Tatizo jingine linalotukabili ni kutokuwa na spirit ya kumaliza mchezo (hili hata Fabregas alilisemea)
Mara nyingi sana tunapopata goli tunapunguza kasi ya kushambulia, ingawa jana tulijaribu kuendelea kushambulia lakini si kwa kiwango kinachotakiwa.
Tulikuwa na uwezo wa kufunga magoli hata manne (4) kama tungetumia nafasi vizuri, tuliingia mara nyingi sana kwenye eneo lao lakini hatukuweza kufunga, sikuona jitihada kubwa za kutaka kufunga isipokuwa kwa Hazard pekee.
Huyu Costa ndio nimekuwa simuelewi kabisa, sijui kapatwa na nini. Nadhani tunahitaji mshambuliaji zaidi ya Costa.
Jana kama tungekuwa na safu nzuri ya ushambuliaji tungepata magoli mengi maana uwezekano huo ulikuwepo.
Kwa jinsi tulivyocheza, kutolewa UEFA ni sawa tu maana hatukuwa wazuri kiasi cha kuweza kuvuka round hii, ukizingatia timu tuliyokutana nayo, maana hata kwao yale matokeo yalikuwa ni bahati kwetu.
Matatizo yetu ni mawili tu yaliyotugharimu, na huwa yanatugharimu sana tu, na yataendelea kutugharimu kama yasipofanyiwa kazi.
1. Udhaifu katika kudefence mipira ya kutenga
2. Safu ya ushambuliaji kutokuwa na uchu wa kufunga magoli mengi. Huwa tunabweteka.
Mimi binafsi naamini jana tulitolewa si kwa sababu PSG walikuwa wazuri sana bali ni ujinga wetu wenyewe, aliyetazama mpira vizuri ataniunga mkono.
#FOREVER BLUE