Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Ni kwamba tu mashabiki wa chelses tushazoea kulalamikia makocha, lakini safari hii tatizo ni kwamba tuna wachezaji wasio na calibre ya kucheza chelsea.

Embu angali goli tulilofungwa, azpilicueta anaona kabisa forward yuko mbele yake baada ya thiago kufanya makosa ila akabaki anamuangalia tu mpaka alipopewa pasi ndo akajifanya anaenda kumkaba. Goli lilikua linazuilika kabisa yani lile.

Tuje kwa ziyech, kusema kweli huyu jamaa tusiwe na matumaini kwamba atakuja kuperfom ndani ya uzi wa chelsea. Amekua kila akicheza hasahas msimu huu ndiye anaongoza kwa kupoteza mipira na kukosa nafasi, hovyo kabisa.

Pulisic ndo zero kabisa, akiingia kama vile hatupo uwanjani.

Naonaga wengi mnamsema Jorginho, lakini ukweli ni kwamba Jorginho ni mchezaji bora kushinda wengi mno ndani ya kikosi cha chelsea.

Bila usajili wa maana tutakua kama Man U, kulalamikia makocha kila siku kumbe tuna wachezaji wapumbavu.
Matatizo makubwa la Jorginho ni
  1. kupoteza possession,
  2. kushindwa kukaba na
  3. pasi za nyuma na kushoto kulia.
Jana naona anataka kutuonyesha kuwa anaweza pia kukaba na kujenga mashambulizi Jorgninho akiacha kupoteza mipira kwenye danger zone halafu akawa anakaba na anajenga mashambulizi kama jana alivyokuwa anajaribu ni kiungo mzuri sana.
 
Broja jana kacheza vizuri, naamini mbele angecheza Auba na Broja, Sterling na Mount wakashuka kwenye atatcking midfield na Jo na Kova wakacheza kama CM na huku nyuma tukacheza backline ya 4, yaani formation ingekuwa 4-4-2 jana ingependeza zaidi.

---------Auba ------------------ Broja-------

Sterling ------Jorgninho -------Kovacic --------Mount

Cucurella ------Koulibally --------Silva au fofana --------James

-------------------- Mendy ---------------------

Jana tungeshinda
 
Broja jana kacheza vizuri, naamini mbele angecheza Auba na Broja, Sterling na Mount wakashuka kwenye atatcking midfield na Jo na Kova wakacheza kama CM na huku nyuma tukacheza backline ya 4, yaani formation ingekuwa 4-4-2 jana ingependeza zaidi.

---------Auba ------------------ Borja-------

Sterling ------Jorgninho -------Kovacic --------Mount

Cucurella ------Koulibally --------Silva au fofana --------James

-------------------- Mendy ---------------------

Jana tungeshinda
Takataka kama Havertz sio ya kuanza
 
CHIEF mbona hilo tulishakubaliana long time. Kikosi chetu kina quantity kubwa kuliko quality.

Beba wachezaji wetu shusha pale CITY wangapi watapata namba 1st eleven?


STERLING - HAALAND - MARHEZ

GUNDOGAN - RODRI - BRUYNE

CHILWELL - THIAGO - STONE - JAMES.
Mkuu unamdharau Sana Jorginho pep mpaka Leo anamkubali huyo mwamba jorginho ni mchezaji mzuri inategemea na namna ambacho utakavyomtumia huyo Rodri hana uwezo hata nusu ya Jorginho abebwa na performance ya team individual ni mchezaji wa kawaida
 
Kwa msim huu tusiwe na matumain yoyote yale, kwenye league tunaweza improve ila huku kwenye uefa tunakazi kubwa sana,
 
Hapo kwa Azplicueta mm ndo nilichoka sijui alifikilia nn kumuanzisha nikaona kabisa hamna matokeo
Halafu kingine sub alizofanya azikuwa sahihi kabisa
Nafikiri kocha alikuwa anataka kuweka harmony katika timu, zingatia ni mechi yake ya kwanza alafu unamuacha Captain nje wakati unajua baadae utamuhitaji kwa ajili ya kuweka mambo ya dressing room sawa.
 
Nasema Thiago alizingua ila stil azp angewah kuclear since ashamuona mtu yuko wapi,
Kepa nae ule mpira sio wa kumpita.
Sio tu Azpi, timu zinazojilinda vizuri kila mchezaji alitakiwa kukimbia kuzuia, hivi karibuni wachezaji wa Chelsea wamegeuka watazamaji mipira ya hatari kama zile. Walitakiwa wabashiri kwamba Silva akipoteza itakuwa na madhara ili wawahi kucover nafasi ila badala yake jitihada za Chelsea kujilinda hivi karibuni imekuwa hovyo tangu akina Rudiger na Christansen waondoke
 
Maurizio Sarri has revealed that he needs N'Golo Kante to stay close to Jorginho when defending as the Chelsea star is 'not very good in open spaces.

"With the ball on the other side, he has to stay very close to Jorginho. Otherwise it's a big problem for us".
Tangu wamuondoe Kante kwenye Holding Midfield, Chelsea back 4 inakuwa too much exposed under Jorginho or any other Chelsea Midfield labda aje mwingine mwenye uwezo wa kukata umeme, Sio Jorgninho au Kovacic au viungo tulionao, Hata Zakaria akiwa mzuri hataweza kukata umeme. Waliowezaga hii kazi ni akina Makelele, Michael Essien
 
Hapa tumepigwa . Huyu kocha tumepigwa, hii timu tumepigwa ..usajili tulofanya tumepigwa. Yani kwa ufupi kila kitu tumepigwa. Hatua ya makundi hatuvuki aise naona.
Acheni kuwa wapumbavu basi, yani mechi 1 majibu yote mnayo ninyi.

Hivi mnatakaje maendeleo ya haraka haraka kwa wiki 1 tu ambapo

Kocha mpya
Wachezaji wapya
Mifumo mipya
Mbinu mpya
Formation mpya
Attitude mpya
Malengo mapya
Mkataba mpya

Kweli Mashabiki maandazi wapo kila mahali
 
Timu Jana imecheza vizuri sana na kuna vitu kocha ameonesha
1.Wachezaji wamepangwa kwenye nafasi zao halisi

2. Uharaka wa kufanya mashambulizi, tuna attack haraka kabla mpinzani ajajipanga

3.Press

4.Jorginho for the first time naona msimu Huu Jana kacheza vizuri

Weekness

1.Finishing, ni tatizo limeendelea kututesa Sana wachezaji wanakosa magoals Sana huwezi kulaumu hapa kocha ikiwa tunatengeneza nafasi nyingi lakini tunashindwa kutumia nafasi

2.Nafikiri kwenye pale sub asingemtoa Auba tungecheza na double striker Auba na Broja kwa zile nafasi za wazi alizokosa Ziyech angekuwa ni Auba zinge kuwa goal

NB: kocha anahitaji muda kwa aina la soka lake naona atafanikiwa pale chelseafc tumpe muda
Mbona kama jana Sterling alicheza kama wingback fulani hivi au?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom