Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Nashukuru ile laana ya no 9 Auba ameiyondoa jamaa nimependa Sana anajua kutumia nafasi namuona kabisa atatupeleka nchi ya ahadi.

Good news pia Mount kiukweli amerudi kwenye ubora wake GP amefanya kazi yake kisawasawa kumrudisha Huyu mwamba mechi mbili ameshatengeneza assist 4
 
Naamini tutaendeleza ubora wetu. Chelsea tuna vijana wazuri ambao wakijengwa kisaikolojikale watafanya wanders. Pia bado ni vijana wadogo so ubora wao utadumu. Natamani tu PG awape nafasi wote au aendelee kufanya rotations kama anavyofanya. Hii itawapa motisha wachezaji wote na kujituma kwenye mazoezi.

Ukiangalia Gadiola hana first 11 yake. Kila siku lazima aingize sura mpya mbili adi tatu.
 
TETESI
Ziyech and Densi Zakaria out of POTTER PLANS
Nasikia January wote wanaondolewa, mkataba wa Denis utafupishwa na Ziyech kuuzwa dirisha likifunguliwa
Denis Zakaria Sajiri ya mchongo hi, Kama Juve mbovu anakosa namba na mwenzake melo ,Ni wazi juve walikuwa wanatafutaga Sehemu ya kuwabwaga.

Liverpool walikuwa na mpango wa kumvunjia mkataba January, tayari kashaumia mazoezin miez minne nje

Denis Zakaria ndio wale wale kina Arthur melo
 
Ila Potter Ni Kocha mzuri hata kimbinu ,Chelsea ilishakuwa butu kufunga , niliwahi kusema humu nikashambuliwa ,Chelsea ushindi wao chini ya Tuchel msimu huu ilikuwa 1-0,1-1,2-1,0-0,

Ila Potter ka unlock Attacking , Sijui man u wanakwama wapi kupata makocha Kama Potter, Yule kipara wao anashinda lkn dah unaona kabisa JINI KATOKA MGANGA HOI.
Mech na everton magoli yote mawili Ni Baada ya Gueye na Iwobi kukosea pass , ila Sio Kwamba eti Man u ya kipara unaona kabisa mipango ya kutafuta goli, do za mwisho Man u akapaki Basi🤣🤣(+_+)

Sio Kwamba ana wachezaji wabaya ila naamini Ten hag uwezo mdogo ,anayebisha nipo tayari kwa mjadala

Kwasasa Chelsea ya Potter lazima tuiangalie kwa makini , nabadili Kauli , 🤣🤣

Chelsea ya Tuchel ilikuwa inatabilika , inarukaruka tu,

Lakini Potter timu yake in flow , Ten hag anasubiri miujiza dk 90 aone kasshinda,

Kwasasa Naiona Chelsea kwenye Challenge pale juu .
 
Naona now back pass, zimepungua tuko more direct now na vertical pass, n sharp katika kushambulia.

Goal la pulisic vs Wolves na goal la Auba vs Milan jana unaona kabisq wqcheza wanajaribu bilq hata kuogopa kitu ambacho mwanzon ni kama walikuwa wanaogopa na wanacheza kwa kuenjoy mpira wao

Natumai tutaendelea kuimarika kadri siku zinavyozidi kwenda,
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom