Wapendwa mashabiki wa Chelsea
Amani iwe nanyi
As-salaam 'alykum
Kwa nini matokeo kwa sasa ni mabaya sana kwa Chelsea?
Sababu yake kubwa ni mbili ambazo ni mabadiliko ya umiliki na uongozi iliyosababisha mabadiliko haya:
- Mabadiliko ya Maono na
- Mabadiliko ya Approach
HOW?
Wakati wa Roman Abramovich lengo ilikuwa angalau kila mwaka kushinda makombe na hiyo ilitimia ila hapa kuanzia 2018 hadi leo ukiacha 2021 iliyumba sana
Jinsi au apprach ya kufikia hayo maono yalikuwa hayana uendelevu ndani yake
Alimradi mbinu mbinu na ujanja ujanja utumike ili kufikia maono
Mbinu mojawapo ilikuwa kuajiri wachezaji walioiva na kubadilisha makocha kila mara
Approach kubwa ilikuwa ni kuwasikiliza zaidi wachezaji kuliko kocha. Hii haina uendelevu kwa sababu kocha anafanya kazi kwenye mazingira ya woga na kutokuwa na jitihada zozote za kujenga timu kwa sababu wakati huo "PROCEES" ilikuwa haiaminiki kabisa. MOU aliletwa darajani mzee wa mbinu mbinu na kweli mbinu zake za kupaki mabasi na kushambulia kwa kushtukiza iliua kabisa ufalme wa Mwanitesa United na Arsenal kila mwaka wao ndio title contenders.
Alipotoka MOU wakaja wengine kwa staili hiyo hiyo na ndio maana makocha wengine walishindwa kuleta makombe walifukuzwa haraka sana. KOcha wa Chelsea wakati huo kama huna mbinu na ujanjuaujanja ulikuwa hufai kuwa kocha wa Chelsea. Wale makocha wenzangu wa kujenga timu na kujali sana process walikuwa hawafai kuwa makocha wa Chelsea.
Nakumbuka ile 2016 akina Fabregas, Costa na Hazard walivyomgomea MOU akatimuliwa ili kambi itulie na Conte alipokuaj na mbinu zake pup tukabeba EPL tena
Sasa wamekuja Wamarekani
Maono yao ni kuwa na timu imara iliyojengwa kutokea kwenye mizizi. Yaani timu ambayo haitegemei tena kuwanunua wachezaji walioiva badala yake kuwepo na pool ya academy ambao wataingizwa kwenye first team bila kutumia ghrama kubwa. Na ndio maana usajili mkubwa wa akina Boehly ni wa vijana chini ya miaka 21
Hawa tunaowaona zaidi ya miaka 21 ni kwa ajili ya kutatua tatizo la muda mfupi ambalo wamelirithi kutoka kwa utawal uliopita
Wao wanaamini ukishakuwa na timu iliyojengwa imara kuanzia kwenye mizizi pia kutakuwa na uendelevu wa kubeba makombe
Juhudi ya kuhakikisha hili linatimia limeonekana pia kwa kuboresha idara ya scouting kwa kuingia mkataba na digital scouting system inayoitwa AiScouting kwa miaka mitano na ikionyesha manufaa nadhani huu ndio utakuwa mtindo wa maisha pale darajani.
"London, UK – Chelsea FC has today announced the signing of AiSCOUT – the world’s first fully automated talent analysis and development platform.
The six-times Premier League and two-times Champions League winners negotiated a deal to secure AiSCOUT as their Official Academy Research Partner, with the platform set to become an integral part of the club’s recruitment and scouting process for academy players over the next five years."
Approach ya wamiliki wa sasa ni kuwa upande wa kocha, wachezaji wasioperform aidha kwa kushuka form au kumgomea kocha kama akina Fab, costa na Hazard, watatimuliwa kama Arteta alivyomtimua Auba
Mimi naona hiii approach ni nzuri kwani itarudisha heshima kwa kocha na wachezaji watamsikiliza kocha na kufanyia kazi maelekezo yake bila mgomo baridi.
Hakutakuwepo na mchezaji aliyemkubwa kuliko kocha au timu. Conte alipogundua hiyo tabia ya kumgomea kocha kwa Costa alimtimua kwa sms kitu ambacho iligharimu ajira yake. Natamani Conte ndie huyo wa 2017 angekuwepo sasa Chelsea ya akina Boehly. Wangeendana ile mbaya. Na Chelsea ingetisha ile mbaya. Ndio maana mimi bado naomba Mungu Boehly na wenzake wangetumia tu busara kukatisha mkataba wa GP na kumchukua Conte pale Spurs kwa sababu hajaridhika kabisa. Spurs hawana jeurii ya kuingia sokoni na kwa hiyo Conte kabakia na matakataka yanamchefua sana pale Hotspurs.
Hii aproach ya kujenga kuanzia kwenye mizizi na kuwa upande wa kocha itakuja kuonekana dhahiri baada ya misimu mitatu hadi minne ambapo utamaduni wa timu nzima itakuwa kila mtu atimize wajibu wake. wachezaji kumheshimu kocha na kocha kufanya kazi kwenye mazingira ya uhuru bila woga. Pia overhead ya timu kwenye manunuzi yatakuwa yamepungua sana na akina Boehly watapiga pesa nyingi za faida ile mbaya. Kwa wakati huo pia Chelsea itakuwa imenunua vilabu mbalimbali duniani kama ilivyo kwenye plan kwa ajili ya kuzifanya hizo vilabu kuwa ni pool ya kuwapata wachezaji ambao ni talented kwa bei rahisi
Ikifika wakati huo kama vilabu vingine havijafanya mabadiliko kama haya watakuwa wanaisikia Chelsea kwenye bomba tu. Kwa sababu kama timu inapata faida na ina wachezaji wanaoweza kufanya lolote uwanjani kwanini UEFA isiwe ya kwetu kila mwaka?
Kwa nini EPL isiwe ya kwetu kila mwaka?
Mashabiki wenzangu wa Chelsea tusiwe na shaka na uongozi kwa mwaka huu. Hata tukimaliza nafasi ya 17 no problems
Tukishalima sangari na kupanda, wakati wa mavuno tutachekelea juu kwa juu
YAJAYO YANAFURAHISHA ZAIDI