Sidhani kama wewe kweli ni mtu wa Chelsea, Uongozi umeamua hivyo kwa sababu zao wanazozijua, lakini kwa mtu wa Chelsea na mfatiliaji mzuri utaona bila kificho ni nini kilichokuwa kinaendelea pale Darajani, Chelsea chini ya Mou haiwezi kamwe kufungwa zaidi ya mechi nne nyumbani kwa msimu mmoja,
Kwa mpenzi mzuri wa mpira hata kama uko team nyingine huwezi kufurahia Jinsi wachezaji wa Chelsea walivyokuwa wanafanya, unaweza kufurahia na kuwakejeli Team inayofungwa kama kweli wamezidiwa uwezo na mbinu za kimchezo, lakini sio team inayoamua kujifungisha na kucheza chini ya kiwango
Mou Kaondoka sisi tutabaki, lakini nimesikitishwa sana na fitna zilizokuwa zinafanywa wazi kabisa na wachezaji wetu, ni fitna za kiswahili kabisa, imagine team inashambulia adui na adui yuko ndani ya peessure kubwa, adui anabahatika kubutua mpira mpaka katikati ya kiwanja na kuwakuta wachezaji wenu watatu na adui mmoja, mchezaji wenu baada ya kurudisha mpira kwenye team iliyo under pressure anaamua kwa maksudi kabisa kurudisha mpira kwa kipa wake ili adui apate relief,
Kwa taarifa yako tu wengine ni wafuatiliaji wazuri sana wa team yetu pendwa na tatizo tangu mwanzo tuliliona na Mou alikuwa analijua
Again mpaka sasa sipati picha inakuwaje Pro wakubwa kabisa wanakubali kujidharirisha kwa kiasi kile?
CC: Ntuzu,
Mentor,
everlink,
peterchoka,
kalou,
Rondo,
Wacha1