Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Nyie jamaa mnaenda kutengeneza project ya kibabe sana pale EPL.
Nilishaelezea Project ya Chelsea inahitaji miaka miwili iive , wamepata kocha mzuri mwenye talent ID,mbinu na ufundi wakufundisha

Mashabiki walimkataa Gallagher wakamtaka Joao Felix

Lakini hapo ndipo unaona utofaut wa 7 hag na Poch ,

Poch ameamua kufata misingi yakujenga timu shindani,

Kwasasa unajua kabisa wanaelekea wapi ,wapi waboreshe ,

Wangetaka matokeo ya zimamoto Kama mwafulani , Hali ingekuja kuwa mbaya Sana

Angalia msimamo utaona 7hag anafanya mambo ya Zimamoto ,baada ya muda atakuwa anapiga hatua moja mbele anarudi 10 nyuma .

ili uwe na timu imara ya kushindana mataji itakayokaa muda mrefu ,unahitaji kutoangalia matokeo Bali Jenga timu ya miaka 5-7 mbeleni
 
Data za Enzo kwenye msimu huu…ila dogo amechoka, anacheza soka msimu wa 3 mfululizo huu

IMG_8092.jpeg

IMG_8091.png
 
Hivi nini kinaendelea pale Notingham na yule dogo tuliyempeleka kwa mkopo ?
Mbona hapati Chance kabisa aisee ?
Hii talent tunapoteza hivi hivi ,so bad
Chelsea wanampango wa kusitisha mkataba wake January
Pi Forest wamekuwa wakilipa faini ya kutocheza kwa sababu mkataba wa mkopo unawataka Forest wampe dakika kama yuko fit, wasipofanya hivyo wanalipa faini
January atarudishwa na kupelekwa kwenye mkopo wenye faida kwake na kwa Chelsea
 
John Obi Mikel kwa Victor Osimhen: "Msimu ujao, najua utakuja Chelsea. Nakwambia, nitakuwa wakala wa udalali huo. Nitahakikisha hilo linafanyika. Tumekuwa tukimlilia mtu kama wewe - tangu Didier Drogba alipoondoka kwenye klabu" (@obionepodcast)
1699908745924.png
 
Kuna wale makenge-za walisema mechi 7 hatutaambulia pts 4. Hii ni mechi ya nne je mnahesabu au mumeacha.
Mlisema oh fixtures ngumu hizi
Arsenal 1
Spurs 3
City 1
Bado mechi 3 na huko tutabeba pts. Heshima wekeni
Sisi bado mabingwa wa Dunia
Mechi zetu ngumu ni Everton na Sheffield sio Newcastle na man u Hawa tunapata points
 
Romeo Lavia na Christopher Nkunku watakuwa full fit baada ya international break. Nini maoni yako
Unafikiri ni wachezaji gani watakosa namba baada ya wao kurudi?
1699909348007.png
 
Kikosi hiki kipya ni tofauti kabisa na kikosi cha dakika za mwisho cha Tuchel. Kikosi hicho cha zamani hakipigani kamwe, kamwe hakisumbuki, kamwe hakijali iwapo Chelsea itapoteza au kushinda. Walikuwa sawa uwanjani na nje ya uwanja wakiwa na matokeo yoyote. Lakini kikosi hiki kipya kinanikumbusha kikosi cha Tuchel chenye wachezaji kama Rudiger
1699928033424.png
 
Achana na points
Kwenye big matches 3 tulizocheza tumefanikiwa kuweka mpira wavuni mara 10
Arsenal 2 expected goals 3
Spurs 4 expected goals 7
City 4 expected goals 5

Chelsea ingefunga magoli 15 kwenye mechi tatu tu za hao wanaojiita timu kubwa kama tungekuwa clinical zaidi

Je kwa maelezo haya tatizo la Chelsea la ufungaji ndio umeisha ama bado safari ni ndefu ya kuwaleta akina Victor?
 
Pengine hawa ndio wanaweza kukosa namba kwa kikosi cha sasa.

Gallagher hatoki tena 1st eleven anakiwasha balaa na tunahitaji zaidi energy yake.

Jackson anaendelea kufunga mechi after mechi, sterling ameanza kutumikia rasmi jezi ya THE BLUES hataki masihara tena.

Ila kurudi kwa Lavia na Nkunku ni Habari njema kikosi kinaendelea kupanuka na ushindani utaongezeka katika kugombania namba hence matokeo mazuri uwanjani.

Ubora wa kila mchezaji uwanjani ndio utaamua nani aanze nani sub. Lavia na Nkunku warudi kwanza watuonyeshe ubora wao dhidi Enzo, Gallagher, Jackson, Sterling.
Lavia atapata nafasi kwa sababu Enzo atakuwa akipumzishwa sana, nahisi hadi tuingie January Lavia atakuwa anapata dakika nyingi zaidi hata kama ni za second half. Hivyo hivyo kwa Nkunku, LW itakuwa na ushindani mkubwa sana. Sijui hatama ya Mudryk itakuwaje?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom