CHELSEA 4-0 CRYSTAL PALACE, Premier League: Post-match reaction
By Mr blue
Siku nzuri kwa Ben Chilwell pamoja na Kurt Zouma bila kumsahau Jorge Luiz Frello Filho pamoja na Jeshi zima la Chelsea fc. Nianze kwa kuwakumbusha wapinzani wetu kuwa, Ben Chillwell ndo kwanza anaumri wa miaka 23. Yani ndo kwanza anaanza[emoji16]
Kai Lukas Havertz huyu ndo real No.10. Dah[emoji847] hii style yake ya uchezaji inavutia mno.
Okay, match ilianza ikiwa na delay ya dakika kibao kutokana na Crystal Palace kuchelewa kutoka kwenye dressing room. Crystal Palace walikuwa wagumu sana kipindi cha kwanza wakicheza defensive zaidi. Chelsea ilikuwa juu upande wa possession pamoja na shots kadhaa kabla ya kwenda mapumziko.
Wakitumia mipira ya counter attack, Chelsea ikiongonzwa na Miamba wanne, chini ya Mikopo safi ya César Azpilicueta, Kurt Happy Zouma, Tiago Silva pamoja na Man of the match Ben Chilwell certainly been a familiar sight for Chelsea, but on the plus side, tulifanikiwa kuzizima zile counter threat na kumuweka mfukoni Zaha dakika zote za mchezo.
Chelsea tulirejea na purpose kubwa katika second half, na hatukukawia sana kuzichana nyavu mara baada ya Callum Hudson-Odoi kumnyang'anya mpira Sakho na kumtengea Ben Chilwell aliyefanya mauwaji ya kimbari dakika ya 50.
Chelsea iliongeza pressure na kufanya mashambulizi kupitia mipira ya pembeni. Alikuwa Kurt Happy Zouma dakika ya 60 aliyefunga bao safi kwa kichwa kutokana pasi safi kutoka kwa Ben Chilwell na kumuacha Guaita asijuwe la kufanya.
Crystal Palace waliamka na kutaka kujitetea, but Chelsea iliwakandamiza bao la tatu dakika ya 79 kwa Njia ya Penalty iliyofungwa na Jorge Luiz Frello Filho mara baada ya Tammy Abraham kuchezewa visivyo.
Haikuchukuwa muda kabla ya Jorge Luiz Frello Filho kutunyanyua tena dakika ya 82 alipofunga Penalty nyingine mara baada ya Kai Lukas Havertz kuangushwa ndani ya penalty box.