Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Shukrani k wa dondoo za yaliyojiri jana, Nimeangalia highlights za match yetu na ajax.

Mimi ni mmojawapo wa mashabiki waliokuwa na imani kwa KEPPA nikiamini baada ya match kadhaa angekuwa moto. NAFUTA RASMI IMANI JUU YAKE.

Kipindi cha babu SARI alitoa clean sheet nyingi kwa aina la soka la SARI BALL kucheza sana nyuma, kwa soka la LAMPARD la kushambulia MADHAIFU ya KEPPA yanaonekana waziwazi.

Kwanza style yake ya kuruka kidogo kabla ya kudaka mpira inaniuzi sana, hii style yeye anaona inampa confidence lakini inamuuza sana. Angalieni clip zake za udakaji lazima aruke kidogo kabla mpira hajapigiwa.

Hongereni kwa draw. Valencia lazima tumfunge lasivyo tutaaga mashindano.
Itakuwa gemu ngumu sana ya kukata kwa shoka.
 
CHELSEA 4-4 AJAX, Champions League: Post-match reaction, ratings

By Mlanzi

Ngoja nianze na Reece James raia wa England ambae anaupiga kama professional player na nafasi yake uwanjani ni full back. Mwezi December tarehe 8, mwaka 1999 ndio alizaliwa pale London Borough of Redbridge, United Kingdom, na sasa ametimiza umri wa miaka 19. Bao la Reece James ndo bao lililoturejesha kileleni katika ile comeback ya kihistoria dhidi ya Ajax.

Kabla sijasahau, first half Ajax walikuwa 3-1 huku wakiwa na shuti moja tu on target, meaning sisi tulikuwa tumejifunga mabao mawili yani 2 own goals.

Zile red cards mbili kwa Ajax zote zilikuwa sahihi kabisa, Tadic alimchezea leg breaker Tammy Abraham na Veltman alikuwa ameushika mpira ndani ya box kosa linalozaa yellow card na penalty juu. Tunahaki ya kujipongeza kwa hii comeback japo tulikosa umakini katika first half. Marcos Alonso ameniangusha kile kiwango hakikuwa cha UEFA Champions League alionekana kuwa chini sana.

Second half ilikuwa powa sana na kama kawaida yetu tulikutana tena na mkono VAR baada ya bao safi kutoka kwa Cesar Azpilicueta kukataliwa kwa kile kilichodhaniwa kuwa handball kutoka kwa TammyAbraham. Hii ilikuwa moja kati ya zile crazy game.

Ndani ya dakika 90+ mambo mengi sana yalijitokeza. Kwanza own goal kutoka kwa Tammy Abraham ndani ya dakika mbili za mwanzo. Pili, Christian Mate Pulisic kushinda penalty iliyotiwa kambani na Jorginho ndani ya dakika tano za mchezo. Tatu, Tammy Abraham kutupia kutokana na through ball ya Mateo Kovačić na bao kukataliwa kutokana na kuwa offside.

Nne, Ziyech wa Ajax kufunga bao tamu kwa njia ya freekick kutoka upande wa kulia mwa uwanja na Kepa Arrizabalaga kujifunga wakati akiokoa.

Tano, Marcos Alonso kupumzishwa half na Reece James na kumfanya Cesar Azpilicueta kuhamia katika left back.

Sita, Kurt Zouma kufanya Maradona-esque style kwa kukimbia na mpira umbali upatao 70-yard na kukosa kosa kufunga.

Next up tutawakaribisha Crystal Palace pale Stamford Bridge katika Premier League siku ya Juma Mosi

KTBFFH
Sijasoma yote kwa sababu ya haraka ila huyo Alonso ni feki, hatufai Chelsea kabisa bado anasinzia na hajitambui kabisa
 
Wewe sio shabiki wa Chelsea na wala mpira hujui. Batshuayi anajulikana na wanaojua mpira, mpaka Batshuayi sio kaliba ya Chelsea, kumtegemea Batsuayi akupe magoli 9 kwenye mechi 11 ni ndoto za alinacha au hadithi za abunuasi.
Hazard Don kachemka sana hapo ndiyomaana mi sikupoteza hata muda kumjibu.

Hivi kaliba ya Diego Costa au Didie Drogba uifananishe na Batshuay Makiri Kiri? [emoji4]
 
Penati 2, kadi 2 nyekundu

Wale waliokuwa wanaponda penati pindi Man Utd wanapopata sidhani kama nitasikia tena kelele zao
Tutaendelea kuponda penalty Ndugu hata kama imetuvusha sisi. Chelsea tulicheza vibaya na Ajax walituzidi na goli zingekuwa 7-9 jana lakini hata magoli ya mkono yanampeleka bingwa mbele kwa mbele atajirekebisha. Hatujafurahia uchezaji ila matokeo tumefurahia kimya kimya na ndio maana kwenye jukwaa hapa hatuna majigambo sio kama nyie mkishinda kwa vipenalti watu hawalali mtaani
 
Kumpanga Batshuayi ni kutafuta ugonjwa wa moyo, nafasi 4 za wazi atafunga goal 1. Sio striker wa kutegemea kabisa AUZWE.

GIROUD mkataba wake unaisha aondoke.

Tusajili striker mwingine mkali ikiwezekana aingie moja kwa moja 1st eleven. TAMMY ABRAHAM yuko soft sana mbele ya goal.

Kwa Chelsea hii ya mpira mwingi namkumbuka sana DIEGO COSTA angefunga sana, hana utani, uzembe, masihara mbele ya goal ni aggressive kwenye kufunga.
Uzuri wa Tammy zikitokea nafasi hapotezi japo sio mchezaji wa kutafuta mpira kwa sababu yeye sio type ya akina Messi wanaojua kudrible
 
Kumpanga Batshuayi ni kutafuta ugonjwa wa moyo, nafasi 4 za wazi atafunga goal 1. Sio striker wa kutegemea kabisa AUZWE.

GIROUD mkataba wake unaisha aondoke.

Tusajili striker mwingine mkali ikiwezekana aingie moja kwa moja 1st eleven. TAMMY ABRAHAM yuko soft sana mbele ya goal.

Kwa Chelsea hii ya mpira mwingi namkumbuka sana DIEGO COSTA angefunga sana, hana utani, uzembe, masihara mbele ya goal ni aggressive kwenye kufunga.
Hapo ndipo ninapozidi kumwona Conte ni mpuuzi tu, ugomvi wako wewe binafsi na mchezaji afu uuze Forward tegemezi no 1 kabisa wa timu? Daaah...[emoji57][emoji849]
 
Jana kapoteza vichwa karibia vitatu vya wazi kabisa, Tammy si wa kumtegemea sana katika mechi ngumu 7bu bado ni mteke sana.

Abraham angekuwa mkomavu kama Batshuay wala nisingesapoti kuwaza usajili wa striker mwingine.
Uzuri wa Tammy zikitokea nafasi hapotezi japo sio mchezaji wa kutafuta mpira kwa sababu yeye sio type ya akina Messi wanaojua kudrible
 
Nakwambia tena ba tena.. kamwe usimuamini batshuati.. labda wewe umeanza kumuangalia msimu huu..

Huyu sio foward wa kumtegemea kabisa...
Batshuay ni forward nzuri sana kuliko Tammy ,pia hapewi sana nafasi kama Abraham.
Mo sarah alipokuwa Chelsea alikuwa akipigwa benchi. Kila kocha anamtu wake.
I'm sure mpaka msimu uishe ubora wa batshuay utakuwa ushaonekana.
 
Nafasi tatu umeziona wapi wakati hukutazama mpira? Aina ya mashabiki ambao hawaangalii mpira hampaswi kuongea ovyo ovyo
Jana kapoteza vichwa karibia vitatu vya wazi kabisa, Tammy si wa kumtegemea sana katika mechi ngumu 7bu bado ni mteke sana.

Abraham angekuwa mkomavu kama Batshuay wala nisingesapoti kuwaza usajili wa striker mwingine.
 
Unajua king Ngwaba sometimes unakuwa unakoment vitu utadhani mtoto wa kike,kwahiyo ulitegemea watu wacheze fouls waachwe tu bila kupewa adhabu ili ufurahishwe wewe.

Umenikosea heshima

Kuna Mtu aliuliza swali kuwa kaona Makala nyingi zinasema Ajax kaonewa akata kujua sababu kwanini wanacomplain kuonewa (Nadhani hakuangalia game).

Mimi Nikamjibu wanalalamika kwa sababu ya 'Red Cards' mbili.

Nilimjibu kiufupi

The rest sihusiki na ufahamu wako juu ya kile nilichokiandika
 
Kabisa Chifu, kuna baadhi ya mechi epl hata UEFA huwa zinahitaji undava la sivyo ukiwa mlaini laini huwezi kuchungulia goli kirahisi na hicho kitu walikuwaga nacho akina Diego Costa na Didie Drogba tu pale Chelsea.
Kabisa mkuu very soft. Akikosa magoli anamuachia Mungu. COSTA alikuwa anasaka goal kwa njia yoyote iwe kupewa assist, uwezo binafsi, nguvu, vikishindikana vyote anatumia ubabe, ujeuri hata usanii kuwatafutia kadi mabeki wachanganyikiwe.

beki Van dijk anaonea dagaa sio kwa mnyama COSTA.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom