje. God forbid.
Chelsea wanapaswa kutumia muda huu kulazimisha Bayern Munich wamnunue kabisa, au waweke clause ya obligation to buy—ili tuachane naye kabisa. Hatufai tena.