Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

1594679320997.png

1594679397540.png
 
Hahahahaha mmetusema sana, mmetunanga sana, mmetutukana sana, kwamba sisi hatufai, takataka, viazi, bomu la kutupwa, tumekata uno.

Kashfa zote tumezipokea, tunafahamu timu yetu ni mbovu, uwezo wa kumaliza top 4 tumemwachia Mungu.

Haya tunaomba mrudi kwenye majukwaa yenu, mtupishe tujadili uozo wa mechi ya jana.
Huna haja ya kuwafukuza hawa, watajifukuzisha wenyewe
 
Sasa ninyi ndio mngetaka apigwe BAN si ndio?

Jana Manure walifurahi sana kuondoshwa kwa Ban ya Man City wakiamini kuwa atakaye komolewa ni Chelsea kuwa ataikosa Top 4,
But huenda kibao kikageuka, Manure watakuja kuililia Ban ya Man City kuondoshwa kwa kusema haki haikutendeka.
 
Kipindi cha pili hawakuwa na on target hata moja au nmeelewa vibaya
Hiyo ilikuwa ktk dkk za 70 hivi ila full 2nd half ni hii wamepigiwa pira la kufa mtu hapohapo uwani kwao,hawajapiga ontarget hata moja
Screenshot_20200714-081032.jpg
 
Leo tunacheza na Norwich city ambayo imeshashuka daraja, kocha na wachezaji wao wameshavunjika moyo.

Kazi kwetu Chelsea kuingia kwenye hii mechi kwa kusaka point 3 muhimu kwa hari, moyo na nguvu kubwa.

Kuna wachezaji wa Norwich city watataka kuonyesha juhudi binafsi kuzishawishi timu zinazobaki ligi kuu ziwanunue, pia timu yao itacheza very comfortable hawana tena la kupoteza, wakavuruga mipira matokeo yake tukapanda mlima.

Lampard asiwadharau hawa Norwich akapanga kikosi dhaifu tutambulia aibu.

Zaidi Lampard ajipange kimbinu, awaandae wachezaji kiakili na kimorale.

Pulisic - Giroud - Willan

Kovacic - Joginho - Mount

Azipu - Tomori - Zouma - James
Sidhani kama Tomori ataanza, ndio tu katoka majeruhi. Christensen anaweza kuanza kwa maana yuko fit
 
Wale Southampton wanaitwa "The Saints" maana yake Watakatifu wa Bwana"
Na wale wengine wanaitwa "Red Devils" maana yake Mashetani wekundu
Tatizo ni mashetani walicheza na watakatifu
Tangu lini Shetani akamshinda Mtakatifu wa Bwana?
 
Leo tunacheza na Norwich city ambayo imeshashuka daraja, kocha na wachezaji wao wameshavunjika moyo.

Kazi kwetu Chelsea kuingia kwenye hii mechi kwa kusaka point 3 muhimu kwa hari, moyo na nguvu kubwa.

Kuna wachezaji wa Norwich city watataka kuonyesha juhudi binafsi kuzishawishi timu zinazobaki ligi kuu ziwanunue, pia timu yao itacheza very comfortable hawana tena la kupoteza, wakavuruga mipira matokeo yake tukapanda mlima.

Lampard asiwadharau hawa Norwich akapanga kikosi dhaifu tutambulia aibu.

Zaidi Lampard ajipange kimbinu, awaandae wachezaji kiakili na kimorale.

Pulisic - Giroud - Willan

Kovacic - Joginho - Mount

Azipu - Tomori - Zouma - James
Kupanga tomori.james na azip kwa pamoja inakuwa ni ngumu kidogo.. Kwa maana hao wote ni wafupi mipira ya juu inawasumbua...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom