Chelsea inategemea kumruhusu Giroud na Pedro kuondoka mkataba ukiisha. Pia Batshuayi atauzwa ili kuruhusu safu mpya ya ushambuliaji wa kuja kushirikiana na Tammy Abraham.
Willian naye pamoja na kuwa bado anatakiwa kwenye timu lakini bado hajatia saini kwa mkataba wa mwaka mmoja, yeye anataka miaka miwili
Uongozi wa Chelsea umempa Lampard paundi mil 150 kuboresha safu ya ushambuliaji na wanaolengwa ni Jadon Sancho wa Borussia Dortmund, Wilfred Zaha wa Crystal Palace na Moussa Dembele wa Lyon. Walengwa hasa ni Zaha na Sacho
Pia Chelsea wana mpango wa kuimarisha safu ya ulinzi kwa kumsajili Ben Chilwell LB wa Leicester city na kumnunua Nathan Ake wa Bournemouth kama mkataba wa mauzo unavyoiruhusu Chelsea kumnunua kwa paundi mil 40