Formation haikuwa na matatizo ndg. Hao vijana wamepewa malekezo yaliyobadili uchezaji kipindi cha pili
Sub za hao waliochoka ilitakiwa ifanyike haraka
Tumezamishwa na kocha mpaka mpigiwe wimbo au ngoma ipi muelewa yanayoendelea kwa huyu kocha?
Kimsingi Chelsea kutangulia kupata goli la kuongoza kipindi cha kwanza ni hatari sana kwa sababu kocha anaingia uwanjani kwa mara nyingine na amelekezo ya kuzamisha jahazi, Brentford walikuwa timu ambayo ilishiwa imani, walikuwa waoga na tulimiliki kila idara. Ila style aliyokuja nayo Kocha kipindi cha pili iliwafanya waamini wanaweza kurudi mchezoni. Hili suala ni la kocha sio la wachezaji.
Enzo kachoka ilioneka hata mechi za nyuma, kocha alitakiwa alishughulikie hili
Gallagher naye hakuwa mzima, uwezo wake wa kupress umepungua sana kwa sababu ya uchovu, hili kocha alitakiwa alijue na kulichukulia hatua muafaka
Chilwell hakuwa mzuri, nadhani alipewa maelekezo ya kupanda eneo lake likageuka uchochoro wa kupitisha mashambulizi
Kwenye benchi yuko Casadei aliyekatishwa mkopo wake uliokuwa unaenda vizuri, hatumiki hadi sasa
Mudryk aliyecheza vizuri mechi dhidi ya Leeds United kawekwa benchi na kuwaacha wachovu wacheze
Kipi kimefichwa hapa?