CHADEMA, Mungu - Yehova anawapenda. Matukio ya Arusha na Hai ni taarifa njema kwenu.!!

The Palm Tree

JF-Expert Member
Apr 13, 2013
7,951
12,535
It sounds awkward, lakini ndivyo ilivyo. Kwamba iweje ofisi kuchomwa moto iwe ni jambo jema? Iweje msafara wa mgombea Urais Tundu Lissu ushambuliwe mbele ya macho ya polisi liwe jambo jema? Iweje Tundu Lissu ashambuliwe kwa Risasi za kivita za SMG na AK47 iwe ni jambo jema?

Well. Tufutane ili kunielewa.

Mungu aliyetuumba, wakati mwingine huachilia matukio mabaya kutendeka ili ikiwa ni ishara ya kusudi jema la Mungu juu yetu.

Kwa wasomaji wa Biblia naomba warejee hadithi ya Ayubu ktk Biblia. Sio kusudi langu kwenda ndani sana juu ya maisha ya mtu huyu.

Lakini itoshe kusema tu kuwa, ni miongoni mwa watu wachache ktk uumbaji wa Mungu waliopitia nyakati ngumu na za kutisha katika maisha yao.

Katika fikra na mawazo ya wanadamu ni kama vile Mungu alikuwa anamwadhibu Ayubu kwa dhambi zake. Lakini ukweli siyo hivyo. Hali hiyo ya mateso ya Ayubu, iliachiliwa na Mungu mwenyewe ili yeye huyu Mungu kitambo kidogo mbele, apate kujitukuza kupitia shida na mateso ya mtu huyu na kwa hakika ndivyo ilivyokuwa.!

Kwa hiyo, tunaweza kusema hivi. Ndani ya shida na mateso ya Ayubu, alikuwemo Mungu mwenyewe akitenda kazi yake.

Yuko mtu mwingine ndani ya Biblia aitwaye Yakobo ambaye baadaye alibadilishwa jina na kuitwa Israel.

Huyu ndiye baba wa watoto 12 na ambao hawa watoto ndiyo wanaunda kabila 12 za Israel kwa majina yao wakati huo na mpaka sasa. Hawa (not) in chronological order ni Reuben, Simeoni, Lawi Yusufu, Benjamin, Yuda, Zabuloni, Isikari, Dani, Asheri, Gadi na Naftali.

Ilitokea kuwa mmoja wa watoto wa mzee Yakobo aitwaye Yusufu (Joseph) aliyempenda sana, wakiwa ktk kuchunga ng'ombe, mbuzi na kondoo wa baba yao nyikani, nduguze wa kuzaliwa kwa sababu ya wivu wa kutoona ndugu yao akifanikiwa, waliamua kumuuza kwa wafanyabiashara wa watumwa wa Misri ili kujaribu kuizima nyota yake iliyokuwa inang'aa kuliko za nduguze.

Baada ya Yusufu kuishi miaka mingi Misri akiwa mtumwa, hatimaye kukatokea njaa kubwa duniani kote.

Chakula kilikuwa kinapatikana Misri tu. Watu wote walifunga safari kwenda Misri kununua chakula wakiwemo nduguze Yusufu kutoka nchi ya baba yake, Mzee Yakobo.

Yusufu wakati huo licha ya kuishi katika nchi ya utumwa ya Misri Mungu alimuinua na akatokea kukubalika na Mfalme Farao wa Misri hata akampa cheo cha Uwaziri Mkuu na ndiye aliyehusika na utunzaji wa ghala zote za chakula ktk nchi ya Misri yote.

Ni kweli na hakika kuwa, hakuna Majuto katika kumtumaini na kumtegemea Mungu katika maisha.!

Watoto ya Yakobo walifika nchini Misri kununua chakula mara ya kwanza. Wakapokelewa na ndugu yao Yusufu mwenyewe. Yusufu aliwatambua. Wao walishasahau, hawakuweza kumtambua ndugu yao.

Kilichowashangaza, ni kupewa chakula kwa kadiri walivyohitaji na baadaye wakiwa njiani kurudi nyumbani kwao, waligundua kuwa ndani ya magunia yao fedha yao waliolipa kwa ajili ya chakula hicho, iko imefungwa ndani ya magunia.

Walipofika nyumbani walimsimulia baba yao namna "mtu huyo" (bila kujua kuwa ndiye ndugu yao waliyemuuza) alivyowatendea.

Baadaye chakula kiliisha. Ikawalazimu tena kusafiri kwenda Misri kununua chakula. Safari hii wakakumbana na kikwazo kidogo.

Wakaambiwa, kabla ya kuchukua chakula, sharti warudi kwanza nyumbani wakamlete ndugu yao mdogo aitwaye Benjamin.

Bila kusita, walirudi nyumbani na kumweleza tena baba yao yote waliyoambiwa na "yule mtu". Na wakamwambia kuwa, mtu huyo amemtaka Benjamin (Mdogo wao) kwanza ndipo atakapowapa chakula.

Ndipo Mzee Yakobo alipolia kwa sauti akilalamika kwanini hayo yatokee kwake? Alipoteza mtoto wa kwanza Yusufu, na Benjamini tena akapotee? Mzee hakutaka hili litokee.

Ambacho hakutambua Mzee Yakobo, ni hiki:

Ndani ya matukio yote hayo alikuwemo Mungu mwenyewe akiyaratibu kwa ajili ya kusudi lake maalumu kwa familia yote ya Yakobo na ulimwengu leo kwa ajili ya utukufu wake Mungu mwenyewe.

Sio kusudi langu kusimulia hadithi hii ya kweli ya kihistoria. Lengo langu ni kuwapa ujumbe muhimu CHADEMA, kwamba siyo kila tukio ni adhabu kwenu kwa sababu iwayo yoyote. Matukio mengine yenye sura ya ubaya na kuhuzunisha ni kwa ajili uzuri ujao.

Matukio mengine yaanaachiliwa kwa ajili ya kusudi maalumu la Mungu.

Lilianza la ndugu yetu Tundu A. Lissu kushambuliwa mchana kweupe na Risasi nyingi. Mungu alimlinda, yuko hai mpaka sasa.

Jana alhamisi trh 13/8/2020 ofisi za chama chenu Kanda ya Kaskazini huko Arusha imechomwa moto na watu "wasiojulikana".

Leo ijumaa trh 14/8/2020 msafara wa Tundu Lissu umeshambuliwa Hai Kilimanjaro na watu "wasiojulikana".

Naomba niwape hii tip. Kwamba, haya yanatokea siyo kwa sababu mna dhambi ama mmekosea mahali fulani, HAPANA.

Hampaswi kulalamika. Mtukuzeni Mungu kwa sababu kibinadamu ni mabaya, ni uonevu, unyanyasi lakini ndani yake yumo Mungu - Yehova ili kutimiza kusudi lake jema kwenu na taifa hili zuri la Mungu (Tanzania) na watu wake.

Matendo yao mabaya, ndiyo kukosa kwao. Ndiyo kupotea kwao

Mungu awabariki sana.
 
Naomba niwape hii tip. Kwamba, haya yanatokea siyo kwa sababu mna dhambi ama mmekosea mahali fulani, HAPANA....

Hampaswi kulalamika. Mtukuzeni Mungu kwa sababu kibinadamu ni mabaya, ni uonevu, unyanyasi lakini ndani yake yumo Mungu - Yehova ili kutimiza kusudi lake jema kwenu na taifa hili zuri la Mungu (Tanzania) na watu wake....

Matendo yao mabaya, ndiyo kukosa kwao. Ndiyo kupotea kwao...
 
Naomba niwape hii tip. Kwamba, haya yanatokea siyo kwa sababu mna dhambi ama mmekosea mahali fulani, HAPANA....

Hampaswi kulalamika. Mtukuzeni Mungu kwa sababu kibinadamu ni mabaya, ni uonevu, unyanyasi lakini ndani yake yumo Mungu - Yehova ili kutimiza kusudi lake jema kwenu na taifa hili zuri la Mungu (Tanzania) na watu wake....

Matendo yao mabaya, ndiyo kukosa kwao. Ndiyo kupotea kwao...
Sahihi Mission ya Mungu lazima itimie.
 
Kuna siku nilisema MUNGU anayo kazi na Lissu ambayo bado hajamaliza kupona kwake sio bure
Kwa kupigwa kwake sisi tutakombolewa dhidi ya udhalimu.
Yesu alitaka kuuliwa na herode akafaichwa Misri akarudi kuwakomboa watu,Musa alifichwa kwenye kikapu mtoni ili asiuliwe na farao ili aje awaokoe wana israel.So kusudi la Mungu ni lzm litimie.
Kazi ya shetani ni kuuwa kuharibu na kuvuruga
 
It sound awkward, lakini ndivyo ilivyo. Kwamba iweje ofisi kuchomwa moto iwe ni jambo jema? Iweje msafara wa mgombea Urais Tundu Lissu ushambuliwe mbele ya macho ya polisi liwe jambo jema? Iweje Tundu Lissu ashambuliwe kwa Risasi za kivita za SMG na AK47 iwe ni jambo jema?

Well. Tufutane ili kunielewa.

Mungu aliyetuumba, wakati mwingine huachilia matukio mabaya kutendeka ili ikiwa ni ishara ya kusudi jema la Mungu juu yetu.

Kwa wasomaji wa Biblia naomba warejee hadithi ya Ayubu ktk Biblia. Sio kusudi langu kwenda ndani sana juu ya maisha ya mtu huyu.

Lakini itoshe kusema tu kuwa, ni miongoni mwa watu wachache ktk uumbaji wa Mungu waliopitia nyakati ngumu na za kutisha katika maisha yao.

Katika fikra na mawazo ya wanadamu ni kama vile Mungu alikuwa anamwadhibu Ayubu kwa dhambi zake. Lakini ukweli siyo hivyo. Hali hiyo ya mateso ya Ayubu, iliachiliwa na Mungu mwenyewe ili yeye huyu Mungu kitambo kidogo mbele, apate kujitukuza kupitia shida na mateso ya mtu huyu na kwa hakika ndivyo ilivyokuwa.!

Kwa hiyo, tunaweza kusema hivi. Ndani ya shida na mateso ya Ayubu, alikuwemo Mungu mwenyewe akitenda kazi yake.

Yuko mtu mwingine ndani ya Biblia aitwaye Yakobo ambaye baadaye alibadilishwa jina na kuitwa Israel.

Huyu ndiye baba wa watoto 12 na ambao hawa watoto ndiyo wanaunda kabila 12 za Israel kwa majina yao wakati huo na mpaka sasa. Hawa (not) in chronological order ni Reuben, Simeoni, Lawi Yusufu, Benjamin, Yuda, Zabuloni, Isikari, Dani, Asheri, Gadi na Naftali.

Ilitokea kuwa mmoja wa watoto wa mzee Yakobo aitwaye Yusufu (Joseph) aliyempenda sana, wakiwa ktk kuchunga ng'ombe, mbuzi na kondoo wa baba yao nyikani, nduguze wa kuzaliwa kwa sababu ya wivu wa kutoona ndugu yao akifanikiwa, waliamua kumuuza kwa wafanyabiashara wa watumwa wa Misri ili kujaribu kuizima nyota yake iliyokuwa inang'aa kuliko za nduguze.

Baada ya Yusufu kuishi miaka mingi Misri akiwa mtumwa, hatimaye kukatokea njaa kubwa duniani kote.

Chakula kilikuwa kinapatikana Misri tu. Watu wote walifunga safari kwenda Misri kununua chakula wakiwemo nduguze Yusufu kutoka nchi ya baba yake, Mzee Yakobo.

Yusufu wakati huo licha ya kuishi katika nchi ya utumwa ya Misri Mungu alimuinua na akatokea kukubalika na Mfalme Farao wa Misri hata akampa cheo cha Uwaziri Mkuu na ndiye aliyehusika na utunzaji wa ghala zote za chakula ktk nchi ya Misri yote.

Ni kweli na hakika kuwa, hakuna Majuto katika kumtumaini na kumtegemea Mungu katika maisha.!

Watoto ya Yakobo walifika nchini Misri kununua chakula mara ya kwanza. Wakapokelewa na ndugu yao Yusufu mwenyewe. Yusufu aliwatambua. Wao walishasahau, hawakuweza kumtambua ndugu yao.

Kilichowashangaza, ni kupewa chakula kwa kadiri walivyohitaji na baadaye wakiwa njiani kurudi nyumbani kwao, waligundua kuwa ndani ya magunia yao fedha yao waliolipa kwa ajili ya chakula hicho, iko imefungwa ndani ya magunia.

Walipofika nyumbani walimsimulia baba yao namna "mtu huyo" (bila kujua kuwa ndiye ndugu yao waliyemuuza) alivyowatendea.

Baadaye chakula kiliisha. Ikawalazimu tena kusafiri kwenda Misri kununua chakula. Safari hii wakakumbana na kikwazo kidogo.

Wakaambiwa, kabla ya kuchukua chakula, sharti warudi kwanza nyumbani wakamlete ndugu yao mdogo aitwaye Benjamin.

Bila kusita, walirudi nyumbani na kumweleza tena baba yao yote waliyoambiwa na "yule mtu". Na wakamwambia kuwa, mtu huyo amemtaka Benjamin (Mdogo wao) kwanza ndipo atakapowapa chakula.

Ndipo Mzee Yakobo alipolia kwa sauti akilalamika kwanini hayo yatokee kwake? Alipoteza mtoto wa kwanza Yusufu, na Benjamini tena akapotee? Mzee hakutaka hili litokee.

Ambacho hakutambua Mzee Yakobo, ni hiki:

Ndani ya matukio yote hayo alikuwemo Mungu mwenyewe akiyaratibu kwa ajili ya kusudi lake maalumu kwa familia yote ya Yakobo na ulimwengu leo kwa ajili ya utukufu wake Mungu mwenyewe.

Sio kusudi langu kusimulia hadithi hii ya kweli ya kihistoria. Lengo langu ni kuwapa ujumbe muhimu CHADEMA, kwamba siyo kila tukio ni adhabu kwenu kwa sababu iwayo yoyote. Matukio mengine yenye sura ya ubaya na kuhuzunisha ni kwa ajili uzuri ujao.

Matukio mengine yaanaachiliwa kwa ajili ya kusudi maalumu la Mungu.

Lilianza la ndugu yetu Tundu A. Lissu kushambuliwa mchana kweupe na Risasi nyingi. Mungu alimlinda, yuko hai mpaka sasa.

Jana alhamisi trh 13/8/2020 ofisi za chama chenu Kanda ya Kaskazini huko Arusha imechomwa moto na watu "wasiojulikana".

Leo ijumaa trh 14/8/2020 msafara wa Tundu Lissu umeshambuliwa Hai Kilimanjaro na watu "wasiojulikana".

Naomba niwape hii tip. Kwamba, haya yanatokea siyo kwa sababu mna dhambi ama mmekosea mahali fulani, HAPANA.

Hampaswi kulalamika. Mtukuzeni Mungu kwa sababu kibinadamu ni mabaya, ni uonevu, unyanyasi lakini ndani yake yumo Mungu - Yehova ili kutimiza kusudi lake jema kwenu na taifa hili zuri la Mungu (Tanzania) na watu wake.

Matendo yao mabaya, ndiyo kukosa kwao. Ndiyo kupotea kwao

Mungu awabariki sana.

Wameanza wao kuchoma ofisi na polisi wapo. Inakuja zamu ya ofisi zao kuchomwa na polisi hawakuwa na la kufanya. Mpuuzi hafundiahwi kistaarabu.

Hizi si zama kama zile!!!!!
 
A
Kwa kupigwa kwake sisi tutakombolewa dhidi ya udhalimu.
Yesu alitaka kuuliwa na herode akafaichwa Misri akarudi kuwakomboa watu,Musa alifichwa kwenye kikapu mtoni ili asiuliwe na farao ili aje awaokoe wana israel.So kusudi la Mungu ni lzm litimie.
Kazi ya shetani ni kuuwa kuharibu na kuvuruga
Amina
 
Wale Magaidi Waliofurumushwa Pale Kibiti Na Kukimbilia Mosimboa Da Praia Na Cabo Delgado Wameanza Kutusumbua Kwa kuwashambulia Wapinzani ili ITUHUMIWE SERIKALI YA JPM....

Raia wenzangu TUWENI makini jama...

Mungu Lilinde Taifa Letu Na Mahasidi,Aaaamin Aaaamin.

Nchi Kwanza,
Tanzania Ni Moja.
 
Ni kweli lakini ni Lazima tuwasomee Zaburi na Albadir ili Mungu atume jeshi lake lifanye kazi yake juu ya wale wenye nguvu wanaowatesa watu dhaifu kwa mabavu ya silaha na mabomu ya kodi za wote.

Lakini ni wakati Sasa kwa Mbowe kuachana na Uovu na kutubu ili auone Mkono wa Mungu ukipigania Chama chake.

Mbowe anaonekana ana mambo mabaya anayafanya kwa siri ndio maana muda wote anawaza Konyagi badala ya kujikabidhi kwa Mungu.

Ni Lazima Chadema kabla ya Uchaguzi kiitishe siku ya maombi na Dua na kufunga siku Saba wakishirikisha ACT Wazalendo ili Mungu asimamie haki katika Taifa hili na awatie laana wote wanaokosa shukurani kwa vyeo vikubwa walivyopewa lakini bado wanawadhulumu uhai wa watu wadogo kama akina Ben Saanani na Alfonsi mawazo na kuziacha familia maskini zikiteseka kwa sababu ya wao kusaka Raha ,anasa na Mamlaka na vyeo. Tumuombe Mungu alipe kisasi .
. Kisasi ni juu ya Mungu mwenyewe. Mbowe atambue hilo.
Lisu na wenzake waepuke Maneno wasiyo na uhakika nayo ili Mungu anayejua yote awaadhibu Waovu wanaotaka kulitumbukiza taifa hili katika Chuki kubwa badala ya upendo wao ndio waangamie wenyewe na familia zao zilaaniwe kwa laana kuu.

Chadema watambue kuwa Tanzania ni nchi ya watu wapole na wenye ukarimu ndio maana hata Uhuru tulipata bila kutumia mtutu wa bunduki wala vurugu kubwa.
Hali kadhalika wale wanaotugawa kidini,kikabila ,kikanda na kisiasa za vyama nao watashindwa na haki itatawala na mwenye haki atainuka kuitawala nchi yetu.
 
Project From Belgium At Work...

Zile BARUA walizoandikiwa Serikali Ya Tanzania,iko siku tutajua kilichosukwa nyuma yake.....

John Stielenger,Arvinder Deepel na Yule Mchora Ramani wa kuikwiba Afrika Bwana Johnson McManon Si Watu Wepesi tu kumsapoti Ndg.Yetu Lissu akiwa Belgium......

Something Savage Has Been Orchestrated Exquisitely.....

Mungu Lilinde Taifa Hili Na Kila Mwenye Nia Ovu Ya Kulichoma Moto....Aaaamin.

Mungu Lilinde Taifa Hili na Wawashaji Moto Kutoka NJE,Aaaamin.
 
Back
Top Bottom