Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

OllaChuga Oc lembu huwa mna kelele sana kwenye jukwaa letu kumbe team yenu ndio hii?Chelsea mnayoitambia?matak* yenu tumewanyanyasa kinyuma na mbele I think itakuwa mwisho wa kuja kupiga kelele kwenye jukwaa na Arsenal
Mmepiga maiti wala hamna haya kushangilia. Timu ina injuries 8 tena wa first team. Mmecheza na development team na bado mmeshindwa kufunga magoli mengi huku mkishangilia. April Mungu akijalia tutakuwa wote hapo Emirate
 
acha tupigweee tuuu maana huyu kocha ni choko, hivi kati ya makocha wote duniani huyu ndio tuliona ni kocha????
Hlo swali ndo la msingi , tafuta kocha mwenye CV , sio kocha et amepandisha timu daraja na anagombea top 4 unampa kisima 😁
 
Tim mbov sana hii,

Tuchel alikuwa yuko sahihi, japo watu tulimuona hafai.

Tumemfanya arsenal aonekane kama prime barcelona or city,

Sion tukishinda game yoyot katika game 2 zijazo
Carabo cup dhid ya city naona kabisa tunatolewa,
Game ya league dhid ya newcastle naona tunaona poteza

Game ya 4 kwenye league hatuna ushindi
Ninyi ninyi mliisifia timu hii hii ilipocheza na goigoi RB Salzburg. Tukawaambia timu hii bado. Middle zaidi ndio imepotea. Cheek hafai kabisa, hata kule mbele kushindwa kufunga ni kwa sababu ya hawa middle wetu.
 
Man city anatutoa carabao na Newcastle wanatufunga. Tushukuru tu kombe la Dunia tupumzike na baadhi ya wachezaji wapone. Team hatuna kiungo mkabaji wa maana, hatuna kiungo mshambuliaji, hatuna mshambuliaji wa kumaliza msimu hata na goli15.
Tatizo la msingi liko middle. Time will tell
 
Timua timua ya makocha haitotupeleka popote kwa sasa, tutaendelea na kuwa vile vile, Arsenal wako hapa walipo coz walimuamini Arteta n now matunda yanaonekana, Arteta kawatoa wale wote aliona haendani nao.

Sisi tukiendelea na huu utamaduni tushinda hivi vikombe vya fa,carabao, ila premier league tutaendeleea kuskia kwa bomba kama hatuna project.
Aterta kaleta nn arsenal , ? Hata msimu huu ataishia kuwa forerunner... Kama ndio mipango yenu endeleeni kumwamini kocha,
 
Generalization sio njema. Mhemko na hisia hazitakiwi. Chemistry ikiharibiwa na mchezaji mmoja muhimu au wawili timu nzima inaweza kuonelana hovyo. Bado mimi naamini kocha bado hajapatia ni chemistry ipi italeta matokeo mazuri. Pia bado formation na falsafa. Hii ya 433 naona itafaa kuliko 343 labda james, Kante na Chilwell wakiwepo uwanjani. tunahitaji addition ndogo tu. DM na cretive midfiel attacker aidha mmoja mmoja au wawili wawili. Tutahitaji pia RB/ RWB. Hawa wakipatikana utawaona akina Sterling, broja, auba hata pulisic na havertz wakifunga kwa urahisi
Katikati hapo anatakiwa kubaki Kova tena awe sub. Cheek, Jorginho hawatufai tena
Tena cheek ndio hovyo
 
Kinacho tuuma ni kufungwa na Arsenal mbovu kwasabb ya majeruhi wengi akiwemo na kocha huyu chakinorisi wenu hatupeleki popote ana bahatisha mbinu.
Arsenal sio mbovu hata tungekuwa na wachezaji wetu wote na tukamfunga Arsenal, tuweke ushabiki pembeni bado Arsenal ya mwaka huu ni imara na yenye chemistry nzuri kuliko sisi, Wana ball control nzuri na utawaona kwenye pasi zile za haraka haraka wanavyothibiti mpira usiwatoke. Tushukuru Mungu tu WC inakuja kutuokoa ili tukirudi Desemba mwishoni tutakuwa na baadhi ya majeruhi kama akina Fofana, James na Kepa
 
Tena cheek ndio hovyo
Cheek akipata mpira lazima aweke miguuni halafu ajifanye mjanja wa mjini, yaani yeye kupata mpira na kutoa haraka hana hiyo tabia. Mpira wa siku hizi wa kasi ukizubaa na mpira watakunyang'anya tu
 
Kosa kubwa kumuondoa Tuchel yule bonge la kocha alitakiwa apewe muda aweke mambo sawa. Rahem kama hawezi kucheza mbele akae bench sio kumpa wing back. katika lazima wacheza watatu hii 4222 haifai
Kocha alishakiri kosa na tangu hapo Sterling amekuwa akicheza nafasi yake. Jana kocha aliweka 4-2-3-1 na tatizo kubwa waliotuangusha jana ni midle Jo na Cheek hawakuweza kuthibiti mpira pale katikati. Hawako cretive pia kushirikiana na CAM kutengeneza nafasi kwa washambuliaji. Tusiwachukulie wachezaji wote ni wabovu. Auba ni mzuri sana wa kutupa angalau goli 15-20 kwa msimu ila asipohudumiwa atawezaje?
 
Me ni mmoja kati ya watu niliokuwa namtetea kila siku tuchel humu ndani, nikiamini wachezaj tulionao hawafai.

Rudi miezi ya nyuma, why tuchel alifukuzwa, according to boehly tuchel hakufukuzwa sio kwa sqbabu ya matokeo, bali kutokuwa na maono tofauti na wamiliki.

Wote tutakuja kukubal ipo siku kuwa wachezaj tulionao sasa ¾ hawafai kuwepo.

Tuendelee kufanya rebuilding itakayoendana na mahitaj ya tim na player watakaofit na si ilimradi tuonekane tumesajili,
Hakuna mtu aliyesema TT ni mbovu, zama zake zimeisha sasa tupo zama za GP. Timu bado inajengwa tusisahau hili. Hao wachezaji wasiofaa wataondolewa ila sio kwa mkupuo mmoja na pia hao wachezaji wanaofaa watasajiliwa ila sio kwa mkupuo mmoja. Tukumbuke pia usajili hata uwe makini sana ni gambling mwisho wa siku. Tulimchukua Silva kwa matarajio ya kumjaribu msimu mmoja tu lakiniu sasa ni msimu wake wa 3 nafikiri. Tulimsajili Havertz kwa mbwembwe nyingi na nyoyo za mashabiki wakaridhika kabisa. Yuko wapi hadi sasa anapeta uwanjani tu bila impact ya maana. Timu imara inajwngwa kwa mikakati mizuri. Boehly ameonyesha anayo mikakati
 
Unamwaga 300M huku ukiwa unaplan zingine, ni wastage of money hapo,

Huwa nasema why uspend 300M huku ukiwa unajua huyo kocha utamfukuza, yani unamsupport kocha kwenye usajil huku ukijua kwamba utamfukuza kwa kutokuwa na maono sawa na wewe, hizo hela ni kama hatujafanya kitu. Tunaonekana wabovu kuliko hata msim uliopita
Boehly hapo alizingua sana
Ilitakiwa Boehly angefanya mambo mawili
  1. Angemfukuza TT kabla ya usajili ili kocha mpya apendekeza wachezaji wake AU
  2. Angemuacha TT ili ajenge timu kwa wachezaji aliowataka wanaoendana na falsafa yake kama Arsenal walivyofanya kwa MA hata alipoboronga walimuacha akamtoa kafara AUBA aliyekuwa anaharibu Dressing room. Naye TT angeachwa angemtoa Jorginho kafara aliyekuwa anamharibia TT
 
Kwa sababu sioni faida ambayo ameipata kwa kumwaga pesa nyingi kufanya usajili wa mapepe bora asingesajili kabisa tukajua msimu huu tumefanya vibaya kwa sababu hatujasajili.

Umesajili replacement za Rudger na Christensen haya ziko wapi? Fofana na Koulibaly
Huu usajili haukuwa wa mapepe, ulikuwa ni usajili wa TT. Kosa la Boehly ni kumfukuza TT huku wachezaji waliosajiliwa ni wa kwake
 
Mmepiga maiti wala hamna haya kushangilia. Timu ina injuries 8 tena wa first team. Mmecheza na development team na bado mmeshindwa kufunga magoli mengi huku mkishangilia. April Mungu akijalia tutakuwa wote hapo Emirate
Na zile nne za mwaka jana msimu uliopita injury walikuwa wangapi?
 
Wakuu, hivi huyu kocha nyie wenzangu umnakwelewa kweli? kuna timu mule ya walau kuwa top four mwisho wa msimu ?

Au na sisi tunaanza kujenga timu upya, maana sikuona lolote jana na tulitakiwa tupate adhabu zaidi ya hiyo.
 
Pierre-Emerick Aubameyang had just four touches in the first half against Arsenal, at least 15 fewer than any other outfield player.

He also received more yellow cards (1) than he had shots (0).
 
IMG-20221106-WA0010.jpg
Hiii🖐️🖐️😁😁
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom