Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Mnaopenda hii hali ya makocha kutimuliwa mjue hii tofauti kati ya wamiliki hawa na Abramovich

Abramovich alifukuza kocha kwa performance based
Hawa wamiliki wanafukuza kocha kwasababu hawaendani na mradi
Nifafanue ya pili

Akina Todd na Eghbali wanataka kocha ambaye atafuata maelekezo yote yaliyo kwenye Terms of Reference ya project

Barcelona ndio ilikuwa na hii approach ya kuwa na team identity kwenye uchezaji wa timu uwanjani

Changamoto hapa ni kwamba makocha wengi wakubwa wanakuja na style yao ya uchezaji ambao hauendani na wanavyotaka hawa akina Boehly

Hii inadhihirishwa na ukweli kwamba sasa wanataka kocha kijana ambaye akili yake bado flexible haijadumalia kwenye mfumo mmoja

Ndio maana makocha kama akina MOU, Conte hawataweza kamwe kujadiliwa kwenye nafasi hii ya kukochi Chelsea kwa zama hizi.

Kwa maoni yangu hii ni nzuri japo kuitekeleza itakwua na changamoto nyingi sana ya kumpata kocha elite na bado akawa na sifa hizo

PEP Guardiolaanaweza kuwa na sifa hizo ila hapatikani kwa sasa

Xabi Alonso anaweza kuwa na sifa hizo sijui ngoja tuone

Robert De Zerbi anaweza kuwa na sifa hizo ila kwa sasa hatujui

Ngoja tuone
 
Bora tutusa kuliko kuletewa kocha wa Ipswich au Thom Frank😂😂😂
Huwez kujua mkuu, kuna ambae angekubali Xab Alonso aje chelsea kabla hajaenda Leverkusen. Kuliko kubaki na huyo kiazi bora achukuliwe yoyote tu.
 
Tuchel alifukuzwa September 2022 na Enzo alikuja January 2023
Kocha aliyebeba timu kablka ya Lampard alikuwa ni Bruno Saltor kutoka kwenye technical coaches ndani ya Chelsea
Makocha kamili ambao hadi sasa Enzo atakuwa amefundishwa nao ni
  1. Potter
  2. Bruno
  3. Lampard
  4. Pochettino
  5. Kocha mpya
1716361609920.png
 
Furaha yangu itakuwa imekamilika akiletwa kocha ambaye atakuwa upgrade ya Pochettino. Atakayeendana na talents tulionao na kuweza kuwaweka pamoja wakafurahi na kucheza soka la kisasa na kushinda makombe na mechi nyingi tu
 
Changamoto KUBWA ni atakayefuata sasa
Tutegemee a very BIG mistake tena tukaletewa kocha wa kurudi nyuma hadi nyuma ya Potter
Sijui kwanini viongozi Hawajui kujifunza kwa upande wangu sitegemei watamleta kocha wa maana wanataka kocha ambaye atakuwa slave wao kwa kocha anaejielewa hawezi kukubali huu upuuzi
 
Y
Mnaopenda hii hali ya makocha kutimuliwa mjue hii tofauti kati ya wamiliki hawa na Abramovich

Abramovich alifukuza kocha kwa performance based
Hawa wamiliki wanafukuza kocha kwasababu hawaendani na mradi
Nifafanue ya pili

Akina Todd na Eghbali wanataka kocha ambaye atafuata maelekezo yote yaliyo kwenye Terms of Reference ya project

Barcelona ndio ilikuwa na hii approach ya kuwa na team identity kwenye uchezaji wa timu uwanjani

Changamoto hapa ni kwamba makocha wengi wakubwa wanakuja na style yao ya uchezaji ambao hauendani na wanavyotaka hawa akina Boehly

Hii inadhihirishwa na ukweli kwamba sasa wanataka kocha kijana ambaye akili yake bado flexible haijadumalia kwenye mfumo mmoja

Ndio maana makocha kama akina MOU, Conte hawataweza kamwe kujadiliwa kwenye nafasi hii ya kukochi Chelsea kwa zama hizi.

Kwa maoni yangu hii ni nzuri japo kuitekeleza itakwua na changamoto nyingi sana ya kumpata kocha elite na bado akawa na sifa hizo

PEP Guardiolaanaweza kuwa na sifa hizo ila hapatikani kwa sasa

Xabi Alonso anaweza kuwa na sifa hizo sijui ngoja tuone

Robert De Zerbi anaweza kuwa na sifa hizo ila kwa sasa hatujui

Ngoja tuone
Yaani Guardiola aje Chelsea? U can't be serious!!
 
Bodi na wamiliki hawakupenda vitu hivi kwa Pochettino
  1. Sio kocha wa kuposses mpira
  2. Mazoezi na aina ya mafunzo aliyowapa wachezaji ni za kizamani
  3. Mbinu zake zilikuwa zinatia mashaka
  4. Hakuwa na muunganiko na mashabiki
  5. Hawakukubaliana kuhusu mchezaji gani asajiliwe na nani auzwe
  6. Nafasi nyingi zilizokuwa zinakoswa na wachezaji
  7. Uduni kwenye kuweza kucheza set pieces - yaani kuzuia na kufunga magoli
  8. Kumkataa kocha wa set pieces kutoka Brentford
  9. Malalamiko kwenye press conferences na media kuhusu uchanga wa kikosi, ukosefu wa uzoefu nk
6 ni kama wanamuonea tu,

No 1 inabidi na wenyewe wajitafakari tangu mwanzo wanamuappoint.liko wazi kabisa kiwa Poch sio kocha wa kupossess mpira. Sporting Director wajitafakar na wao

Hiyo namba 1 why wanamzungumzia Thom Frank hiv kweli huyu ndie kocha wq kupossess mpira?

Sporting Director nao inabidi waangaliww linapokuja swala zima la kuappoint kocha
 
Chelsea inatafuta kocha wa kisasa na kijana, mahiri ambaye ana sifa hizi nne hapa chini
  1. Kucheza soka la kushambulia
  2. Kucheza soka la kumiliki mpira
  3. Kucheza soka la kuvutia
  4. Awe ni kocha kijana na mbunifu
  5. Anayeweza kujilinda na kutengeneza solid defense
  6. Kuamini vipaji vya vijana walioko kwenye timu kuwatumia na kuwaendeleza
  7. Anayeweza kutenegeneza muunganiko na mahsabiki
@FabrizioRomano
 
Majina yanayohusishwa na kocha mpya wa Chelsea.

Kabla hatujampata kocha mpya tutasikia mengi sana

  • Kieran Mckenna
  • Thomas Frank
  • Eddie Howe
  • Michel
  • Enzo Maresca
  • Sebastien HoeneB
  • Wayne Rooney
 
Majina yanayohusishwa na kocha mpya wa Chelsea.

Kabla hatujampata kocha mpya tutasikia mengi sana

  • Kieran Mckenna
  • Thomas Frank
  • Eddie Howe
  • Michel
  • Enzo Maresca
  • Sebastien HoeneB
  • Wayne Rooney
Hawa wamiliki ni wehu ,bora Dezerbi au Ange Yule kocha wa spurs ,
Ila Ndio hivyo ,sidhani kama wana nature ya kuwa slaves
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom