Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Ndg umejibu kwa kuchambua vizuri
Pochettino alisaini mkataba wa miaka miwili tu
Pochettino alikatiziwa mkataba wake kwa sababu alianzisha ubishi na uongozi, wamiliki wakaona hayuko tayari kufanya nao kazi kama teammate, alitaka mamalaka zaidi kwenye usajili na uuzwaji wa wachezaji, hili likapingana na maono na muelekeo wa uongozi kwenye hii project
Changamoto kubwa iliyoko kwenye uongozi kwa sasa ni kutosajili kwa kuchanganya wachezaji wenye umri mkubwa na uzoefu, wanaosajiliwa wote ni watoto wanaohitaji muda
Ila kwa upande wa usajili mimi sina shutuma juu yao, wachezaji tulionao ni wazuri na chini ya uongozi muafaka tutavuna tunachokipanda
Kinachowachanganya wengine wasiojua dynamics za soka humu ni kwamba walidhani ubora wa timu mwisho wa ligi utaendela mwanzoni bila kutilia maanani kuwa kocha ni mpya, mfumo ni mpya na wachezaji bado ni wale wale wachanga a,mbao wanajitahidi kuzoea ligi na consitency.
Mimi naamini wachezaji wote wakiwa fit, na kocha akajua naman ya kuwapanga, kuwatumia na mazoezi, timu itashindania top 4, hilo sina shaka nalo
Hapo kwa Petrovic ni ngumu mkuu, ingekuwa hivyo makocha wangekuwa wanawafundisha, ndio maana sio kila mchezaji anaendana na style flan ya uchezaji,

Petrovic na Jorgensen hawalingani

Petrovic anaweza kuwa anamzidi Sanchez kwenye shot stopping
Niliangalia mpira dk 90 zote nilichogundua ni haya:
1. Sanchez siyo kipa wa kutegemewa, long ball zote alizipiga nje.
2. Sanchez alichelewa kutoa maamuzi ya kuanzisha mashambulizi na pindi akianzisha mashambulizi lazima apeleke mpira kwenye uelekeo usiyo sahihi.
3. Levia na Chukuemeka hawawezi kusimama sehemu ya kiungo, Levia ni mzito sana...kila mara alikuwa nyuma ya adui pale timu ikipoteza mpira kitu kilichosababisha walinzi kupata shida sana kwasababu hawakuwa na usaidizi.
4. Levi Colwil hqwezi upande wa left back, sijui shida ni nini asiwekwe katikati.
5. Badiashile ile style yake ya kusimama juu ya mpira sijui alijifunzia wapi...anapoza mpira alafu anakuwa mzito kuanzisha mashambulizi, either apigwe benchi au abadilishe namna ya uchezaji, hakuna timu ya kumchukuwa kwa mkopo.
6. James hajakaa sawa, Jana alikuwa anachelewa sana kurudi kufanya recovery pindi timu ikiwa inashambuliwa.
7. Modrik amebadilisha nywele ila hajabadilika.
8. Madueke akiongeza umakini ni mchezaji mzuri.
9. Marc Geui ni mchezaji mzuri sana, kila wakati alikuwa sehemu sahihi.
nadhani kwa lavia nahisi ni kwa sababu ya kuwa nje mda mrefu ,
 
Chelsea wako tayari kuwaruhusu hadi wachezaji 12 zaidi kuondoka msimu huu:
  1. Conor Gallagher
  2. Trevoh Chalobah
  3. Đorđe Petrović
  4. Ben Chilwell
  5. Kepa Arrizabalaga
  6. Romelu Lukaku
  7. Lesley Ugochukwu
  8. Armando Broja
  9. Cesare Casadei
  10. David Datro Fofana
  11. Harvey Vale
  12. Leo Castledine
(Chanzo: Sun Sport)

Nini maoni yako
Hapo kuna wachezaji sidhan ht kama waliwahi kucheza na kama wamecheza bc hawajafikisha ht mechi 5.
 
Kumbe Disasi kama Enzo walicheza wakiwa na hernia msimu uliopita na sasa kafanyiwa upasuaji na anaendelea kupona

1722196005864.png
 
Nawajulisha kwamba mchezaji Filip Jørgensen amesafiri jioni ya leo kuelekea Marekani ili kusaini mkataba nchini Marekani ili kujiunga na kikosi cha Enzo Maresca kwenye ziara ya maandalizi ya msimu mpya.

