MANCHESTER CITY 2-1 CHELSEA, Premier League: Post-match reaction
By Mlanzi
It's okay it's okay sote tulizitaka points tatu na kingine tulitaka sana kuona kiwango chetu dhidi ya Manchester City. Sure vijana yalikuwa na sloppy mistakes but kiwango chetu kilikuwa kizuri ukizingatia tulikuwa nyumbani kwa City. Amini usiamini, kuna mambo mazuri yanakuja katika kikosi chetu.
Pamoja na mambo mengine, Kepa Arrizabalaga Revuelta alikuwa average kiasi katika hii game. Fikayo Tomori alikuwa mzito kiasi cha kupigwa tobo lililozaa bao. Kurt Zouma na Jorge Luiz Frello Filho a.k.a Jorginho walikuwa down kiasi. Nadhani hangover ya International break imechangia japo kuwa defence yetu ilikosa umakini.
Team iliuanza vyema mchezo tena ikienda mguu kwa mguu na wenyeji. Bao la kwanza kutoka kwa N’Golo Kanté dakika ya 21 kijana anaelifahamu vyema lango la Manchester. Team iliendelea kuleta matumaini huku ikionekana ku dominate mchezo.
Kosa la kupoteza mpira katika midfield liliwapa City chance ya kusawazisha kupitia kwa De Bruyne. Poor defending kutoka kwa defense yetu iliwapa Manchester City nafasi ya kuongeza bao kupitia kwa Mahrez.
Second half ilikuwa imetawaliwa na City huku wakitengeneza chances zao kutokea kwenye middle.
Mabadiliko mawili kutoka katika game yetu iliyopita ambapo César Azpilicueta alirejea katika nafasi yake na badala ya Reece James, na Jorginho kurejea kutoka katika suspension badala ya Mason Mount kukamilisha three-man midfield wakiwa sambamba na N’Golo Kanté pamoja na Mateo Kovačić.
James aliingia upande wa kulia na kupishana na Cesar Azpilicueta mala baada ya Emerson kupumzishwa.
Dakika ya 73 team ili switch na kuanza kutumia 4-2-3-1 baada ya Jorginho kumpisha Mason Mount, na Mitchy Batshuayi kumpumzisha Tammy Abraham.
Bao la N'golo Kanté’s ni bao la tatu msimu huu
City wanakuwa points tisa nyuma ya Liverpool na Chelsea tume-drop mpaka nafasi ya nne tukiwa mbele kwa tofauti ya points saba kutoka nafasi ya tano inayoshikiliwa na Wolves kwa sasa.
Next up: tunawafuata Valencia siku ya Juma tano katika UEFA Champions League, na hii itakuwa more important game.
KTBFFH