Jaji Mfawidhi
JF-Expert Member
- Feb 20, 2016
- 14,047
- 20,411
Jokate ambaye hivi karibuni akiwa amekaribia kufika miaka 40 amebahatika kupata mtoto bila ndoa rasmi, akiwa na mtoto ambaye haonekani kuwa na baba , na ambaye alikuwa msanii wa Muziki na movie maarufu kama Bongo movies, sasa akaingizwa kwenye siasa na kubebwa nafasi za kuteuliwa
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Wanawake UWT, Jokate Mwegelo amewapigia magoti Wananchi wa Mbinga Mkoani Ruvuma ambako ndiko nyumbani kwao akiwashukuru kwa kumlea huku akiwaomba wamuombee na wamuunge mkono Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan na kumpa kura nyingi za Urais mwaka 2025 kwa heshima aliyowapa Mbinga kutokana na kumteua yeye kuwa Katibu Mkuu wa UWT.
“Nimekuja kwa Wazee wangu nyumbani kwa Wazazi wangu mnipe baraka zenu na naamini jinsi nilivyoingia sio kama nitakavyotoka nikitoka moto utawaka, nimekuja kupata baraka zenu lakini naomba niwapigie magoti niwashukuru yaani nawashukuru mno, mniombee mnitie nguvu kazi hii huko nyuma walikuwa wanapewa akina Mama wazitowazito lakini safari hii nimepewa Mimi”“Niko tayari kusumbuliwa na kutumika Mimi ni Mtumishi wenu, tushikamane , tupendane , tuombeane kheri, mmenilea mmenitunza nimerudi kwenye ardhi ya Wazazi wangu”
“Naomba tumuunge mkono Rais Samia kwa heshima aliyotupa Wana Mbinga kuniteua Mimi Mtoto wenu, zawadi pekee ninayoomba na wala msinipatie Mimi hizi zawadi tumpatie Mh. Rais kura za kishindo kutoka Mbinga tukatae Watu wanaokuja kutudanganya nasikia wanapitapita Wazee wangu tusiruhusu hayo mambo”