Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Sisi mashabiki wa Harry Potter tuna imani nae

Tajiri muongezee mkataba huyu
20230108_224807.jpg
 
Potter ni kocha mzuri ila mashabiki ndio sio waelewa
Sir Alex Ferguson time anaanza kazi MANCHESTER United alifungwa mechi 38 tu ila akavumiliwa na akawa kocha mzuri

Potter mitano tena
We unataka kuwaponza wenzio
 
Jana Fofana kapigana sana, huyu ndie mfano halisia wa mchezaji anayestahili kuvaa jezi ya Chelsea
Kule nyuma mabeki walitulia vizuri. Sikuwa na shida ya performance ya Kou na Badi
Chilwell anaanza taratibu kuja kwenye form yake ya uwezo wake wa kupokea mipira mbele kwenye maeneo ya hatari kwa timu pinzani. Kuna nyakati kama mbili au tatu Chilwell alikuwa kwenye best position anaomba mpira ila kama kawaida ya wachezaji wetu kila mtu anataka awe shujaa.
Havertz sijui ana matatizo gani, clinicality yake siku hizi hata wale wa Championship wanamzidi mbali sana. Ile chance yake ya jana angewahi kumpelekea kipa mp[ira wa juu lile lilikuwa ni cool goal, ila kamfuata kipa hadi amemfikia karibu ndio=po anajifanya super star
Wachezaji wangekuwa makini jana tungetoka na goli 4 au 5-0
Sisi mfumo wetu mzuri ni wa 3 ndio maana umeona chilwell kan'gaa na hata angecheza James nae angen'gaa
 
Nikikumbuka humu ndan kuna watu walikuwa wanampigia chapuo Potter nabaki naishiwa nguvu.

Tungeenda kwa Luis Enrique kwa project tuliyonao ni mtu sahihi.

Tunaweza kuwa na wachezaj wazuri ila wakakosa kocha, inanikumbusha wakat tuliokuwa na MaZaCa(Mata,Hazard,Oscar) kocha akawa Di mateo
Mimi ni mmojawapo niliyempigia chapuo Potter kwa sababu ndie alikuwa kocha wetu na alikuwa bado mgeni. Tulidhani atakuwa kocha mzuri ila tulikuwa wrong tena far wrong. Naamini Potter anaweza kubadilika akawa kocha mzuri ila tukimsubiri tutaumia sana na bado hakuna uhakika kama atabadilika.

So now I hate very much yeye na Boehly anayeendelea kuleta ubishi wa kumng'ang'ania na nasiklia kule kwenye bodi wamegawanyika, wengi wanataka afukuzwe ila yeye bado anamng'ang'ania abaki
 
Ninawakumbusha tu msije sema sijawaambia kuwa kesho timu yetu itaaga rasmi michuano ya Ulaya kwa mwaka 2022/23 na 2023/24
 
Man city ndio timu pekee ya England itakayofuzu robo fainali uefa.
Asanteni kwa kushiriki.
 
Havertz itakua anampa Potter miuno ya kitanga sio kwa mahaba haya
Kwenye penalty kumpa havertz sio shida cos kai ni mpigaji mzuri wa penalty ila shida kuu ni kwanini anamuanzisha kila game na hamfanyii sub hata kama hayupo kwenye performance nzuri
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom