Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

IMG-20221012-WA0007.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Barcelina kaponea chupuchupu kufungwa tena na Inter. Huwa nafuurahi hii timu ikifungwa. Inter wanahitaji ushindi mmoja tu ili kuwapeleka Barca Europa
Sikuangalia match match ila baada ya kuona interanaongoza mbili moja, Nikaanza kupiga maombi barca asukumizwe uropa.

I wish Inter angeshinda jana. Japo chance yake kushinda kwa Victoria ni kubwa sana.
 
Ngolo Knate kaumia tena mazoezini hata bila kuja kucheza
Huyu auzwe tu, Chelsea sio wodi ya majeruhi
 
Ngolo Knate kaumia tena mazoezini hata bila kuja kucheza
Huyu auzwe tu, Chelsea sio wodi ya majeruhi
Hiyo kauli mbaya kutoka kwa shabiki kama wewe tu heshimu na kutambua mchango wa Kante katika timu yetu kabla ya majeruhi, tuwe na roho ya ku-appreciate wachezaji wetu kama wazungu walivyo mpokea Diego Costa alivyo pokelewa na wenye timu licha ya kua kwenye timu kizani, futa hiyo kauli yako tafadhari hamna anaye jitakia majeruhi tujitahidi kuonyesha maturity kwenye ushabiki wetu.
 
Hiyo kauli mbaya kutoka kwa shabiki kama wewe tu heshimu na kutambua mchango wa Kante katika timu yetu kabla ya majeruhi, tuwe na roho ya ku-appreciate wachezaji wetu kama wazungu walivyo mpokea Diego Costa alivyo pokelewa na wenye timu licha ya kua kwenye timu kizani, futa hiyo kauli yako tafadhari hamna anaye jitakia majeruhi tujitahidi kuonyesha maturity kwenye ushabiki wetu.
Covax kweli huwa una weight parameters zotre za hoja?
Nilivyosema hivyo haimaanishi sikuappreciate kazi yake, center ya hoja yangu sio appreciation bali future yake Chelsea
Wach kukurupuka, sina kauli ya kufuta au unajitakia umaarufu kwenye hoja yangu. Mimi ni top admirer wa Kante but when it come a time to partways na mtu unayempenda inakaa hivyo hivyo wala hakuna mbadala. Atabakia kuwa Legend wa Chelsea ila kwa hii era tuliopo Kante umuhimu wake unazidi kupungua penda usipende

  1. Parameter ya kwanza Kante ana zaidi ya miaka 31
  2. Pili Kante freequencies za kuingia majeruhi zinaongezeka jinsi umri unavyokwenda
  3. Anadai mkataba mrefu ambao tajiri hayuko tayari kumpa
  4. Kwa hali hii tunahitaji kufocus long term replacement plan
 
Kocha mkuu wa Chelsea ya wanawake Emma, hatofundisha timu kwa muda
Screenshot_20221013-182403.png
 
Chelsea wants to buy Raphinha. Barca hijacks. Chelsea wants Kounde. Barca hijacks. Chelsea wants to renew Christensen. Barca hijacks. Chelsea are not in form and on their way to the Europa League. Barca hijacks
 
Hiyo kauli mbaya kutoka kwa shabiki kama wewe tu heshimu na kutambua mchango wa Kante katika timu yetu kabla ya majeruhi, tuwe na roho ya ku-appreciate wachezaji wetu kama wazungu walivyo mpokea Diego Costa alivyo pokelewa na wenye timu licha ya kua kwenye timu kizani, futa hiyo kauli yako tafadhari hamna anaye jitakia majeruhi tujitahidi kuonyesha maturity kwenye ushabiki wetu.
Hilo taira Lembu ni mamluki tu linaropokaga tu bila kutumia akili ake vizuri
 
Deadwood zinapunguzwa inabaki moja ya kuitwa Pulisic

Sent using Jamii Forums mobile app
GP anawapenda sana young age na anajua namna ya kuwainua viwango vyao. Sidhani kama Pulisic atawekwa nje ya plan za GP. Unaweza ukashangaa akina Callum Hudson Odoi, Levi Colwill. Ethan Ampadu wote wakabakizwa msimu ujao. Kizuri kwa Pulisic ni kwamba anayo speed na ana uwezo wa kudrible. Stayle ya mashambulizi ya Tuchel ndio ilimpoteza Pulisic. Mbona wakati wa Kampard alikuwa anaenda vizuri?
Tumpe muda angalau msimu huu utaona nafasi chache atakazopewa kwa style hii ya GP ataboresha kiwango chake. Na hizo dalili zimeshaonekana. Na pia nilipenda kauli zake za mwanzoni mwa msimu aliposema atabakia Chelsea kupambania nafasi yake. That mentality is very good in football. Tofauti na Ziyech aliyejawa na hasira ,,kuktaa tamaa na kulalamika. Ziyech sijui anamgomea nanai. Akipewa muda hapambani kabisa na ZIyech ni bonge la mchezaji.
 
Kuna mjadal uliwahi kuwa hapa kuhusu mfumo, formation nk

Tuchel alikuwa akitumia 343 lakini defensively
Potter anatumia 343 lakini ofensively
Same formation diferent style of play
ndio maana mimi nasema formation kwa kiswahili ni mpangilio wa wachezaji uwanjani kulingana na uwezo wao wa kucheza hizo nafasi
Ndio maana Potter anakuja na formation tofauti kila game
Anapofanya mabadiliko kwenye timu mfano rahisi, ukitaka Chilwelll awepo uwanjani na James ni lazima formation iwe ni ya kutumia wing-backs, James na Chilwell wanakuwa at their best when they play as wing-backs rather than Full Backs.
Halafau pia kwa kipa. Mendy ataendelea kukaa benchi kwa sababu Poter na Tuchel ni makocha wenye falsafa ya mpira tofauti kabisa

Tuchel ni defensive coach wakati Potter ni Offesnive coach
Wakati wa Tuchel kila mchezaji anakaba na aliwataka wachezaji wenye uwezo wa kukaba hata kama hawafungi magoli.
Sasa ni tofauti, wakati huu wa Potter anawataka kila mchezaji awe na uwezo wa kutoa mchango kwenye kushambulia.
Kepa anajua kufanya distribution ya mipira ambayo ni nzuri sana kwenye kujenga mashabulizi yakiwepo yale ya counter attack. Mendy sio mzuri kabisa kwenye distribution ya mipira anafaa kwenye mfumo wa Tuchel wa defensive approach

So Kepa is an offensive golie while Mendi is a defensive golie

Hii falsafa inaenda pia kwenye nafasi zingine hasa za kwenye midfield
Denis Zakari is typical a defensive midfield ambaye angefaa sana kwenye style ya Tuchel sasa tunaye Potter ambaye yeye anapenda hata DM awe na uwezo wa kujenga mashambulizi. Na nahisi hii ndio sababu kubwa kwa nini Denis Zakaria hachezi hadi sasa hivi

Huko mbeleni tutashuhudia Potter akiwaleta wachezaji wenye mindset ya kushambulia kuanzia kwa Kipa, Mabeki, Viungo na ikifikia hapa tutakuwa na a very dangerous team kwenye EPL na UCL

Nitolee mfano tu zile pasi mbili zilizosababisha magoli, yaani pasi ya James kwenda kwa Mount na Pasi ya Kovacic kwenda kwa Mount zilikuwa ni pasi za haraka kama zile za Man City au Liverpool. Hatujawahi kufunga magoli Chelsea kwa hivi karibuni kwa pasi za kasi kwa style ile, Sasa ndio tumeanza kuziona kwa Potter
 
Sikuangalia match match ila baada ya kuona interanaongoza mbili moja, Nikaanza kupiga maombi barca asukumizwe uropa.

I wish Inter angeshinda jana. Japo chance yake kushinda kwa Victoria ni kubwa sana.
Barca to Europa 90%...Afu kocha wao xavi anautaifa Sana...watu kazi kina frenkie kessie sio WA Kula mbao mechi km Ile au FDJ
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom