Hahahaaaa na mimi siwezi kuwa na mwalimu kama wewe ningekufukuza darasani kwani hauna madini,
haya ndio yanayotokea kule united muda huu, wanalalamika kuuzwa wachezaji wakubwa kina herrera,sanchez na lukaku bila kusajili mbadala wake na kocha kuamua kutumia vijana wa academy....
Sasa jiulize swali je, wale kina Greenwood,Chong,Rashford wangekuwa wanafanya vizuri hivi vilio ungevisikia????
Ndio hili linalotokea Chelsea leo hii mnapamba timu na vijana wenu kwa kuwa wana upepo mzuri kwa sasa wanafanya poa,ila upepo ukikata hao madogo vile vilio vya united vitahamia humu nakwambia,mtaanza kukumbuka hazard mpaka morata mtamtaka kama united walivyokuwa wanamkashifu lukaku leo hii wanaona bora angebaki....
Washabiki wa mpira hawajawahi kuwa wanafki hata siku moja,timu ikifanya poa wanashangilia ikivurunda wanazomea...
Na hizi timu 6 za juu hazinaga muda wa SUBRA
Suala la muda tu