Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Cheek
Ziyech
Pulisic
Jorginho
Harvetz
Azipculeta

New coach, same story
Cheek muondoe kwenye hiyo list, hata akija kiungo mzuri Cheek kwa uchezaji wake anafaa kwa rotation au backup ila hao akina Pulisic, Ziyech, Jorginho HAPANA, Havertz Premium league maji mazito ila bado nina imani atainuka hivi karibuni
 
Watakuelewa baadaye kuhusu kuboronga kwa Kepa. Ule mpira haukuwa na nguvu/kasi yoyote Kepa kushindwa kuudaka. Alikosa umakini tu.
Sio kuudaka, alitakiwa tu kuugusa utoke nje, Kepa ni mzito kwenye kutabiri
Japo lazima tukiri ule mpira kipa yeyote angeudaka au kuupangua kwa kubashiri kwa sababu mpigaji alikuwa na option ya kupiga katikati, kulia au kushoto na pili Azpilicueta alikaa mbele ya kipa asingeweza kuchanganya mahesabu yote na kujua mpigaji anapigaje. So punguzeni mashambulizi kwa Kepa.

Kwa mimi Kosa la msingi ni la Silva (Silva asingemkaba bali angemchelewesha kwa kumbana asipige ili kuruhusu wengine kurudi kukaa kwenye position, haraka ya kukaba imesababisha mpira upigwe haraka wakati golini yuko Azpi peke yake na adui), Kosa linalofuta kwa uzito ni la Azpilicueta (angembana huyo mshambuliaji na alikuwa peke yake asingeweza kushoot, yeye alimuacha akakasita kumfuata, alipotaka kumfuata it was too late) na kosa la tatu ni la Wachezaji wengine (cucurella, Jorgninho, James, Mount) hawakujituma, hawakufanya jitihada za kurudi haraka kusaidia kuokoa ule mpira. Kama ni kosa la Kepa linakuja nyuma ya hao niliowataja
 
Acheni kuwa wapumbavu basi, yani mechi 1 majibu yote mnayo ninyi.

Hivi mnatakaje maendeleo ya haraka haraka kwa wiki 1 tu ambapo

Kocha mpya
Wachezaji wapya
Mifumo mipya
Mbinu mpya
Formation mpya
Attitude mpya
Malengo mapya
Mkataba mpya [emoji848]

Kweli Mashabiki maandazi wapo kila mahali [emoji1]
Hii timu tumepigwa. Huu msimu tutaboronga.
 
Name: Christoph Freund
Age: 45yrs
Position: Sporting Director
Current Team: RB Salzburg

Kasema nini?

Amekataa kukataa kuwa anataka kuwa Chelsea next Sporting Director
Mazungumzo yako kwenye advanced stage

1663266446143.png
 
Chelsea majanga, sitaamini kuwa zile mbio zote msimu uliopita za kushiriki uefa pale top four then muishie makundi na kwenda Europa, hapo ndo ntaamini hii team ni kichwa cha mwendawazimu
 
Chelsea majanga, sitaamini kuwa zile mbio zote msimu uliopita za kushiriki uefa pale top four then muishie makundi na kwenda Europa, hapo ndo ntaamini hii team ni kichwa cha mwendawazimu
Inakuhusu nini, tunajenga timu yetu na hili liko wazi ila kiherehere chako kuja kutuchokoza tu
 
The blues tunapitia kipindi kigumu hiki kwasbb hi team ndo inasukwa upya ili iwe tishio mbeleni, wakati huo sie mashabiki wa Chelsea tume zoea kubeba vikombe au trophies kila msimu angalao kimoja au viwili sisi hatuna stress kama mashabiki wa arsenal au Man u hiyo ndo hobby yetu.

Sasa tuko tayari kuvumilia hilo ila wasi wasi yangu ni Ghram Potter huyu kocha muingereza ana falisafa gani ambayo atakao fundisha the blues!!!!

Makocha wengi wa uingereza hawana mbinu za kisasa za soka ndo maana hamna kocha mngereza ambaye kasha wahi kuchukua Epl, simaanishe kwamba Potter ni kocha mbaya hapana, lakini ni kweli ni upgrade ya TT? au tutarudu kule kule mpaka afukuzwe ndo tuanze upya tena.

Soka la sasa limebadilika lakini uingereza hawajabadilika ukocha wao ndo maana wengi wana struggle kwenye league yao wenyewe, makocha wageni wanafanikiwa wao hata nafasi ya nne hawapati, hata timu ya taifa alisha wahi kutafuta makocha wageni kufundisha timu yao baada ya kugundua hilo.

Je kocha potter atakua na jipya?
 
The blues tunapitia kipindi kigumu hiki kwasbb hi team ndo inasukwa upya ili iwe tishio mbeleni, wakati huo sie mashabiki wa Chelsea tume zoea kubeba vikombe au trophies kila msimu angalao kimoja au viwili sisi hatuna stress kama mashabiki wa arsenal au Man u hiyo ndo hobby yetu.

Sasa tuko tayari kuvumilia hilo ila wasi wasi yangu ni Ghram Potter huyu kocha muingereza ana falisafa gani ambayo atakao fundisha the blues!!!!

Makocha wengi wa uingereza hawana mbinu za kisasa za soka ndo maana hamna kocha mngereza ambaye kasha wahi kuchukua Epl, simaanishe kwamba Potter ni kocha mbaya hapana, lakini ni kweli ni upgrade ya TT? au tutarudu kule kule mpaka afukuzwe ndo tuanze upya tena.

Soka la sasa limebadilika lakini uingereza hawajabadilika ukocha wao ndo maana wengi wana struggle kwenye league yao wenyewe, makocha wageni wanafanikiwa wao hata nafasi ya nne hawapati, hata timu ya taifa alisha wahi kutafuta makocha wageni kufundisha timu yao baada ya kugundua hilo.

Je kocha potter atakua na jipya?
Tusubiri tuone
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom