Kama ilivyo kwa wachezaji hata makocha pia kuna baadhi yao ni wa timu ndogo kwa maana ya kutaka muda kuweza kufit in formation yake kwa wachezaji, kuhandle pressure, kuwin dressing room, lakini pia kusajili wachezaji wake. Sasa wengi wetu kwa ufinyu wa maarifa namna mambo yanavyoenda tunahisi kocha akifanya vizuri timu fulani tunahisi basi hata akienda timu fulani itakua rahisi😂
Tujikumbushe David Moyes na Everton yake walikua moto kweli lakini alipoenda Man Utd mambo yalikwenda hovyo ndani ya msimu mmoja akatolewa, Steven Gerald alipokua Rangers mpaka akabeba ubingwa lakini alipoenda Aston villa mambo yalimwendea kombo akatolewa, Potter yule na Brighton yake alipikuja Chelsea kila mtu akabaki anashangaa.
Wanaochagua makocha wanaangalia mambo mengi sio kirahisi rahisi tu kama tunavyoandika hapa.