CHATO: Rais Magufuli asema Serikali haitafunga mipaka wala kuwazuia watu kutoka ndani ili kujikinga na maambukizi ya virusi vya Corona

Jamani Mimi naomba mnitoe kwenye mambo zenu za siasa za bongo. Nitauliza maswali nitaomba wajibu wenye kufikiria tu.

Hivi ile hali kama ya Italy ikija Kwetu (God forbid) bado tutasema hivi hivi kwamba sisi tukijifungia ndani hatuwezi kuishi??

Hivi hali ikija km USA sasa je tutakua tunachapa kazi tu ili majirani zetu wapate huduma?
Trump mpk leo wazi wazi ametamka hii kujifungia ndani sitaki kusikia. Na alisema kabisa Easter ntafungua nchi watu wafanye kazi. Lakini Easter ndio hiyo death rate ina surge tu day in day out. Je mbona Trump hafungui nchi? Si hapendi?! Kama ambavo na sisi hatupendi. Kwa wenye kufikiria hapa waseme kwa nini lockdown marekani ipo wakati Raisi roho yake inamuuma uchumi unashuka? Kwa nini?
Umesema USA wamelickdown lakini vifo vinaongezeka. Huoni kama umejibu swali lako mwenyewe kuwa lockdown aisaidii?
 
Utakwenda kwa NANI wakati Kila nchi imefunga mipaka yake
 

Attachments

  • IMG_20200409_001808.jpg
    IMG_20200409_001808.jpg
    99.2 KB · Views: 1
View attachment 1415673

Amesisitiza kuwa Serikali imeamua kutowazuia Watu ndani ya nyumba zao wala kufunga mipaka kwa kutambua madhara mkubwa yanayoweza kutokeza kwa kufanya hivyo.

Aidha, amesema madhara hayo yanaweza pia kuziathiri nchi 8 ambazo zinatengemea kupata huduma na bidhaa kupitia Tanzania hususan bandari ya Dar es Salaam.

Lakini pia amebainisha kuwa kutokana na madhara ya #CoronaVirus upo uwezekano mkubwa wa kutokea kwa upungufu wa chakula, hivyo amewataka Wananchi kuzalisha chakula cha kutosha.

Pia, amesisitiza Wananchi waendelee kuchapa kazi kila mahali walipo huku wakichukua tahadhari ya kutokuambukizwa kwa kufuata ushauri wa Wataalamu na pia wasisahau kumuomba Mungu atuepushe na janga hili.

Rais Magufuli ameyasema hayo alipokuwa akiongea na Waumini wa Kanisa Katoliki katika Parokia ya Mlimani, Wilayani Chato mkoani Geita ambapo alihudhuria ibada ya Ijumaa Kuu.



View attachment 1415488View attachment 1415489
Rais wa Tanzania, John Magufuli akiwa katika Ibada ya Ijumaa Kuu iliyofanyika katika Kanisa Katoliki la Mtakatifu Yohana-Maria Mzeyi Parokia ya Mlimani Chato mkoani Geita leo. Picha na Ikulu
Unajua ni rahisi sana kutoa matamko kama haya ukiwa unadhani huu ugonjwa hauwezi kuchukua uhai wako na ukiwa bado hujaona matokeo hasi ya huu ugonjwa. Huko nje watu wanakufa 400 hadi 1000 kwa siku halafu tunachukulia mzaha. Je hatupendi uhai wetu? au akili zitarudi tukianza kufa? Na msidhani watakufa watu wengine hata nyie mpo kwenye hiyo hatihati ya kufa na huu ugonjwa.
 
Akilitime,
Mbona CHADEMA wamekuharibu akili kiasi hiki. Unadhani Corona ni kwa ajili ya CHADEMA TU. Pendekeza Suluhisho kwa ajili ya Tanzania na si eti kuwakomoa CHADEMA. Hii corona ni ya kwetu wote tuunganishe nguvu sio Swala la kutafutia Sifa.
 
Akilitime, Fuatilia S.A watu wanapinga kwa kuwa serikali haitoi chakula.
Usipozuia watu kutoka kisa wajitafutie ugali utapata maafa makubwa.
Maghala ya taifa hayana chakula?

Na ninyi mnaotoa misaada kwenda serikali hamjifunzi?
 
Chadema wameingiaje hapo? Ndio wanaosababisha uchumi wa nchi kuharibika vibaya ndani ya miaka mitano ya Magufuli? Ndio waliosababisha wakulima wa korosho wasilipwe? Wamesababisha biashara kufungwa? Wamesababisha kusiwe na ajira mpya miaka 5 wala kusiwe na nyongeza ya mishahara? Hizi ndio tabia za nyie na kutumia makalio kufikiri
 
Hongera sana Raisi Pombe.
Wewe Ni kiongozi usiyeongozwa na hisia. Una tabia za uongozi ( acha wanaolalamika walalamike tu maana Ni kazi yao)

Mwagize ndalichako atangaze wanafunzi warudi vyuoni, #Hapa kazi tu.

Tunamtumaini Mungu. Na hajawahi kutuacha tumeonesha imani kwake.
.