Ofa ni hadi Juni 2030 pamoja na chaguo hadi 2031

@fabrizioromano

1722196883058.png
 
Je, unajua kuwa Celtic walicheza michezo 5 mwezi Julai, wakashinda 4 na kutoka sare moja?
Je, unafahamu kuwa katika michezo yote mitano walifunga mabao 19 na kufungwa 9 pekee
Je, unajua pia kwamba Man city walipoteza mechi zao zote mbili za preseason dhidi ya Celtic na AC Milan?
Kufungwa siyo shida kubwa. Shida ni kuruhusu magoli 4
 
Uchambuzi wa kuwachezesha wachezajki nje ya nafasi zao hasa James na Gusto

 
Kufungwa siyo shida kubwa. Shida ni kuruhusu magoli 4
Na mimi sioni shida kwa sababu tatizo linajulikana, uzembe uzembe
magoli mawili mabeki wanachelewa kurudi kuweka shape ya ulinzi na Enzo kalielezea hilo hivyo mimi sioni shida
Goli la tatu ni la Badisahile, akitupwa nje ya XI hatatutosa tena
Goli la nne Madueke alipoteza posseion kizembe na pia mabeki walikawia kurudi nyuma kuweka defensive shape.
Ttaizo la kufunga magoli jana tulikuw ana bahati mbaya, kosa kosa zilikuwa nyingi, kipa kaokoa. gonga nguzo nk
 
Tulikuwa na mikwaju 23 (mikwaju 10 iliyolenga goli),
iligonga nguzo za goli mara 2 dhidi ya Celtic, na bado tukaweza kufunga penalti moja pekee.
Umaliziaji wetu ulikuwa duni na ulinzi wetu ulikuwa mbaya zaidi.
1722198828294.png
 
Sijui watu wanalalamika nini? Ukiangalia timu inavyocheza unaona kuna kitu mwalimu anakifundisha sema tu wachezaji hawajafahamu namna ya kufanyia kazi mafunzo ya mwalimu.

Uzuri mwalimu ameshaona shida ipo kubwa sana wakiwa hawana mpira. Wanaacha magape. Hata wakipress wanapitika kirahis sana.
 
Sijui watu wanalalamika nini? Ukiangalia timu inavyocheza unaona kuna kitu mwalimu anakifundisha sema tu wachezaji hawajafahamu namna ya kufanyia kazi mafunzo ya mwalimu.

Uzuri mwalimu ameshaona shida ipo kubwa sana wakiwa hawana mpira. Wanaacha magape. Hata wakipress wanapitika kirahis sana.
Mara nyingi hili gape kubwa linatokea kama pairing sio nzuri

Kuna tatizo sehemu ya nyuma, mabeki wote tulionao hawana uzoefu wa kusoma mashambulizi na kuwa kwenye njia yenye hatari kwa wakati sahihi kama alivyokuwa akifanya Silva. Chalobah alianza kujua kusoma moves za mashambulizi na sasa anauzwa. Tuna tatizo kubwa katika ulinzi

Sioni hata moja kati ya haya; Fofana, Tosin, Disasi, Badiashile, Colwill ambao wanaweza kubeba jukumu hilo zaidi ya Chalobah. Ikiwa anauzwa, basi beki mwenye uzoefu na wasifu huo au juu ya hapo anapaswa kununuliwa, vinginevyo, Maresca atahangaika sana na mabeki hawa tulionao.

Kwenye safu ya kiungo, sina tatizo, tunajitosheleza kwa options.

Hata kwa washambuliaji, sina shida sana hata tusiposajili striker. Nadhani msimu huu utakuwa mzuri kwa Sterling na atavutia msimu huu kwa sababu namuona anaendana sana na mfumo wa Marseca.
 
Chelsea fc ni bingwa wa epl msimu huu akipatikana beki mmoja kiongozi...mengine tutasema mwisho wa msimu.
 
Mara nyingi hili gape kubwa linatokea kama pairing sio nzuri

Kuna tatizo sehemu ya nyuma, mabeki wote tulionao hawana uzoefu wa kusoma mashambulizi na kuwa kwenye njia yenye hatari kwa wakati sahihi kama alivyokuwa akifanya Silva. Chalobah alianza kujua kusoma moves za mashambulizi na sasa anauzwa. Tuna tatizo kubwa katika ulinzi

Sioni hata moja kati ya haya; Fofana, Tosin, Disasi, Badiashile, Colwill ambao wanaweza kubeba jukumu hilo zaidi ya Chalobah. Ikiwa anauzwa, basi beki mwenye uzoefu na wasifu huo au juu ya hapo anapaswa kununuliwa, vinginevyo, Maresca atahangaika sana na mabeki hawa tulionao.

Kwenye safu ya kiungo, sina tatizo, tunajitosheleza kwa options.

Hata kwa washambuliaji, sina shida sana hata tusiposajili striker. Nadhani msimu huu utakuwa mzuri kwa Sterling na atavutia msimu huu kwa sababu namuona anaendana sana na mfumo wa Marseca.
Tumpe muda tusijudge kwa mechi mbili za pre season, huwezi kujua akafanyia kazi makosa ya beki wake.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom