Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

UEFA wameitahadharisha Chelsea na Aston Villa kuwa swap yeyote itakayoambatana na inflated price za wachezaji watapewa adhabu stahiki. Chelsea na Aston Villa wanaweza kufanya swap deal ya wachezaji nahisi ni Morgan Rodgers na Jackson au Nkunku

View attachment 3410894
Kama ni hivyo sijui itakuaje ila namuona Morgan anaweza aisipate number ingawa nimchezaji mzuri kwasababu nafasi yake anacheza Cole Palmer
 
🚨🇮🇹 Gianni Infantino: “Tuzo ya Ballon d'Or ya mwaka huu itaathiriwa kwa kiasi kikubwa na kiwango kilichoonyeshwa kwenye Kombe la Dunia la Klabu. Mchango wa wachezaji kwenye mashindano hayo utakuwa na uzito mkubwa.”
 
🚨🇮🇹 Gianni Infantino: “Tuzo ya Ballon d'Or ya mwaka huu itaathiriwa kwa kiasi kikubwa na kiwango kilichoonyeshwa kwenye Kombe la Dunia la Klabu. Mchango wa wachezaji kwenye mashindano hayo utakuwa na uzito mkubwa.”
Tayari hapo mshindi ameshajulikana
 
  • Thanks
Reactions: K11
FIFA sasa wamebadilisha majina ya washindi wote wa awali wa Kombe la Dunia la Vilabu kuwa sasa "Mabingwa wa Mabara wa FIFA" - FIFA inatambua Chelsea kuwa Mabingwa wa Dunia pekee.
1752949583169.png
 
Kama ni hivyo sijui itakuaje ila namuona Morgan anaweza aisipate number ingawa nimchezaji mzuri kwasababu nafasi yake anacheza Cole Palmer
Kocha msimu huu atawarotate sana kwa sababu mchezaji mzuri hawezi kuozea benchi. Ndio maan kwenye CWC alisema anajaribu mifumo mipya. Kwenye mechi tuliyofungwa na Flamengo alifanya hivyo. Palmer kacheza LW na RW. Pia wachezaji karibu wote isipokuwa Jackson wanaweza kucheza zaidi ya nafasi moja akiwemo Rodgers kama atakuja anaweza cheza No. 10/CAM/RW/LW
 
Kocha msimu huu atawarotate sana kwa sababu mchezaji mzuri hawezi kuozea benchi. Ndio maan kwenye CWC alisema anajaribu mifumo mipya. Kwenye mechi tuliyofungwa na Flamengo alifanya hivyo. Palmer kacheza LW na RW. Pia wachezaji karibu wote isipokuwa Jackson wanaweza kucheza zaidi ya nafasi moja akiwemo Rodgers kama atakuja anaweza cheza No. 10/CAM/RW/LW
Kwenye Lw hapa atakuwa ana namba ya kudumu
 
Alafu kuchukua hilo kombe kusiwadanganye kuwa Chelsea iko imara kuzi challenge Liverpool na Man City kwenye ligi. Chelsea bado sana inabidi tutoe matakataka kuanzia Kocha.
Msimu wake wa Kwanza tu huu wa Enzo Maresca tumeingia big 4 baada ya kustruggle kwa miaka miwili kwa makocha tofauti Lamps, potter na pochentino, kabeba conference cup na mwisho kashinda kombe la club bingwa kwa kutoa dozi Nene Real Betis kala 4 vizuri, PSG kala 3 takatifu hivi uoni Kama tumepiga hatua kubwa? Anakuaje ni takataka?
 
Alafu kuchukua hilo kombe kusiwadanganye kuwa Chelsea iko imara kuzi challenge Liverpool na Man City kwenye ligi. Chelsea bado sana inabidi tutoe matakataka kuanzia Kocha.

Hatuwezi kuendelea kubadilisha makocha kila mara. Mojawapo ya mambo ninayompenda Enzo Maresca ni jinsi alivyoelewana vyema na wamiliki pamoja na uongozi wa klabu. Unaweza kumleta kocha mwenye hadhi kama Luis Enrique au Hansi Flick, lakini ikiwa hatakuwa na maelewano na viongozi wa juu, mambo yanaweza kwenda kinyume cha matarajio.

Kitu muhimu ni kwamba timu iboreshwe kulingana na mapendekezo ya kocha. Wachezaji wasiotoa mchango thabiti wanaondolewa hatua kwa hatua, na wale wapya wasiofaa pia wataondolewa kadri muda unavyokwenda hadi Chelsea iwe na kikosi chenye uwezo wa kushindania Ligi Kuu ya England (EPL) na Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL).

Ninaamini kuwa usajili wa msimu huu umefanikiwa kupunguza pengo kubwa lililokuwapo kati ya Chelsea na Liverpool. Kadhalika, pengo baina ya Chelsea na Manchester City na Arsenal limefutwa. Tutapambana nao kwa nguvu sawa—jino kwa jino, mguu kwa mguu, na pointi kwa pointi. Ikiwa usajili wa Liverpool msimu huu wa kina Florian Wirtz, Hugo Ekitike, Jeremie Frimpong, na Milos Kerkez hautazaa matunda kama walivyotarajia, tutawazidi na kuwapiku.
 
Binafsi huwa naamini THE BLUES ipo vizuri kwenye mashindano ya mtoano kuliko ya EPL mbio ndefu za kukusanya point.

Sitashangaa msimu ujao tukabeba UCL

Kwa ajili ya kudumisha utulivu wa kiwango cha mchezo, nimegundua kuwa kushuka kwa ubora wa Cole Palmer kulitokana na mgogoro wa kimahusiano kati yake na mchumba wake, Connie Grace. Kwa sasa, kuna taarifa kuwa wamefanyiana block kwenye Instagram, jambo linaloashiria kuwepo kwa mvutano mkubwa. Mwezi Januari, niliandika kwa kubahatisha kwamba huenda Palmer hachezi vizuri kwa sababu ya matatizo ya kifamilia, na baadaye ikathibitika kuwa ni kweli.

Hali kama hiyo iliwahi kumkumba Enzo Fernández, ambaye kiwango chake kilishuka alipokuwa na mgogoro na mke wake. Walipopatana, aliweza kurejea katika ubora wake wa awali. Naam, naamini kwamba Palmer akiyarejesha mahusiano yake katika hali ya amani, utulivu wake wa kiakili utarudi na kiwango chake kitaimarika katika msimu mzima.

Mbali na hilo, usajili wa washambuliaji wawili wenye uwezo mkubwa kuliko Nicolas Jackson wa Liam Delap na Joao Pedro unatarajiwa kuondoa tatizo la ukosefu wa mabao lililoikumba timu msimu uliopita. Safu ya ulinzi pia imeimarika sana, hata kwa wachezaji wa akiba, hivyo Chelsea ina nafasi ya kuwa na moja ya ngome imara zaidi msimu ujao.

Kurejea kwa Andrey Santos pamoja na usajili wa Mahamoud Sar, Jamie Gittens, na Estevão Willian kutatoa mchango mkubwa katika kuongeza ubunifu na hatari katika safu ya kati na ya mbele. Na iwapo tutafanikiwa kumsajili Jorrel Hato, Morgan Rogers au Xavi Simons, bila shaka dirisha hili la usajili litakuwa mojawapo ya madirisha bora kabisa ya hivi karibuni.
 
Binafsi huwa naamini THE BLUES ipo vizuri kwenye mashindano ya mtoano kuliko ya EPL mbio ndefu za kukusanya point.

Sitashangaa msimu ujao tukabeba UCL
Kabla ujaongea hivyo itathimini team kwa ujamla na jiulize Nini sababu ilitufanya tu struggle hapa katikati, ukishafanya hiyo tathimini ndio itakupa picha halisi ya mwelekeo wa team ngoja Sasa nikupe majibu. Moja Kati ya changamoto kubwa team ilikuwa nayo ni kuwa tunaruhusu magoal lakini pia mbele tupo butu, alivyokuja Maresca hapa mwanzoni na katikati bado tulikuwa tunashida za kuruhusu magoal ingawa tulikuwa tunacheza vizuri but karibia na hizi mechi za mwisho za epl tukaimarika kwenye defense sana na tulikuwa tunafunga lakini sio sana kwasababu tunapoteza chance nyingi za kufunga mbele.

Nakukumbusha katika mechi 15 za mwisho tumeshinda mechi 14 na katika hizi mechi za mwishoni mwa ligi tumeruhusu magoal machache sana hiyo ndio namna unaona improvement ya team, kushinda kwa hili kombe imetengeneza positive mentality na spirit ya wachezaji na hii imeanzia baada ya kushinda conference cup wachezaji watakuwa na high demand ya kudai mafanikio.Nini Chelsea wamekifanya baada ya kumaliza ligi?
Jibu ni kwamba tumeanda sokoni kuimarisha mbele tumemsajili Joao Pedro na umeshaona deliver yake, tumemsajili pia Delap ambao ni mastrikers wazuri maana kwenye mechi tulizokuwa tunapoteza sio kwasababu tulikuwa tunazidiwa na wapinzani la hasha! Tunacheza vizuri ila the end tunapoteza game na ukiangalia hiyo game tumetengeneza nafasi nyingi kuliko mpinzani.Kingine tulichofanya ni kuimarisha depth ya kikosi sasa hivi tunaweza kumkosa Caicedo nafasi yake ikachezwa na Essugo na Usione gape kubwa maana Essugo ni kiungo mzuri na hivyo hivyo tumefanya kwa maeneo mengine na bado tunaendelea na usajili kwa namna hii unawezaje kusema hatuwezi ku wachallenge Liverpool na Man city???
Papaa Gx
 
Kwa ajili ya kudumisha utulivu wa kiwango cha mchezo, nimegundua kuwa kushuka kwa ubora wa Cole Palmer kulitokana na mgogoro wa kimahusiano kati yake na mchumba wake, Connie Grace. Kwa sasa, kuna taarifa kuwa wamefanyiana block kwenye Instagram, jambo linaloashiria kuwepo kwa mvutano mkubwa. Mwezi Januari, niliandika kwa kubahatisha kwamba huenda Palmer hachezi vizuri kwa sababu ya matatizo ya kifamilia, na baadaye ikathibitika kuwa ni kweli.

Hali kama hiyo iliwahi kumkumba Enzo Fernández, ambaye kiwango chake kilishuka alipokuwa na mgogoro na mke wake. Walipopatana, aliweza kurejea katika ubora wake wa awali. Naam, naamini kwamba Palmer akiyarejesha mahusiano yake katika hali ya amani, utulivu wake wa kiakili utarudi na kiwango chake kitaimarika katika msimu mzima.

Mbali na hilo, usajili wa washambuliaji wawili wenye uwezo mkubwa kuliko Nicolas Jackson wa Liam Delap na Joao Pedro unatarajiwa kuondoa tatizo la ukosefu wa mabao lililoikumba timu msimu uliopita. Safu ya ulinzi pia imeimarika sana, hata kwa wachezaji wa akiba, hivyo Chelsea ina nafasi ya kuwa na moja ya ngome imara zaidi msimu ujao.

Kurejea kwa Andrey Santos pamoja na usajili wa Mahamoud Sar, Jamie Gittens, na Estevão Willian kutatoa mchango mkubwa katika kuongeza ubunifu na hatari katika safu ya kati na ya mbele. Na iwapo tutafanikiwa kumsajili Jorrel Hato, Morgan Rogers au Xavi Simons, bila shaka dirisha hili la usajili litakuwa mojawapo ya madirisha bora kabisa ya hivi karibuni.
Kumbe hadi Xavi Simons nae tunataka kumsajili? Timu itakuwa nzuri sana safu ya ushambuliaji
 
Ili kikosi kiwe kizuri zaidi
1. Jackson akiondoka, msaidizi wa Palmer atafutwe.
2. Jackson akibaki, hivyo kocha amfanye acheze nyuma ya mshambuliaji ili awe mgawa mipira make hapo yupo vizuri sana.
3. Msaidizi wa Cucurella atafutwe.
Mawinga wetu...Netopia, Gittens, Estavao, George pia Joao Pedro anaweza kucheza nafasi hizo. Sasa ni wakati wa timu kutulia
 
Ili kikosi kiwe kizuri zaidi
1. Jackson akiondoka, msaidizi wa Palmer atafutwe.
2. Jackson akibaki, hivyo kocha amfanye acheze nyuma ya mshambuliaji ili awe mgawa mipira make hapo yupo vizuri sana.
3. Msaidizi wa Cucurella atafutwe.
Mawinga wetu...Netopia, Gittens, Estavao, George pia Joao Pedro anaweza kucheza nafasi hizo. Sasa ni wakati wa timu kutulia
Jackson awe back_up ya Palmer au atokee Winga kama tutapata majeruhi.
 
Hapa mtaani kwangu wamepotea, hasa Arsenal na Liverpool, aibu yao hawaonekani mtaani asubuhi ya kuamkia jana. Na naamini leo wakionekana watajifanya hakuna kilichotokea duniani kwa upande wa Chelsea.
Wao Arsenal walikuwa mstari wa mbele kuishambulia Chelsea na kuyaita mashindano ni pre-seaosn yenye kombe.
Liverpool wao walikuwa mstari wa mbele kuyashambulia haya mashindano wakidai ni mashindano ya hovyo kuwahi kutokea. Ila utashangaa mashindano ya 2029 watapambana kufa na kupona wawepo na kuzima data kana kwamba hawajawahi kuyadharau
Walitatamni wawepo lakini haikuwa bahati yao. Waliulize kama ni kombe la ovyo Bigwa Club world Cup amepewa kiasi gani cha fedha. Wanatamani lakini hawana uwezo huo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom