Chadema CUF TLP NCCR - LIVE from Urafiki Social Hall

Mwawado:
Kuhamia Malawi si suluhisho, utaendelea kuumia kila siku kwa kuwaona babu/baba/dada zako wakiendelea kuumia chini ya himaya ya CCM na serikali zake. Huko Malawi maisha yako hayatakuwa ya amani hata kidogo.

Washindani wasiwe na papara, inabidi wawe na subira wakati huu hata kama matokeo ya uchaguzi wa leo yatakuwa sio ya kuridhisha. Matokeo haya sio kipimo cha kupendwa kwa watawala hawa, ila yachukuliwe kwamba ujumbe haujawafikia wananchi huko waliko vijijini. Kumbuka kuwa mambo haya yanayosemwa na washindani hayatangazwi kwa mapana na marefu yake na vyombo vya habari vinavyowafikia wananchi. Usichukulie tunavyopata habari humu JF ndivyo ukadhani na wananchi nao habari hizo zinawafikia kiurahisi hivyo. Ni mhimu sana kulitambua hili haraka kabla hata ya viongozi wategemewa kama akina Kitila kuanza kujiuliza na kutoa hisia za kukata tamaa kama zilizotolewa hapo juu.

Njia pekee na ya uhakika kabisa ya kuwafikia wananchi na kuwapelekea ujumbe wa mambo yanavyotokea nchini mwao ni kwa hawa viongozi kuwafikia hao wananchi kwa kila njia inayowezekana kati ya sasa na kabla ya 2010.

Ujumbe wangu ni kwamba, msiwaharakishe wananchi. Wapeni ukweli wa mambo yalivyo, na sababu za wao kutoa uamzi wao wa kutowachagua tena CCM. Sababu hizo sasa zipo nyingi tu, ni namna ya kuzifikisha tu huko zinakotakiwa ndiko bado hakujapatiwa msukumo unaostahili.

Itasikitisha sana kama nafasi hii itawaponyoka tena washindani.

hata matokeo bado unatoa excuse eeh. si mlisema CCM kwisha sasa mnasema ujumbe haujafikia wananchi vijijini.

kwani mliowafundisha kuzomea walikuwa wananchi wa mjini?

nyie endelezeni fitna na kuigawa nchi kwa kumbandika huyu fisadi huyu mkombozi.

sisi tuko karibu na wananchi kutatua shida zao.nyinyi ukaribu wenu na fitna na ubinafsi endeleeni na sambazeni chuki lkn mpanda shari huvuna shari
 
Mtu wa Pwani,
Ndugu yangu hata Mobutu aliyasema hayo, Haile Selassie alidai hayo, Mugame anayasema hayo kwa sababu kama unazoziorodhesha hapa. Lakini kumbuka nguvu ya masikini hata siku moja haitakufa bure...
Kilichowaangusha watawala hawa wote kama utawala wa Roman Empire ni pale ufisadi wao unaposhindwa kubebeka na kuwa mzigo kwa wananchi...
Trust me, soma historia za watu hawa pengine wangeweza tawala milele lakini nguvu ya maskini kama vile nyati alonyakuliwa mwanae na Simba hurudi kwa kishindo!..wakajikusanya wakafanya kisichowezekana..Pamoja na unyama wa kuliwa (Prey) hupata nguvu ya kuwa wao Predator.
Nitarudia kusema hata Hitler alikuwa na wapenzi tena kwa asilimia kubwa ya Wajerumani na kwa muda mrefu sana. Hivi sasa tunafikia ukingoni mwa somo hili na sintaomba yatokee machafu ambayo yataharibu jina la nchi yetu. Ni wakati mzuri kwa watu kama nyie kuwaasa viongozi wenu/wetu kuwa haya yana mwisho na hayana sifa hata kidogo.
Upo karibu na wananchi wasiojua kula yao kesho, maskini ambao kipande cha mkate ni msaada mkubwa kwa shibe ya siku...hawa watu bado hawajafamu kuwa hiyo ni haki yao sio yako na wala sio watawaliwa. Watakuja toa tongo hizo sii muda mrefu na kusema kweli sikubaliani na usemi unaosema safari bado ndefu....kiyama kipo karibu sana, dalili zote zimekwisha jitokeza.
 
mzee Mkandara, hayo ni maneno mazito sana ndugu yangu.. ni wachache wanaelewa somo hilo, na wale wanaofuzu ni wachache zaidi!!
 
WanaJF,

Mimi ni CCM damu damu. Ninaomba kuuliza na kuchangia.

Hizi fedha za Deep green (ita rangi ya chama) mnajuaje zilienda kwenye uchaguzi na zilitumiwa na CCM?

La pili, nikisema kuwa hizi pesa zililiwa na wajanja wachache na wala wana CCM hawajui hilo mtakataa?.

Hivi Karamagi ni mmoja wa wamiliki wa TICS au TISS? nataka kujumlisha 2 na 2 nipate NNE.

Ninachomaanisha ni kuwa tuzipe hizi habari nafasi na sisi tutafakari. Inawezekana kabisa mkurugenzi asielewe fedha zimepelekwa wapi (Tangold Ltd) kwa sababu si mmiliki wa kampuni husika. Hivyo kuwajumlisha wakurugenzi wote wa Tangold Ltd sio HAKI.

Ninawapa changamoto Wapinzani kuacha kusema uongo, huwezi kupata cheque number na tarehe ukashindwa kujua hela zilienda wapi. This is a political stunt, hela zilikoenda mnajua na inajulikana, zilivyotumika ndio tatizo.

Come up wapinzani, sio wananchi wote tunatazama upande mmoja wa sarafu.
 
Mzee FD, ukishasoma hii ripoti natumaini maswali yako ni ya msingi. Ila jaribu kutazama kutoka nje na kufikiri kama habari hii ni kweli ina maana gani? Angalia majina ya wote walioatajwa na wadhamini wa Deep Green na Tangold ni kina nani? na wako wapi?

NImeweka ripoti hii katika pdf hapa chini.
 

Attachments

  • CCMILIVYOCHOTABOT.pdf
    125.6 KB · Views: 124
Ninawapa changamoto Wapinzani kuacha kusema uongo, huwezi kupata cheque number na tarehe ukashindwa kujua hela zilienda wapi. This is a political stunt, hela zilikoenda mnajua na inajulikana, zilivyotumika ndio tatizo.

Come up wapinzani, sio wananchi wote tunatazama upande mmoja wa sarafu.


ukifikiri kidogo utaona kuwa, wapinzani hawakusema "yote" kwani sasa mpira uko upande wa CCM, wakane kuwa hawakuzichota, na wakane kuwa hazikutumika kwenye kampeni... mzee huu siyo mchezo wa draft, hii ni chess!!
 
ukifikiri kidogo utaona kuwa, wapinzani hawakusema "yote" kwani sasa mpira uko upande wa CCM, wakane kuwa hawakuzichota, na wakane kuwa hazikutumika kwenye kampeni... mzee huu siyo mchezo wa draft, hii ni chess!!

Nashawishika kwamba Upinzani una haraka sana, pupa kwa lugha nyingine!!! wangekuwa wanachukua muda kufanya tafiti zao zaidi, wangeweza kufanikiwa malengo yao kwa uhakika na kwa urahisi zaidi!!!

Lakini nadhani hawako hivyo!!!

Wasingekuwa na sababu ya kuacha njiani ati ili CCM wamalizie kiporo kwa kujibu, No, walitakiwa watumie njia hizo hizo wafike mpaka kwenye malipo (vouchers)... siku zote ukiniambia una copy ya cheque, well labda nimesahau kwa kuwa nimelewa,,, lakini cheque, inaonyesha mlipaji na mpokeaji na kiasi gani... full stop haisemi ni hela ya nini!
 
hivi unafikiri unaweza kuhamisha mabilioni ya shilingi na ukayatumia bila kujulikana? Hivi waliposema "wamarekani wanajua mengi" mnafikiri walikuwa na maana gani? Wacha nisije mwaga mtama kwenye "kuku wengi"...
 
Hii kampuni ya uwakili ya IMMMA ni disaster kwa taifa!imeusishwa ni mikataba mingi yenye utata. Lakini naona anayetajwa mara kwa mara ni Ishengoma (i ya mwanzo), kumbe pia kwenye hizo triple m zilizofuatana, mojawapo ni Masha ambaye alikuwa naibu waziri madini na nishati lakini kutona na conflict of interest (kwamba ni director share holdetr wa tanzanite one) ikabidi muungwana amwamishe kule.Hizi syndicate ni muda mwafaka wa kuzianika hadharani wananchi waamue wenyewe sasa

Muhimu kujua haya!
 
Mwanakijiji,

Let me put it this way, kwako wewe na mimi ni rahisi sana kuelewa, kwa Mwingine ni tatizo. Mfano ngoja ni spin hiyo taarifa yao:

"Hawa wapinzani waongo kabisa, hawa lengo lao ni kuleta machafuko hapa nchini, mmenisikia wananchi? wakataeni, wanachekesha kweli eti juzi juzi wanasema hela zimelipwa na BOT kwenda kakampuni flani halafu wana cheque namba na tarehe lakini hawajui hela zilienda wapi au zilitumikaje, jamani huu si uongo jamani?, utapataje cheque na husijue hela zimeenda wapi au zimetumikaje, hawa ni wa kupuuza kabisa, CCM hoyeee! CCM hoyeee!"

Hapo ninawahutubia watanzania walalahoi hawajui hata cheque inaonekanaje, kosa dogo tu la kutomalizia ninaweza kuli CAPITALIZE.
 
Hii ni karne ya 21, wapinzani wa Tanzania bado wapo kwenye karne ya 19. Trust me, this he said, she said politics imekwisha. CCM hawatajibu shutuma hata moja, according to my little knowledge as political analyst, CCM will wait until end of 2008 then they will create zimamoto system( ujenzi wa visima, usawazishaji wa barabara and so on),and this will overturn the whole picture and CCM will win again.

Wapinzani need to change their strategy. You know why? Because CCM will not fight on the media, matokeo yake wananchi watakuwa na upande mmoja wa story ambazo hazijulikani kama ni fact au personal opinions.

what upinzani need to do is, first to show if they have democracy in their marriage. First, call for open election in order toform party structure, set the goals, how will they help Mtanzania, what will be their 2010 strategy, 2015 what will be their strategy, how about education, health care,Economy, how they will they close tax loopholes, how will they minimize small business tax, and many others.

CCM they are about to die, but Upinzani provide CPR for them, trust me they will come back and we will see what happen after 1995 election.
 
Hapo ndipo hawa viongozi wa upinzani wanapokosa mwelekeo, siku ya leo ambayo ni siku ya uchaguzi wa kata 16 za udiwani sehemu mbalimbali za nchi, badala ya wao kuwa huko wapo busy na sera za kutupisha "makombora" it sound they have got their priorities up-side down.

Kesho ikitangazwa CCM imeshinda kata zote wataibuka na kusema ooh tumeibiwa kura! upuuzi kama huu ndio unaowafanya credibility yao kwa wananchi iupungue na ku-resort kwenye sera za kuzomea.

Walianza vizuri kwa kupanga kuachia kata vyama mbalimbali, na wakasema watafanya kampeni ya pamoja kuelekea chaguzi hizi, sasa cha ajabu wakati wote wa kampeni wote wapo Dar busy na kurusha makombora ya mafisadi. Mzee wangu aliwahi kuni hadithia zamani kuwa ukiona mtu ana kukimbiza muda mrefu na mara anaanza kurusha matusi na vitisho basi ujue kishaishiwa pumzi huyo sasa anatapatapa, katika hili nadhani wapinzani ni sawa na huyo mkimbizaji alieishiwa pumzi..

Haya endeleni kusubiri yatakayojiri huko urafiki mimi nasubiri matokea ya chaguzi za Majengo-Songea, Katazi, Kabwe, Namanyere nk.

Majengo alipokwenda Zitto CHADEMA 1 CCM 0. Kule Sombetini napo TLP 1 CCM 0. Tusubiri Kabwe, Namanyere nk.....Hakuna Kulala...
 
kobole kobole, mliojificha tunawaona.

lunyungu tusaidie matokeo mwisho yatakuwa ngapi ngapi?

bwana zitto alianza moja sufuri na sasa yako 1 kwenu na 2 mbili CCm

jee at the end ngapi ? au mshashinda vyote ndio mmeamua kuja furaha kurelax?

au mnapanga kuja kutueleza ufisadi uliotokea kwenye uchaguzi? maana si hasha mkatujia hapa uchaguzi haukuwa fair na free ila tunakusubirini tukusuteni, tena kwa masinzi mwaka huu


MAFISADI WA KUUZA UHURU WA NCHI YETU>

MAFISADI WA KUDUMAZA MAENDELEO YA TAIFA>

BAADA KUKAA NA KUTAFAKARI TUFANYE NN TUSONGE MBELE NYIE DAIMA MNAWAZA NI JINSI GANI KUINGIZA NCHI KWENYE BALAA

Songea CHADEMA 1 CCM O Arusha TLP 1 CCM 0= UPINZANI 2 CCM 0. Huu si ushindi wa menzani, ni kwa kadiri ya kura zilizopigwa jana! chama cha mafisadi?
 
Mwanakijiji,

Let me put it this way, kwako wewe na mimi ni rahisi sana kuelewa, kwa Mwingine ni tatizo. Mfano ngoja ni spin hiyo taarifa yao:

"Hawa wapinzani waongo kabisa, hawa lengo lao ni kuleta machafuko hapa nchini, mmenisikia wananchi? wakataeni, wanachekesha kweli eti juzi juzi wanasema hela zimelipwa na BOT kwenda kakampuni flani halafu wana cheque namba na tarehe lakini hawajui hela zilienda wapi au zilitumikaje, jamani huu si uongo jamani?, utapataje cheque na husijue hela zimeenda wapi au zimetumikaje, hawa ni wa kupuuza kabisa, CCM hoyeee! CCM hoyeee!"

Hapo ninawahutubia watanzania walalahoi hawajui hata cheque inaonekanaje, kosa dogo tu la kutomalizia ninaweza kuli CAPITALIZE.
FD!
Hawa wanajua nini wanafanya kama kweli wana ushahidi kamili wamewekeza kwa wananchi na mahakamani kama watafikishwa.Kama CCM WATAJARIBU KUSPIN KAMA ULIVYOELEZA WEWE HAPO JUU,Wao watapita tena kwa wananchi Tanzania na kila alipopita CCM na kuwaambia ushahidi ni huu na CCM inawadanganya hapo ndiyo Pumba na Mchele utajulikana,Ikija upande wa sheria kama kweli waliotishia kwenda Mahakamani watafanya hivyo (Kitu ambacho siamini watafanya)ndiyo wataibua huo uwezo wote kama wanao ushahidi na kuhitimisha msumari wa ushindi kwa upande wa utetezi.Ninachojua CCM Kwa kuyaangalia haya yote kama wanayajua waliyafanya wataendelea kupoteza muda kwa kuendelea kuelezea bajeti yao kama wanavyofanya sasa na kungojea chaguzi washinde kwa njia wanazozijua wao Kama ilivyozoeleka na kuwaacha upande wa pili ukiendelea na mikutano ya ufisadi na kupata wananchi wengi na kushangiliwa huku wakiwa haiwafaidishi kisiasa kwa minajili ya kupata ridhaa ya kuongoza Nchi.Wanachopaswa kufanya ni kujenga uelewa kwa wananchi juu ya haki zao za msingi kama raia,nini jukumu la serikali yao na majukumu ya viongozi wake ktk kuwaletea maendeleo wananchi na nini mchango wao kama raia ktk kuchangia upatikanaji wa maendeleo hayo bila kusahau kuelezea sera zao na nini watafanya kuhakikisha wanatimiza wajibu wao kwa wananchi endapo watapewa ridhaa ya kuongoza kwa kuwekeza hadi ngazi ya mashina na Kaya, na kama wanaamua kuungana wafanye hivi sasa na kugawana majukumu yatakayoleta muono Chanya kwaajili ya kuleta Mapinduzi ya Kiuchumi na kiutawala kupitia demokrasia.
 
Lunyungu
Pengine huhusiki sana, lakini kuna katatizo kadogo ka kiufundi sehemu fulani kwenye hiyo ripoti. Wanapohitimisha maelezo juu ya kampuni ya Deep Green...(sisiem colour), wanasema katika kipindi cha miezi 4 ziliingizwa shilingi....namba iliyowekwa ni milioni kumi na ushee. Nadhani walimaanisha us dola milioni kumi, au shing za kibongo...bilioni zaidi ya 10.

Invisible na Kitila.

Yes. There is typo. There .815. that has been ommitted in btn figure. Check at the beggining the correct figure has been indicated.

Also August- not presidential nomination, its parliamentarians nominations!

Thanks

JJ
 
Majengo alipokwenda Zitto CHADEMA 1 CCM 0. Kule Sombetini napo TLP 1 CCM 0. Tusubiri Kabwe, Namanyere nk.....Hakuna Kulala...

Mnyika tupeni matokeo yanaendaje huko.achana na hawa mbimbumbu wana wa mafisadi,wapo tayari kushangilia kila jambo la ccm,siye hapa tumewa-ignore na hoja zao za kibepari,usibishane nao wapo kama 5hivi,tujulishe kipi kinaendelea huko?
 
Mtu wa Pwani,

Unachotaka wewe ni kwamba Watanzania wasiambiwe wakati fedha zao zinapotumiwa vibaya na wachache ambao wanajichotea tu watakavyo?

Katika demokrasia, kazi ya upinzani ni 'checks and balances', kusema hiki hakiendi vizuri na hiki kiko sawa. Usiwaone 'wapinzani' kama watu wanaomwaga sumu tu, hapana. Lazima kila Mtanzania aachane na dhana mbaya ya kwamba wako watu 'wanaostahili' kujichotea tu mabilioni ya fedha, bila kuwajibishwa. Hizi ni fedha zetu, lazima kuwe na 'accountability'.

Kama kuna mtu anaona ameonewa, basi, aende mahakamani kushtaki. Taarifa hizi zote zimepatikana kwa Chief Accountant General (CAG), sasa wakamshtaki CAG kwamba amewakashifu?

Mbona waliosema wanakwenda mahakamani sijawasikia?

Waende tu!

Mimi mshenga namjua... naona mwenzangu Mtu wa Pwani bado hujamjua. Pole!



mie nimeshawaambia hawana chao, na weshalijua hilo, hawa kazi yao kumwaga sumu tu, lkn wananchi wa tanzania wako macho sana hadi masaa ya usiku.

na safari hii watajua nani washenga wa mabibi zao
 
Songea CHADEMA 1 CCM O Arusha TLP 1 CCM 0= UPINZANI 2 CCM 0. Huu si ushindi wa menzani, ni kwa kadiri ya kura zilizopigwa jana! chama cha mafisadi?

Mdogo wangu John Mnyika,

Naomba nikusifu kwa propaganda, Hongera sana mkuu,,, maana hizo statistics, ukizisoma kwa kweli Utaona Upinzani Umeshinda saaaana!!! Lakini Ungeweza tu kutulia ukatupatia wakati viti ni 10 hadi 20 at least ungeweza kufanya sisi wengine tulibahatika kusoma kwenye shule za kalimanzira kuwapa Hongera ya Halali Kwenu...

Ni sawa sawa na kipima Joto cha ITV kinachotoa statistics za percentage bila kusema washiriki ni wangapi!!!

Tunaomba usitulazimishe kuamini kwamba Upinzani kwa uwezo wa kufikiri, kuchambua hakuna clear differentiation other than kwamba huko ni Mnyika na kule ni Tambwe,,,, please!!!
 
Back
Top Bottom