Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

We may take both ladies
1620289459033.jpg
 
Kweli nimekubali kwamba Kumbe Benchi la Ufundi ni Muhimu saaaana, timu hii hii iliyokuwa ina matobo nyuma leo hii inamelemeta kweli....jamani

Huyu huyu Rudiger aliyekuwa anajikwaa watu wanapita amesimama leo hii ni kisiki cha mpingo..kweli jamani
Huyu huyu Zuma waliyekuwa wanasema mzee kijana leo hii ni Super Star....

Ama kweli KOCHA ni kitu muhimu sana, hata mtaa wa saba nao wanaweza kuanza kucheza mpira sambusa na kuacha ule kwa kwao wa nitangulizie nitakuta nao huko huko...

Kweli, Benchi la ufundi ni kila kitu.. Kwa Lampard, sidhani kama Chelsea ingefikia hapa ilipofika - Top Four, Final FA Cup, Fina UEFA...
 
Nyie mtajuta kuja final ...

Tunawawashia moto mpaka mtakimbia uwanja ..

Kuna takataka zinatembelea historia ,ooh sijui 2012 tulichukua ,wakati saizi tupo 2021 [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Naona unaongea kishabiki zaidi kuliko kimpira

Wakati wa lamps chelsea ilikuwa inaruhus magoal kiasi gani,
Kufungwa 5 sio sababu useme kocha hana mbinu,
Sir Alex Ferguson alifungwa 6, guardiola alifungwa 5 msimu huu utasema alikuwa hana mbinu, kufungwa katika mpira huwa kupo tu hata uwe na mbinu kiasi gani kuna mechi utafungwa tu, na mtu akifungwa sio hana mbinu kuna siku unakuta kila unachokifanya kinaenda ndivyo sivyo ila isiwe sababu ya kusema huyu kocha hafai,
umeongea vema sana mkuu sisi mashabiki tuna tabia ya kutokubali unachokiona bali unakubali unachokiwaza,mimi ni shabiki wa United lakini naona Chelsea imebadilika sana hasa kwenye ukabaji ni wazi kwamba kiufundi Thomas kamuacha mbali sana Lampard.nikivyoona tu ratiba ya mechi za nusu fainali ulaya nakumbuka nilimwambia shabiki wa Chelsea kwamba naziona fainali zote mbili za UEFA na EUROPA zikikutanisha timu za England tupu.
 
Klop alikuwa na historia ipi hasa kabla hajaichukua Liverpool?

Usiwe na ubishi usio na maana, ni heri kujifunza kuliko kujua kila kitu.
Umewahi kuisikia ligi inaitwa Bundes liga? Borrusia? Umewahi kujua kama Klopp kafundisha Borrusia kabla ya Liva?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom