Asante kwa maoni yako mazuri, ila labda nikufahamishe vizuri, kila kocha anakuwa na mfumo wake wa kujenga timu na pia anakuwa na mfumo wake wa ushindi,
Kwa Mou, timu yake inaanzia kufunga/ ushindi kutokea kwenye defence, na ndio maana unakuta madefender kama Terry au Inanovic wana magoli mengi kuliko mabeki wote wanaocheza EPL, na hata kama umechunguza vizuri mara nyingi Chelsea wanapenda kutumia Striker mmoja tu na wanaweza kuwa zaidi kama hali sio nzuri
kwa Muktadha huo, baadhi ya wachezaji wa Chelsea hawawezi kucheza vizuri kwa sababu ya kulegea kwa mfumo wa ulinzi, Fabregas hawezi kupata support nzuri kutoka kwa Matic kwa sababu Matic sasa ndio amekuwa kama namba nne, Hazard hawezi kucheza kwa sababu Terry na Inanovic na Fabregas hawachezi kwenye kiwango chao,
kama ulishawai kuichunguza Chelsea vizuri, last season Fabregas alikuwa anacheza kama mchezaji huru kiwanjani, Terry na inanovic walikuwa wako kwenye form, hivyo Matic likuwa anapanda vizuri na fabrigas alikuwa anafungua na kujikuta yupo huru kila saa na ndio maana alitengeneza magoli mengi kwa sababu alikuwa na muda wa kujipanga na mpira
shida kubwa ya Chelsea kwa sasa ni beki wa kati, ukiangalia vizuri Zouma, Terry na Cahill wote wanacheza almost namba moja yaani wote ni watu wa mwisho, so combination yao haiko perfect, Zouma anaweza kupanda kidogo, lakini Nafasi ya Terry na Cahill lazima atafutwe mtu, hilo Mou kaliona na analifanyia kazi usiku na mchana
defence ya Chelsea ikitulia na timu nzima itacheza mpiara maridadi mliouzoea kuuona na furaha yenu wote watu wa Man U, Arsenal, Liver ya kuona kabumbu murua itarudi palepale
tunawaomba radhi sana kwa usumbufu mnaoupata kwa sasa