Vyuo vifunguliwe maana na vyenyewe Ni sehemu ya kazi.

Tuchukue Tahadhari juu ya Corona , tuwasikilize wataalamu wetu wa afya
Metaphor
 
Yan kagonjwa ka corona ninkadogo ? aisee hizi dhihaka za viongozi na uwongo kwa raia utawakost sana waunga juhudi na watatucost sisi pia daaah aisee, YAN ITALY WAMESHINDWA KWA DINI TUTAWEZA SISI ? sio kweli na TUSIDANGANYANE KABISA WAKUU


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kuna vichaa humu!!
Shule na vyuo vilifungwa tukiwa tuna kesi za ugonjwa kwa watu wanaoingia nchini. Leo Waziri wa Afya anatangaza kuanza kuwa na maambukizi ya ndani (wenyewe kwa wenyewe), bwege mmoja anataka shule na vyuo vifungue!!!
 
Mask siyo kama khanga mkuu. Zina utaalam wake. Ingekuwa ni kitambaa hata leso ingefaa.

Muhimu hapa ni kuwa tuna nchi zinatutegemea. Sisi tuchape kazi tu ili nao wenzetu wasije wakapata madhara.

..mask ya kitambaa au leso ni afadhali kuliko kuji-expose.

..tuchukue tahadhari zote ambazo tunaweza kuzichukua kulingana na mazingira yetu.

..essential transit goods ziruhusiwe mipakani kama huduma kwa majirani zetu, na safari zisizo za lazima zisiruhusiwe.
 
Mbona kama yuko peke yake? Usalama wa viongozi wa kitaifa ni usalama wa taifa, ndio maana makamu wa rais na rais kipindi hiki lazima wana usalama wahakikishe wako salama kiafya ili taifa liwe salama, hawaonekani mara kwa mara wakiwa wamejichanganya katika jamii
Tazama picha kwa makini sana,huyu ni kiongozi mkuu wa nchi,kazi picha macho.
 
Umesema USA wamelickdown lakini vifo vinaongezeka. Huoni kama umejibu swali lako mwenyewe kuwa lockdown aisaidii?
Nlitaka nikuchunie ila ngoja nikujibu.
Trump haku take action mapema alikua akisema we will b fine. We are doing good. It's Chinese virus. ....na kila aina ya BS.
Wakati anayasema haya watu wakaendelea kuambukizwa mmoja baada ya mwingine. Kuja kushtukia the shit has has hit fan already. Lockdown. Too late. Very late. Na lockdown ilikua ya kishkaji. Beaches zilikua zinafurika balaa. Kirusi hakikuwaacha. Sasa ikaja total lockdown. Extremely late. Hivyo hawa wanaokufa ndio walee waliokua locked down wakati it was already late. Ndio hao wanakufa sasa. Kwa nini wanaongezeka kila siku? Sababu watu wako locked down na maambukizi tayar hivyo wanazidi kuambukizana tu. Health system imekua overwhelmed. Total chaos.
Tanzania kwa sasa tuko pazuri. Kama tungefumba macho tukapiga lockdown hata ya mwezi mmoja tu tutakua tumecheza safi sana. Tukisubir maambukizi shazi ndio hayo ya wamarekani yatatukuta.
 
Anakumbuka shuka kumekucha!

Hivi siku zote alikuwa wapi? Au leo alitaka tu auze sura kwenye TV? Kauli yake aliyoitoa leo inatusaidia nini?

Bora tu angejinyamazia kimya huko alikokimbilia.
 
Mzeebaba yupo sawa kabisa, tuna matatizo mengine yanahitaji more attention kuliko hayo mafua ya mizungu. Kufunga mipaka sio suluhisho.
 
Kwanini aligoma kufunga tangu mwanzoni?

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakukua na haja hiyo, huwezi funga mipaka ya nchi hujaanalyze tatizo vizuri kujua effect yake itakuaje, ni obvious mipaka ikifungwa nchi itakua kwenye wakati mgumu sana kiuchumi na ugonjwa wenyewe hata bado ilikua haijulikani kama utasurvive kwenye mazingira kama ya Tanzania ambayo climate ni tofauti.
 
Kumbe upo pazuri mkuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mi hua nasifia panapo sifiwa na napondea panapopondewa sina upendeleo. Kwa hili Magu kafanya la maana sana. Nchi kama Italy zilikua za kwanza kufunga mipaka leo hii wanaongoza kwa vifo. Kufunga mipaka sio solution maana watanzania watarudi tu huwezi fungia wananchi wako wasirudi sanasana utafukuza wageni peke yake ila watanzania watakaorudi nyumbani watauleta
 
Mkuu kwani majirani wakifunga mipaka na sisi Tanzania hatujafunga mipaka ni faida gani tutapata?
Angalau sio sisi tuliofunga ni wao, hapo tayari tuna kadi moja ya kucheza wakitusumbua au tukitaka kitu toka kwao huko mbeleni tunaitumia tunawapiga mkwara na sisi wa kuwafungia mipaka.
 
Back
Top Bottom