Kuna kocha ambae amewai kuulizwa swali na mwandishi akajibu kwamba mchezaji flani simtaki alafu ukizingatia ni kocha mpya
Hili la Conor Galagher Poche hakuulizwa, tangu mwanzo alisema Galaghjer yuko kwenye mipango yake
Aliwataja wachezaji wa academy kama watatu hivi
- Mason Mount
- Conor Galagher
- Levi Colwill
Msimamo wa Poche ni kwamba Galagher sio wa kutupwa na ndio maana Chelsea wamekataa ofa ya pauni 40m kutoka kwa Westham wanataka 50m
Haya mambo huwa uongozi unakaa na kocha kwanza ndipo wanaamua
Odoi kocha hamtaki ona sasa anauzwa milioni 8 na bado hakuna timu inamtaka na bado ana miaka 23 tu
Wale wachezaji wote waliouzwa ukiondoa Mount Poche hakusema kitu maana yake hakluwataka kwenye Project, na ninaamini kabisa huko nyuma ya pazia wanazungumza viongozi na kocha, nani abaki na nani auzwe
factor kubwa ya mchezaji wa zamani kubaki ya kwanza ni
- kuipenda Chelsea na kuwa na positive mentality juu ya timu
- pili uwezo wa mchezaji kwa standard za kocha ila ile ya kwanz andio muhimu zaidi na ndio maana mwanzo
Poche alitaka amjaribu Lukaku ila kwa mentality yake Poche kamzuia kabisa asije darajani kabla hawajaondoka kwenye USA. Hivyo hivyo kwa Ziyech. Hawa wachezaji walioko sasa hivi kama Chalobah na Galagher ni kweli wanaipenda Chelsea ila Chalobah hajavutiwa na Kocha, Galagher kocha anamuona kama anaweza kufundishika na akaboresha uwezo wake ila kama atauzika na kuipatia timu mapato mazuri auzwe ndio soka na alisema hivyo kwenye interview ya mwisho juzi nadhani au jana kuwa Galagher yuko kwenye mipango yake ila akipatikana mnunuzi wa bei nzuri auzwe ili asije akakalia benchi na kuanza kunung'unika na kudondoshea sumu dressing room kama akina Mount, Ziyech, Pulisic, Koulibaly, Lukau na wengine
Nasikia leo pia tetesi ni kwamba P{ochettinoi anamtaka kipa mpya naona hajaridhishwa na Kepa pamoja na kupatiwa kocha wa kumfundisha. Na anamtaka kipa mwenye uzoefu na EPL kama akina Sanchez wa Brighton, Raya wa Brentford na yule wa Shakhtar Donesty