Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Uongozi wa team ujui unataka nini ndio tatizo kubwa tulionao na litatutesa sana
Uongozi unajua unachotaka ni vile sisi mashabiki hatutaki kubadilika tunaishi katika zama za miaka ya nyuma za kutaka big names, while soka sasa hiv aliangalii hilo.

Ingekuwa hawajui wanataka nini wasingefanya investment yoyote au hata poch asingetimuliwa.

Sisi mashabiki ni watu rahisi sana katika kuhukumu tunasahau malengo ya pre season ni yapi.

Form ya pre season huwa sio hata ya kuiangalia bali ni sehem ya kuangalia wapi unahitaji kurekebisha au ufanye maboresho.

Nani anakumbuka
Pre season ya lampard 2nd season
Pre season ya Poch
Pre season ya Carlo ancellot akiwa kocha wetu
Lampard na Poch walikiwa na pre season nzuri ila kwenye league yaliyotokea mmmh
Carlo alikuwa na pre season mbov ila kwenye league alienda kuwa bingwa

Wachezaj waliofanya vizuri pre season
Kenedy,Batshuay,Marko Marin,Wallace, etc ila league zilivyoanza hakuna aliyekuwa anatamani kuwaona


Ushindi wa kwenye pre season huwa sio hata kuufurahia ni kama unakufumbaza, ila ni better upoteze ili ujue wapi unatakiwa kurekebisha
 
ila ni better upoteze ili ujue wapi unatakiwa kurekebisha
Nimeipenda hiyo ya "ni better upoteze ili ujue wapi unatakiwa kurekebisha"
Preseason ni kama mazoezi ya kuingia vitani. Bora kushindwa wakati wa mazoezi kuliko kushindwa vitani
 
Hii picha inakupa ujumbe gani The Blues
1722164900173.png
 
Maresca: "Wazo na Marc na wachezaji wote wachanga ni kuangalia kisha kuamua kama tuwatoe kwa mkopo au la. Kwa sasa Marc atabaki na hatakwenda popote”
1722165582176.png
 
Nimeangalia highlights za mechi ya jana , qmamae hamna timu hapa .
Narudia hatuna timu
usihukumu kitu hapa kwa sababu waliocheza sio Chelsea halisi. Kocha anapata takwimu na wapi pa kurekebisha. Ilitakiwa iwe hivyo ili timu iandaliwe bila kujidanganya
 
Mimi huwa kama kocha simjui huwa namuunga mkono hadi nimjue vizuri. Kwenye preseason huwezi kumjua kocha hadi ligi ianze na acheze mechi kadhaa angalau hadi Desemba ndipo utamjua kama atatufikisha nchi ya ahadi au la
 
Uongozi unajua unachotaka ni vile sisi mashabiki hatutaki kubadilika tunaishi katika zama za miaka ya nyuma za kutaka big names, while soka sasa hiv aliangalii hilo.

Ingekuwa hawajui wanataka nini wasingefanya investment yoyote au hata poch asingetimuliwa.

Sisi mashabiki ni watu rahisi sana katika kuhukumu tunasahau malengo ya pre season ni yapi.

Form ya pre season huwa sio hata ya kuiangalia bali ni sehem ya kuangalia wapi unahitaji kurekebisha au ufanye maboresho.

Nani anakumbuka
Pre season ya lampard 2nd season
Pre season ya Poch
Pre season ya Carlo ancellot akiwa kocha wetu
Lampard na Poch walikiwa na pre season nzuri ila kwenye league yaliyotokea mmmh
Carlo alikuwa na pre season mbov ila kwenye league alienda kuwa bingwa

Wachezaj waliofanya vizuri pre season
Kenedy,Batshuay,Marko Marin,Wallace, etc ila league zilivyoanza hakuna aliyekuwa anatamani kuwaona


Ushindi wa kwenye pre season huwa sio hata kuufurahia ni kama unakufumbaza, ila ni better upoteze ili ujue wapi unatakiwa kurekebisha
Wakati wanamsajili poche walimpa mkataba mrefu na jukumu la kutengeneza team mwishoni team ikaanza kujipata wakamfukuza hiyo ni sign ya kutokujitambua. Tumemuuza Thiago silva hatusikii kabisa team inampango wa kuziba nafasi yake badala yake kuna dogo kasajiliwa but atabakia Bocajunior kwa mkopo wakati tuna uhitaji huo mkubwa, unataka kumuuza Chalobah ambaye ameperform vizuri sana msimu uliopita but unawabakisha Bachiashile na Dissasi hii ina maana gani?

Tumemsajili tu msimu uliopita Petrovic leo unasikia wanataka kumuuza wakati huyu kijana katubeba sana msimu uliopita eti kwa kigezo sio mzuri kwenye footwork wakati huo huo unampa nafasi Sanchez kama kipa no 1 ambaye anamakosa mengi kwenye footwork ndio tunaambiwa kamzidi Petrovic hii inatoa taswira gani kwa uongozi inajua kweli inachofanya?
 
Wakati wanamsajili poche walimpa mkataba mrefu na kujukumu la kutengeneza team mwishoni team ikaanza kujipata wakamfukuza hiyo ni sign ya kutokujitambua. Tumemuuza Thisgo silva hatusikii kabisa team inampango wa kuziba nafasi yake badala yake kuna dogo kasajiliwa but atabakia Bocajunior kwa mkopo wakati tuna uhitaji huo mkubwa, unataka kumuuza Chalobah ambaye ameperform vizuri sana msimu uliopita but unawabakisha Bachiashile na Dissasi hii ina maana gani?

Tumemsajili tu msimu uliopita Petrovic leo unasikia wanataka kumuuza wakati huyu kijana katubeba sana msimu uliopita eti kwa kigezo sio mzuri kwenye footwork wakati huo huo unampa nafasi Sanchez kama kipa no 1 ambaye anamakosa mengi kwenye footwork ndio tunaambiwa kamzidi Petrovic hii inatoa taswira gani kwa uongozi inajua kweli inachofanya?
Hoja za msingi hasa kuziba pengo la Silva, ulinzi hauko imara kabisa. Petrovi hana tofauti kubwa na kipa wa Villareal ambaye tunamsajili, Petrovic ni mzuri kuliko Sanchez kwenye kulinda goli. Kama ana udhaifu wa kucheza mpira si ni kazi ya kocha wa makipa kumfundisha.; Mbona punda, mbwa nguruwe wanafundishwa na wanaelewa?
 
Wakati wanamsajili poche walimpa mkataba mrefu na jukumu la kutengeneza team mwishoni team ikaanza kujipata wakamfukuza hiyo ni sign ya kutokujitambua. Tumemuuza Thiago silva hatusikii kabisa team inampango wa kuziba nafasi yake badala yake kuna dogo kasajiliwa but atabakia Bocajunior kwa mkopo wakati tuna uhitaji huo mkubwa, unataka kumuuza Chalobah ambaye ameperform vizuri sana msimu uliopita but unawabakisha Bachiashile na Dissasi hii ina maana gani?

Tumemsajili tu msimu uliopita Petrovic leo unasikia wanataka kumuuza wakati huyu kijana katubeba sana msimu uliopita eti kwa kigezo sio mzuri kwenye footwork wakati huo huo unampa nafasi Sanchez kama kipa no 1 ambaye anamakosa mengi kwenye footwork ndio tunaambiwa kamzidi Petrovic hii inatoa taswira gani kwa uongozi inajua kweli inachofanya?
Cha kwanza Thiago Silva hajauzwa, bali mkataba wake uliisha na akataka kwenda kumalizia kwao Brazil
Useme labda tunahitaji beki kiongozi ila sio kuwa tunauhitani wa mabeki
Tuna mabeki 5-6 wakati (Colwill,Badiashile,Disasi,Fofana,Tosin,Achempong)

Huwez sajili beki mwingine bila aliyepo kuondoka

Poch hakusaini mktaba wa muda mrefu alisign kama miaka 2 o 3 kama sijakosea.

kwa chalobah uko sahihi ni mzuri kuliko Disasi ila Disasi mda wote amekuwa akipatikana, na nafasi ya Chalobah amechukua dogo wa Academy Josh Achaempong
Na nafasi ya Chalobah wako wachezaj 4(Tosin Fofana Disasi na Achaempong)

Petrovic ni muhanga wa kocha,If kocha singebadilishwa Petrovic angeendelea kuwepo, Mfano mzuri wakat Pep anakuja City alimkuta Joe Hart yuko kwenye form nzuri ila kwa kuwa hakuwa anaendana na style ya Pep akawa phased out na akamlete Claudio Bravo. Petrovic ni muhanga wa style ya uchezaji Maresca anataka kipa anaeweza kuwa sweeper, anaejua wakati huu nipige long ball au short pass yani anataka kuwa i.e Raya,Onana,Alison,Vicario,Ederson, etc

Issue ya Poch ilikuwa inajulikaba mda mrefu tu kuwa hatokaa aliletwa kutengeneza msingi , ila kwa aina ya wachezaj tulionnao ilikuwa ni tofauti na uchezaji wa poch,

Chelsea now wanataengeneza identity kuanzia academy mpk team mkubwa na hata Strasborg wote kuwe na aina moja ya uchezaji na si hii iliyokuwepo ya kila kocha kuwa na style yake bali team kuwe na style moja inayotambulika hata mchezaji akitoka academy hapati wakat mgumu kwa sasa toka chini anajua team inachezaje
 
Cha kwanza Thiago Silva hajauzwa, bali mkataba wake uliisha na akataka kwenda kumalizia kwao Brazil
Useme labda tunahitaji beki kiongozi ila sio kuwa tunauhitani wa mabeki
Tuna mabeki 5-6 wakati (Colwill,Badiashile,Disasi,Fofana,Tosin,Achempong)

Huwez sajili beki mwingine bila aliyepo kuondoka

Poch hakusaini mktaba wa muda mrefu alisign kama miaka 2 o 3 kama sijakosea.

kwa chalobah uko sahihi ni mzuri kuliko Disasi ila Disasi mda wote amekuwa akipatikana, na nafasi ya Chalobah amechukua dogo wa Academy Josh Achaempong
Na nafasi ya Chalobah wako wachezaj 4(Tosin Fofana Disasi na Achaempong)

Petrovic ni muhanga wa kocha,If kocha singebadilishwa Petrovic angeendelea kuwepo, Mfano mzuri wakat Pep anakuja City alimkuta Joe Hart yuko kwenye form nzuri ila kwa kuwa hakuwa anaendana na style ya Pep akawa phased out na akamlete Claudio Bravo. Petrovic ni muhanga wa style ya uchezaji Maresca anataka kipa anaeweza kuwa sweeper, anaejua wakati huu nipige long ball au short pass yani anataka kuwa i.e Raya,Onana,Alison,Vicario,Ederson, etc

Issue ya Poch ilikuwa inajulikaba mda mrefu tu kuwa hatokaa aliletwa kutengeneza msingi , ila kwa aina ya wachezaj tulionnao ilikuwa ni tofauti na uchezaji wa poch,

Chelsea now wanataengeneza identity kuanzia academy mpk team mkubwa na hata Strasborg wote kuwe na aina moja ya uchezaji na si hii iliyokuwepo ya kila kocha kuwa na style yake bali team kuwe na style moja inayotambulika hata mchezaji akitoka academy hapati wakat mgumu kwa sasa toka chini anajua team inachezaje
Ndg umejibu kwa kuchambua vizuri
Pochettino alisaini mkataba wa miaka miwili tu
Pochettino alikatiziwa mkataba wake kwa sababu alianzisha ubishi na uongozi, wamiliki wakaona hayuko tayari kufanya nao kazi kama teammate, alitaka mamalaka zaidi kwenye usajili na uuzwaji wa wachezaji, hili likapingana na maono na muelekeo wa uongozi kwenye hii project
Changamoto kubwa iliyoko kwenye uongozi kwa sasa ni kutosajili kwa kuchanganya wachezaji wenye umri mkubwa na uzoefu, wanaosajiliwa wote ni watoto wanaohitaji muda
Ila kwa upande wa usajili mimi sina shutuma juu yao, wachezaji tulionao ni wazuri na chini ya uongozi muafaka tutavuna tunachokipanda
Kinachowachanganya wengine wasiojua dynamics za soka humu ni kwamba walidhani ubora wa timu mwisho wa ligi utaendela mwanzoni bila kutilia maanani kuwa kocha ni mpya, mfumo ni mpya na wachezaji bado ni wale wale wachanga a,mbao wanajitahidi kuzoea ligi na consitency.
Mimi naamini wachezaji wote wakiwa fit, na kocha akajua naman ya kuwapanga, kuwatumia na mazoezi, timu itashindania top 4, hilo sina shaka nalo
 
Maresca: "Off the ball, for sure, we need to improve things. You can see sometimes we confuse when we need to play short and when we need to play a little bit longer but that is part of the process."

Yani sio sisi tu ndio tumeona shida iko wapi hata kocha yeye mwenyewe ameona wapi tulipokuwa nashida.
Naamini endapo akiendelea kuona wapi kunashida na akafanyia kazi tutafika nchi ya ahadi.

Dalili ya kwanza ya kocha mzuri ni kujua wapi kwenye shida wakat game ikiwa inaendelea na si kwa indivivual tu bali kwa team nzima. Kuanzia hapo unajua kabisa jinsi ya kuimprove.
 
Niliangalia mpira dk 90 zote nilichogundua ni haya:
1. Sanchez siyo kipa wa kutegemewa, long ball zote alizipiga nje.
2. Sanchez alichelewa kutoa maamuzi ya kuanzisha mashambulizi na pindi akianzisha mashambulizi lazima apeleke mpira kwenye uelekeo usiyo sahihi.
3. Levia na Chukuemeka hawawezi kusimama sehemu ya kiungo, Levia ni mzito sana...kila mara alikuwa nyuma ya adui pale timu ikipoteza mpira kitu kilichosababisha walinzi kupata shida sana kwasababu hawakuwa na usaidizi.
4. Levi Colwil hqwezi upande wa left back, sijui shida ni nini asiwekwe katikati.
5. Badiashile ile style yake ya kusimama juu ya mpira sijui alijifunzia wapi...anapoza mpira alafu anakuwa mzito kuanzisha mashambulizi, either apigwe benchi au abadilishe namna ya uchezaji, hakuna timu ya kumchukuwa kwa mkopo.
6. James hajakaa sawa, Jana alikuwa anachelewa sana kurudi kufanya recovery pindi timu ikiwa inashambuliwa.
7. Modrik amebadilisha nywele ila hajabadilika.
8. Madueke akiongeza umakini ni mchezaji mzuri.
9. Marc Geui ni mchezaji mzuri sana, kila wakati alikuwa sehemu sahihi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom