CCM Manyara yakutana kumjadili Pauline Gekul, kutoa tamko Novemba 27, 2023

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,034
Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Manyara kimefanya kikao leo Jumapili Novemba 26, 2023 kujadili sakata la Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul anayekabiliwa na tuhuma za ukatili na udhalilishaji, na kesho Novemba 27, 2023 kitatoa tamko lake.

Gekul anatuhumiwa kutoa maelekezo kwa kundi la vijana wake kumwingizia chupa mfanyakazi wake, Hashim Ally au kumpiga risasi kwa madai kwamba alitumwa kimkakati kwenda kwenye hoteli yake ya Paleii Lake View Garden.

Sakata hilo liliibuka baada ya video kusambaa mitandaoni ikimwonyesha Hashim akieleza jinsi alivyofanyiwa ukatili huo na Gekul ambaye hadi jana, alikuwa ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, kabla ya uteuzi wake kutenguliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, jana usiku.

Akizungumzia sakata hilo leo Novemba 26, 2023, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Manyara, Peter Toima amesema wako kwenye vikao kwa ajili ya kujadili suala hilo, akiahidi kesho, atafutwe, atakuwa na maelekezo kamili.

Chanzo Mwananchi

====

Zaidi soma:


Naibu Waziri na Mbunge Pauline Gekul adaiwa kumfanyia Ukatili wa Kimwili Mtoto

Breaking News: - Rais Samia Suluhu atengua uteuzi wa Pauline Gekul saa chache baada ya kutuhumiwa kufanya unyanyasaji

Pauline Gekul ajibu tuhuma za kumdhuru na kumdhalilisha kijana

Pauline Gekul anastahili kuvuliwa uanachama na kufikishwa mahakamani haraka sana. Amekichafua na kukipaka matope chama
 
Kosa la kuunga juhudi ndio hili. Huna mizizi. Ni wa kwao lakini hukutokana na wao. Sasa wakipata pa kukuzika wale waliostahili hiyo nafasi ukapewa wewe kinguvu, hutaamini. Huyu hana hata wajumbe wa mashina nyuma yake yaonekana. Tuendelee kujifunza.
 
Chama cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Manyara kimefanya kikao leo Jumapili Novemba 26, 2023 kujadili sakata la Mbunge wa Babati Mjini, Pauline Gekul anayekabiliwa na tuhuma za ukatili na udhalilishaji, na kesho Novemba 27, 2023 kitatoa tamko lake.

Gekul anatuhumiwa kutoa maelekezo kwa kundi la vijana wake kumwingizia chupa mfanyakazi wake, Hashim Ally au kumpiga risasi kwa madai kwamba alitumwa kimkakati kwenda kwenye hoteli yake ya Paleii Lake View Garden.

Sakata hilo liliibuka baada ya video kusambaa mitandaoni ikimwonyesha Hashim akieleza jinsi alivyofanyiwa ukatili huo na Gekul ambaye hadi jana, alikuwa ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, kabla ya uteuzi wake kutenguliwa na Rais Samia Suluhu Hassan, jana usiku.

Akizungumzia sakata hilo leo Novemba 26, 2023, mwenyekiti wa CCM mkoa wa Manyara, Peter Toima amesema wako kwenye vikao kwa ajili ya kujadili suala hilo, akiahidi kesho, atafutwe, atakuwa na maelekezo kamili.

Chanzo Mwananchi

View: https://www.instagram.com/p/C0HRsRcgGh2/

Hakuna huruma kwa huyu dada yaani kapewa wizara ya Sheria na katiba halafu yeye ndo mvunjaji Sheria mkubwa!,Hastahili hata ubunge Tena muuaji na mpumbavu
 
Kwenye kura za maoni ya ubunge kuna mwanamke mwalimu alishinda, Gekul akapewa na magufuli
Asante kwa uthibitisho huu Sikulijua hili ila kwa kauzoefu kangu kadogo kwenye siasa nilihisi hili. Huyu ana mtihani wa usaliti CDM na ana wa kupinduliwa matokeo ndani ya CCM kumpitisha. Wabunge wa Magufuli wana mtihani, CCM tunaheshimu maamuzi ya vikao vya juu ila mioyoni kama hawakutaki ukapata balaa ndio utajua hujui. Shindeni kwa haki, mtawapenda mnaowaongoza na kujua thamani yao. Huyu anatumia nguvu kubwa kwakuwa nguvu ilimpa nafasi.
 
Back
Top Bottom