Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Chelsea FC (The Blues) | Special Thread

Arsenal-v-Chelsea-Didier-Drogba-celeb_2391174.jpg
 
Sawa mumeshinda nami sina budi kuwapa hongera! anyway own goal, free-kick sio kwamba tulizidiwa kimpira,tulizidiwa zaidi kisaikolojia.

si ndio madhara ya kuwa na timu ya watoto..mkitishiwa kidogo ya na mipira ikigonga miamba hofu inawajaa mnaanza kujifunga ..hahaaaaaaa ..poleni samaki mmeliwa jicho
 
Hongereni sana ,watoto walianza kupiga sana kelele ,mara 4-3-3
 
You all need to shut it and wait for Sunday! maneno meengi, nasema pamoja na majeruhi mpira dakika 90 na bado tuna uwezo wa kuwafunga Chelsea tena sana, kama A/villa na Wigan wameweza kwa nini sisi tushindwe? hatutaki mind games hapa tusubiri j/pili. Na naamini nitaingia hapa jamvini kwenu kifua mbele!!!!


Masanilo!!! Belo atakuwa kafa kwa mshtuko au kaamua kujinyonga. ila kwa Mashabiki wa the gunners nilipenda kuwaambia msihuzunike sana kwa sababu babu yenu alishasema kikosi chake ni cha ushindani na sio cha ubingwa.
 
Hongera sana watani...AB-Tichaz (aka mzee wa mapicha), Masanilo (aka mzee wa Zenj), Peasant, Mvina (aka mzee wa ugimbi), Eglypz etc! Huu mpambano bado ni asubuhi kabisa.....tutajipanga upya.........!
 
Na jana vp? naona watoto walikuwa wanakimbizwa kimbizwa tu, ule mpira wao wanaouita eti full flow football or Intertaning football mbona natukuuona jana? tena kipigo cha nyumbani kwao?

Chelsea walifanya hivi

1. Kutawala vioungo na ku make sure Fab hatambi pale katikati
2. Diamond Mid ni hatari hasa ukipata wachezaji wazoefu kama Essien, Obi, Lampard, Ballack, Mauluda na Deco

Naona sasa mmenza kuona nini maana ya kocha na umuhimu wa kocha kwenye timu, so unakuwa na kocha asiye na uwezo anayegawa wachezaji na majungu ndo yanakuwa yele yale ya scolari na rafiki yake maximo

Habari ndo hiyo.
 
Masanilo!!! Belo atakuwa kafa kwa mshtuko au kaamua kujinyonga. ila kwa Mashabiki wa the gunners nilipenda kuwaambia msihuzunike sana kwa sababu babu yenu alishasema kikosi chake ni cha ushindani na sio cha ubingwa.

Taratibu wewe mimi ni MAN UNITED sio hao watoto wa chekechea,
Tuanawafuata mkipotea stepu tu kama kawaida
 
Hongera sana watani...AB-Tichaz (aka mzee wa mapicha), Masanilo (aka mzee wa Zenj), Peasant, Mvina (aka mzee wa ugimbi), Eglypz etc! Huu mpambano bado ni asubuhi kabisa.....tutajipanga upya.........!

Kila mwaka mtajipanga upya ,now tunawapa miaka 5 mjipange upya
 
Masanilo!!! Belo atakuwa kafa kwa mshtuko au kaamua kujinyonga. ila kwa Mashabiki wa the gunners nilipenda kuwaambia msihuzunike sana kwa sababu babu yenu alishasema kikosi chake ni cha ushindani na sio cha ubingwa.

Belo alitishia sana amani hapa, jana nilikuwa na hamu naye sana uzuri akawa amesepa ushindi raha sana, nani kwenye top four atasimama ngoja niwakumbushe

Tot 0 chelsea 3
Liver fool 0 chelsea 2
Arse 0 Chelsea 3
Manure 0 Chelsea 1

Manure najua watatusumbua kidogo, maana wale huwa hawapotezi mechi za kushinda kama na Wigan ama A villa

Hongera Mbu uliko
 
Taratibu wewe mimi ni MAN UNITED sio hao watoto wa chekechea,
Tuanawafuata mkipotea stepu tu kama kawaida

unajua uzuri wa ushindi wa jana ilikuwa ni two in one. tuliwafunga The gunners direct, ila indirect Man utd nao tuliwapiga, ukitaka kujua hilo tafuta kama utampata shabiki yeyote wa Man utd aliyefurahia ushindi wa wanaume wa darajani dhidi ya vijivulana vya Emiretes.
 
Vile vitoto visubiri kukuwa!

Hongera Mkuu kwa ushindi Mkubwa. Mimi nilishasema kwamba mwaka huu sina imani kabisa na timu yangu maana usajili ulikuwa si wa kuridhisha halafu kumuuza Ade ambaye kwa maoni yangu katika misimu miwili iliyopita alikuwa ndiye mchezaji mzuri ilikuwa ni makosa makubwa sana. Kilichobaki ni kupigania kubaki katika nne bora lakini pia utakuwa ni mtihani mkubwa labda kama watatumia kipindi kifupi cha usajili (Dec to Jan) kuwasajili wachezaji wawili au watatu wazuri.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom