Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Utayatumia kumsajili nani, kila mahali tunapopeleka ofa inapigwa chini?
City wakimnunua Kane na Grealish hawatakuwa salama
Na taarifa zinasema kuwa city wakimsajili Grealish kwa mil 100 deal la Kane litakuwa limekufa kifo cha mende
 
Roman Abromovich hajawa maskini kiasi hicho.
Pesa za naman hiyo itaingiza timu kwenye matatizo ya kisheria ya matumizi mabaya ya pesa kutokana na sheria za UEFA - FFP
Klabu hairuhusiwi kutumia zaidi ya kipato chake cha halali.
Kuuza wachezaji na vipato vingine kama za kushinda makombe kushiriki UEFA, mikataba ya matangazo na udhamini ndio njia pekee ya kubalance mahesabu
 
1627972222933.png
 
Udinesse wamewafuata Chelsea FC kuhusu Armando Broja kumtaka kwa mkopo mpaka June 2022. Mazungumzo yanaendelea baada ya kuongeza mkataba Chelsea siku chache zilizopita..

[Fabrizio Romano]
 
Kuna watu wanalalamika kwa nini Chelsea haiko serious kwenye madirisha ya hivi karibuni
Kama unafuatilia Chelsea huwa inafanya manunuzi mapema sana au ikichelewa inachelewa kwelikweli
Je unajua kwa nini?

Ulishaenda sokoni au dukani kufanya manunuzi na mzungu
Au ulishawahi kwenda sokoni au dukani kununua kitu ukiwa na gari la bei mbaya imepaki hapo pembeni mwa duka
Walahi utapandishiwa bei hadi ukome kwenda na mzungu au Gari la bei

EPL kuna timu tatu zikiingia sokoni bei za wachezaji huwa zinapanda automatically
Chelsea na Man city zinaongoza kwa sasa ikifuatiliwa kwa mbali na Man United
Hizo timu zingine hawasogelei kabisa kwenye duka Chelsea au Man city au Manure anafanyia shopping

Kinachoipa Chelsea shida sasa kwenye manunuzi ni bei kupaa
  1. Jules hakuwa wa Euro mil 80
  2. Lukaku sio wa Euro mil 150
  3. Haaland labda Euro mil 120 lakini sio wa Euro mil 175
Sasa kwa sababu tumeamua kuwa wazungu itabidi tupambane na hali hiyo
 
Udinesse wamewafuata Chelsea FC kuhusu Armando Broja kumtaka kwa mkopo mpaka June 2022. Mazungumzo yanaendelea baada ya kuongeza mkataba Chelsea siku chache zilizopita..

[Fabrizio Romano]
No no, huyo abaki na kama anaondoka wamlete Haaland au Lukaku kwanza
 
Kwa maoni yangu naona deal la Haaland au Kane ndio rahisi kuliko la Lukaku
  1. Dortmund wakipewa ofa nzuri watapokea kwa sababu hata mwakani anaweza kuondoka kwa bei rahisi karibu nusu ya pesa ambayo wangepata msimu huu. Na pia Dortmund wameshamnunua replacement wake.
  2. Harry Kane anaonyesha kuwa na ugomvi na bodi kwa sababu ya ukame wa Spurs kwenye vikombe, na naona Kane kakasirika zaidi baada ya England kutoka kapa kwenye michuano ya Euro 2020. Sasa Chelsea wakitoa ofa nzuri kwa Spurs wanaweza kumuachia kirahisi.
Dil la haland ni rahis kama tuko tayar kuchoma 200M kwa yeye tu
Maana mchezaj pekee ni €150-170M bado hujampa Raiola na baba yake haland 50, hapo ndipo ugumu unapoanzia,
Ila ndani ya wiki hii na wiki ijayo mwanzon tutakuwa tushapata majibu, tho kwa tim wanaona usajil w lukaku ni rahisi kuliko w haland
 
Deal la Jules Kounde pia halipo, tusiwe na matumaini bandia hapa
Sevilla wanataka Euro mil 65 na ni cash wanataka tena hapo wameshusha maana ilikuwa mil 80
Chelsea wanaweza tu kufikiria kumnunua Jules kama Zouma atauzwa na sio chini ya Euro 35 milioni, bei ya chelsea walioweka kwa Zouma ni Euro mil 29 tu,
Timu zinazomuwania Zouma ni Spurs, Westham na Palace. Westham wamesema waziwazi kuwa hawawezi kulipa Euro mil 29 kwa Zouma bali wao wametoa Euro Mil 23
Kwa hiyo usajili wa Chelsea dirisha hili ni mgumu kweli kweli ukiondoa usajili wa kipa
Bado dakika za kusajili zipo ila sioni kama zitatosha kwa usajili wa maana kama wa Haaland, Kane na Lukaku
Fabrizio n other reliable source zinasema chelsea watamsajil kounde haijalishi mchezaj amewekwa au hajawekwa ila watamsajili tu, ngoja tuona kama maamuzi yatabadilika kwa tim
 
Haaland January anasign mkataba mpya kuendelea kusalia Dortmund. Kuondoka kwa bei rahisi futa kichwani.

Dortmund sio wajinga kiasi hicho. Wakatae kumuuza sasa hivi kwa dau kubwa ili aondoke mwakani kwa dau dogo? Haaland amewahakikishia atasign mkataba mpya
Halland anakuja Old Trafford mwakani, nyinyi kumfuatilia ni kupoteza muda wenu bure.
Tunza hii comment.
 
Haaland January anasign mkataba mpya kuendelea kusalia Dortmund. Kuondoka kwa bei rahisi futa kichwani.

Dortmund sio wajinga kiasi hicho. Wakatae kumuuza sasa hivi kwa dau kubwa ili aondoke mwakani kwa dau dogo? Haaland amewahakikishia atasign mkataba mpya
Akifanya hivyo ataishia kuwa kama Kane na kama ana akili hatasaini mktaba wakati kuna timu zinamfukuzia na mshahara mnono
 
Hao wote tupa kule, tumchukue Ivan Toney
Chelsea wame peleka bid ya pili kwa Lukaku
Tunasubiri majibu

Huku nyuma niliwahi kumtetea Lukaku kuwa ni mfun gaji mzuri kuliko strikers tulionao na kuna baadhi wanamkebehi na kumuona hafai kwa sababu ya uzito wake

Kwangu mimi Lukaku anatetewa na takwimu za ufungaji wake, ni striker mwenye uwezo wa kuforce magoli na yuko sharp na anaona goli hata kama physically haangalii goli. Ana uwezo wa kukaa na mpira na kwa umbile lake ni stable na ni ngumu kumshinda kwa ugali

Chelsea leteni Lukaku darajani, hatutaki sura nzuri za mastrikers kama ya akina Morata
Tunahitaji mharibifu kule mbele, mtu asiyetumia demokrasia kwenye kufunga, mtu ambaye akiwa mbele unajipigia tu mpira uende mbele yeye anajua cha kufanya na huo mpira

Wenye uwezo huo kwa sasa ni Haaland, Kane na wakishindikana hao wawili basi Lukaku ni option ya tatu
 
Chelsea wanaandaa bid ya tatu ya euro mil 120+ Alonso kwa ajili ya kumleta Lukaku Darajani. Nimesikia pia kuwa Inter hawatakataa hiyo ofa
kwa hiyo tujiandae kisaikolojia
 
Chelsea wanaandaa bid ya tatu ya euro mil 120+ Alonso kwa ajili ya kumleta Lukaku Darajani. Nimesikia pia kuwa Inter hawatakataa hiyo ofa
kwa hiyo tujiandae kisaikolojia
Cha kuomba hasa aje ang'ae, daah
 
USAJILI WA MSIMU HUU VICHEKESHO!!

📌timu nyingi hazitaki kuuza wachezaji wao hii inaonyesha vilabu vingi havina tamaa ya fedha kila mtu anataka makombe😂😂

📌HARRY KEANE - huyu mwamba amesusia mazoezi jana akishinikiza kutaka kuondoka ndani ya klabu tottenham na anataka kuelekea katika klabu ya man city, mwanzoni alikuwa akisikilizia kuona labda inawezekana tottenham ikamuachia lakini baada ya kuona tottenham wamegoma kumuuza huku man city nao wakiachana nae na wakamgeukia jack grealish ikabidi aweke mgomo baridi na kushinikiza kuondoka.

📌Ikumbukwe jamaa anatuzo binafsi za kutosha kwake anachotamani ni medali na makombe😂😂😂

🔵Sasa hili kumkomoa klabu ya tottenham imeweka dau la £160m ni sawa na €200m kwa timu yoyote inayomtaka harry kane😂😂😂

📌LUKAKU - Intermilan imegoma kumuuza lukaku kwa Chelsea Football Club licha ya chelsea kupeleka ofa ya €100m pamoja na alonso lakini ofa imekataliwa tena wamesema kama chelsea wakitaka kumnunua wasubiri mpaka mwaka 2024 na watamnunua kwa bei chee ya €7.5m tu🤣🤣🤣

🔴Lakini cha ajabu intermilan kumuuza lukaku hawataki badala yake wanataka #Chelsea iwauzie ALONSO🤣🤣

HAPA NI MWENDO WA KUKOMOANA TU!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom