Mbali na ukweli mchungu kuwa Giroud ni bora kuliko Abraham lakini haiondoi ukweli kuwa Lampard anatengeneza long term planning kwa Chelsea na Tammy Abraham ili aje awe mchezaji bora huko mbeleni lkn si kwa mwaka m1 au miwili ijayo tu.
Kelvin De Brune na Mohamed Salah walichukuliwa poa mno na kuachwa Chelsea lkn sasa hivi tunaona moto wake jinsi wanavyong'aa ktk soka bora baada ya kuaminiwa na kupewa muda wa kutosha na akina Klopp na Pep.
Kumbukeni hata Raheem Sterling naye alikuwaga kimeo vivyo hivyo akiwa Liverpool lkn Pep alimuamini kwa kumpatia muda mwingi wa kucheza hatimaye alikuja kutisha na kuwa mchezaji tegemezi ktk kikosi cha Man City na hata England National Team.
Nawaomba washabiki wezangu tuendelee kuwa na uvumilivu tusiwe na mihemuko na Kocha wala Wachezaji kwa kutaka mafanikio ya haraka haraka.
Ilivyomgharimu Juggen Klop kutengeneza timu kwa zaidi ya misimu mi3-mi4 kuisuka Liverpool hadi ikawa na football chemistry nzuri England hadi Ulaya nzima ndivyo pia inapaswa kumvumilia Lampard ambaye hajamaliza hata msimu m1 na wachezaji aliowasajili.
Ikumbukwe usajili wa wachezaji wapya zaidi ya 8, watahitaji muda wa kumuelewa kocha na kuzoeana ndipo tutamtendea haki Lampard kumuhukumu ubora na ubaya wake.
Sent from my ONEPLUS A3010 using
JamiiForums mobile app