Tajiri miluzi mapepe, papara, ujuaji mwingi mbele giza. Mipango yake anaifanya vise versa.
1. Angemuajiri kwanza Mkurugenzi wa michezo.
2. Tajiri na Mkurugenzi wa michezo washauriane na kumleta kocha mpya, atakayematch maono na mipango yao.
3. Kufanyika kwa Usajili.
4. Kuajiri na kuboresha vitengo vingine vya kimasoko n.k

Sasa Tajiri miluzi ameanza kwa kufukuza watendaji wakuu, amejimilikisha vyeo vyote, kafanya sajili za kukurupuka kwa kushirikiana na TT na amemfukuza.

Kamleta Potter ambaye atapata Changamoto ya kufanya kazi na wachezaji ambao hakuwasajili, wachezaji kachumbari, mwisho wa siku tajiri miluzi atakurupuka tena atamfukuza.

Yaani bora dirisha hili tusingesaji wachezaji bali wangeletwa kwanza Mkurugenzi wa michezo na kocha halafu Tajiri, Mkurugenzi na Kocha wakakaa pamoja wakakisoma kikosi na kushauriana kisha kuja na mahitaji na mipango ya kukiboresha kikosi kimkakati kwenye madirisha yajayo ya usajili.
Tungekwenda vizuri kuliko hii vise versa ya sasa