CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

Nimesoma hotuba zote mbili ila ile ya kwanza inanipa wasi wasi kwani ina makosa madogo madogo ambayo ama yanaonesha kuwa waandisha hawakuwa makini au ni mwendelezo wa yale yale ya CCM. Hotuba ya pili ni nzuri pia ila imeishia hewani. Sikuona hitimisho lenye uzito ule ule kama ilivyoanza kwenye utangulizi.

Nakubaliana nawe kuna typing errors kidogo lazima CCJ iwe tofauti! Pia hotuba ya pili ni nzuri kwa waelewa wa mambo yanavyokwenda nchini lakini kwa akina 'bendera yafuata upepo' kunahitajika ushabiki na vibwagizo vya ziada kuwafanya wasisimkwe na kuiona CCM na Serikali yake ilivyo chai rangi!!
 
Mkandara, Kwanini hadi hivi sasa (kabla ya ujio wa CCJ) vyama vya upinzani havijaweza kuungana na kupata huo ushindi?
Mkuu wangu labda nikwambie kwamba limeisha kata tamaa ya ushindi kwa mwaka huu 2010. Nadhani unakumbuka vizuri kwamba hii kazi ya kuomba au kutaka muungano sikuianza jana na kamasikosei tulikuwa sote kabla ya uchaguzi wa mwaka 2005. Nimeendelea kusema hili hata baada ya uchaguzi kwa malengo ya uchaguzi huu na wala sintabadilisha imani yangu ktk Hili. Chadema,CUF,TLP na NCCR kama vyama vya Upinzani wanatakiwa kuungana ili kupata Ushindi. Na nimesikia wameshindwa kufanya hivyo kutokana na Mapandikizi ya CCM ndani ya vyama hivyo. Haya ni madai ya baadhi viongozi niliowahi kuzungumza nao na tatizo hili limezua makundi ndani ya vyama vyote ikiwa ni pamoja na chama tawala.

Kwa hiyo nimepoteza matumaini yangu toka siku nyingi lakini niliweka mlango wazi kwa tumaini jipya. sasa maadam CCJ wamekuja na wanataka kufanya vitu, basi halahala la kwanza kufanya ni kuunganisha watu. Tukumbuke tu chama ni WATU sio Viongozi wanaokijenga chama... Kupata nguvu na support kubwa ya wafuasi wa vyama vya Upinzani inaanza na hatua hii ya Kuungana. Kunyoosha mikono na kuomba kuungana ni Strategic move ya kisiasa ambayo inakupa wewe sauti kubwa kwa wananchi. Watu watajua malengo yenu sii kutawala ila kuwaondoa wananchi ktk adha waliyopo.. Na Umoja wao ndio pekee utawawezesha Ushindi. Nakumbuka Chadema walijaribu hili lakini nao pia kuna ushindani ndani ya chama, kuna makundi na kwa bahati mbaya zaidi wametengwa zaidi na vyama vingine kwa sababu ya hofu ya hao incumbents.

CCJ haina sababu wala haja ya kuogopa Mapandikizi, ni chama kipya ambacho kinatakiwa kuwa na lengo moja tu..Kuing'oa CCM Madarakani, hizi habari za Itikadi ziwekeni kando kwa sasa. Nguvu yenu iwe KUASI (Upinzani) dhidi ya chama CCM kama ilivyotokea kuundwa kwa CCJ. Hivyo itakuwa rahisi kwenu kuwasoma Mapandikizi wanaoingia kama waasi..Na sii rahisi kwa Mapandikizi kuingia chama kinachopingana na CCM kwa kuasi Uongozi..
Hili neno WAASI litumike kwa faida zaidi badala ya kupiga vita kuitwa hivyo. Na moja ya move kubwa mnayotakiwa kuifanya ni kuwavuta wote wanaotaka KUASI (Upinzani) kujiunga nanyi ili kumshinda CCM.. Amini maneno yangu, mtapata wafuasi red shirts kibao kuliko mnavyofikiria kwani wananchi wamechoka na siasa. Wananchi wanataka kuona chama chenye kufanya kweli na hatua ya kwanza ni kutafuta support ya wananchi mkianza na jumuiya zao. Huko ndiko walikoweka imani zao, na any approach yenye malengo ya kumwondoa CCM itapokelewa kwa nguvu zote isipokuwa kama kuna kiongozi atajaribu kuzuia muungano huu wa Mapinduzi itakuwa amejitenga mwenyewe.

Kwa hiyo mkuu wangu, nachojaribu mimi kufanya ni kutoa ushauri dhidi ya CCM..Nimewahi kusema wazi kwamba JK atapita 2010 kirahisi kutokana na upinzani uliopo lakini sijachoka kupigia debe upinzani na kushauri, inapofikia swala la rais nimependekeza Dr.Slaa kugombea ili kuweka ushindani ktk kiti cha rais. Ushindani ambao utampa mtihani mkubwa kiasi kwamba atumie muda wake mkubwa kutafuta ushindi wake, maadam rais au niseme JK ndiye aliwabeba wabunge wengi mwaka 2005, lengo la mtihani huu ni kutompa nafasi ya kutupiga chenga za Messi.

Mwisho, nimekuwa nikifikiria, kusoma na kuuchosha ubongo wangu kutafuta undani wa kila hatua inayochukuliwa na JK au chama CCM..Kwa mfano kulikuwa na dalili kubwa sna ya wabunge wa CCM waliopo sasa hivi kutorudi mwaka 2010, tena kwa hesabu kubwa lakini maamuzi ya huu uchaguzi wa ndani CCM kupitia wanachama ni mfumo bora kwao kuwaondoshaa viongozi wasiopendwa na wananchi (wasiouzika). Kwa hiyo CCM itaonekana imenza kujisafisha toka ndani (changa la macho) hivyo, kwa hatuua hii wajinga wengi wataipokea na najua haitakuwa ushindani rahisi dhidi ya CCM pasipo nguvu ya umoja wa vyama pinzani..
Bila Umoja nakuhakikishia JK atashinda kwa kishondo tena, na CCM watashinda hakuna cha CCJ, Chadema,CUF,TLP, NCCR wala mjomba wake. niliyasema haya mwaka 2005 na narudia tena kusema hatuwezi kuishinda CCM kwa makundi makundi hali jeshi lake ni kubwa kuliko makundi haya..Tunapoteza muda wetu zaidi kuunda vyama, unless hizi nguvu zote za vyama vya Upinzani ni kutafuta KULA (ruzuku).
 
Mkuu acha mazingaombwe. Mimi ni msomaji mzuri wa posti zako, kuanzia mashairi mpaka uchambuzi. Mtazamo wako wa kisiasa naweza hata kuuandikia wasifu - hili la CCJ ni bango tu la kutimiza uliyoshindwa kuyatimiza kupitia vyama vingine. Hebu jibu maswali haya kama u mwana-CCJ:

1. Wanachama waanzilishi wa CCJ wapo wangapi?
2. Ulipata kadi ya CCJ lini, wapi na ni namba ngapi?

hapa umesema vizuri sana. Na yes najua tumetoka mbali sana!! Na katika maisha kuna progression of thoughts...
 
Kilicho bora kabisa kwa WaTanzania kwa sasa ni CCM. CCJ mtaanzia wapi ili kuubadili mtazamo huu? Zingatieni pia kwamba vyombo vyote vya DOLA ni "mali" ya CCM na Serikali yake. Mliwaona juzi wakuu wa vyombo hivi walivyokuwa wamempamba JK siku ile anahutubia wazee wa Dar. CCJ mtafanyaje kuyabadili haya?

bado mnafikiria in terms of CCM na upinzani.. you need to widen the spectrum of possibilities..
 
Naona wewe na jmushi hamuoni umuhimu wa cross-checking na triangulation. Rejea posti #33 ya Mwanakijiji. Jibu lake linadhihirisha kuwa sio mwanachama mwanzilishi 'absolutely'! Pia tembelea posti zake za zamani kuhusu CJJ. Kisha angalia falsafa zake na uzilinganishe na falsafa mchanyato anazodai kuwa ni za CJJ - tangu lini chama kikawa na mirengo miwili. How can you talk left and walk right or talk right and walk left?

Kwani hilo jibu lilikuwa la swali gani? Au tatizo hapa ni lugha?
 
Hotuba nzuri ikiturejesha tulipotoka, lakini haitupi nafasi ya kujua why CCJ, na wanataka kutupeleka wapi. Picha unayoipata harakaharaka ni kwamba wanataka kuturudisha miaka ya 80, na kabla ya hapo. Nimehesabu kwa haraka haraka CCM inatajwa kwenye hotuba mara nyingi kuliko hiyo CCJ, unajiuliza why this pre-occupation with CCM. Kila mtu sasa anajua kwamba CCM is a crap, why can't you be straight and build your case.
na huyu aliyetoa hotuba ni nani na kwa nini anajificha? Hii siri ya kuwa mysterious ni strategy au woga?

Ni hatua nzuri kwenda kwa wananchi. Lakini lazima nisema kwamba kuanzisha chama na kukisimamisha is a tough business. Cope walifanya kosa hilohilo. Walikuja wakadhani kwamba wapinzani wote waliokuwepo walikuwa hawana maana, na wao ndio walikuwa wakombozi kwa kuwa walikuwa uzao wa ANC. Wakakataa ushirikiano wowote na wenzao waliokuwepo. Matokeo walianguka vibaya, wakishindwa hata na chama cha makaburu!! Karibu kwenye uwanja wa upinzani.
 
Hotuba nzuri ikiturejesha tulipotoka, lakini haitupi nafasi ya kujua why CCJ, na wanataka kutupeleka wapi. Picha unayoipata harakaharaka ni kwamba wanataka kuturudisha miaka ya 80, na kabla ya hapo. Nimehesabu kwa haraka haraka CCM inatajwa kwenye hotuba mara nyingi kuliko hiyo CCJ, unajiuliza why this pre-occupation with CCM. Kila mtu sasa anajua kwamba CCM is a crap, why can't you be straight and build your case.
na huyu aliyetoa hotuba ni nani na kwa nini anajificha? Hii siri ya kuwa mysterious ni strategy au woga?

Ni hatua nzuri kwenda kwa wananchi. Lakini lazima nisema kwamba kuanzisha chama na kukisimamisha is a tough business. Cope walifanya kosa hilohilo. Walikuja wakadhani kwamba wapinzani wote waliokuwepo walikuwa hawana maana, na wao ndio walikuwa wakombozi kwa kuwa walikuwa uzao wa ANC. Wakakataa ushirikiano wowote na wenzao waliokuwepo. Matokeo walianguka vibaya, wakishindwa hata na chama cha makaburu!! Karibu kwenye uwanja wa upinzani.

unajua mojawapo ya vitu ambavyo vinafanya siasa za Tanzania kuwa na raha ya pekee ni kuwa Watanzania sijui ni kutokana na malezi yetu au na vitu vingine tunaendesha siasa zetu tofauti kweli. Hata kitabu kinachotumika nchi nyingine hakiwezi kutumika Tanzania.
 
utaweza kujiunga hata ukiwa nje ya nchi; tayari hadi hivi sasa wameweza kujiunga kuanzia Japan, South Africa, Uingereza na US yenyewe.. lakini kwa sababu sasa hivi ni zaidi katika uanzilishi basi kujiunga kwa kwanza kabisa siyo kadi bali ni itikadi! Hivyo utaona uanachama wa CCJ utakuwa ni tofauti sana na uanachama wa vyama vingine vyote Tanzania, hautategemea kadi bali zaidi itikadi. Huu ndio mtindo uliopo kwenye nchi nyingi za kidemokrasia. Watu wanaposema mimi ni Republican au Democrat haina maana ana kadi rasmi ya chama bali anakubaliana na itikadi za vyama hivyo.

So, endapo baada ya kuona kuwa CCJ inaakisi fikra na mtazamo wako wa kisiasa, consider yourself a member; ni pale tu inapokuja sasa katika kuwezesha CCJ na kutafuta nafasi za uongozi ndipo uanachama wa kadi na wa kuunga mkono unapojitokeza.

Basi najichukulia kuwa mimi ni mwanachama wa CCJ, nikiangalia mwenendo wake; uanachama wangu unawea kufutika wakati wowote.
 
Mbona ni jambo la kwaida kwa watu kuhama vyama,hata keshokutwa waloko CCJ watahama kwenda vyama vingine...hata kwenye dini watu huhama kila leo,sembuze vyama vya siasa...hata Mawaziri wa Kikwete huhamishwa toka Wizara moja kwenda nyingine,sembuse wanachama wa chama cha siasa..Halafu ukija kukagua hao watu wanaohamahama toka chama kimoja kwenda vingine wengi wao huwa ni vimeo,Believe me..We furahia hivyo vimeo..Ha ha ha!Watu credible huwa hawahami vyama,teh teh teh..Kila shemu kuna matatizo hakuna mahali mabko kuko purely salama,matatizo hayakimbiwi,ukiona mtu anakimbia ujue yeye ndio tatizo..Ni mtazamo tu!
 
Mbona ni jambo la kwaida kwa watu kuhama vyama,hata keshokutwa waloko CCJ watahama kwenda vyama vingine...hata kwenye dini watu huhama kila leo,sembuze vyama vya siasa...hata Mawaziri wa Kikwete huhamishwa toka Wizara moja kwenda nyingine,sembuse wanachama wa chama cha siasa..Halafu ukija kukagua hao watu wanaohamahama toka chama kimoja kwenda vingine wengi wao huwa ni vimeo,Believe me..We furahia hivyo vimeo..Ha ha ha!Watu credible huwa hawahami vyama,teh teh teh..Kila shemu kuna matatizo hakuna mahali mabko kuko purely salama,matatizo hayakimbiwi,ukiona mtu anakimbia ujue yeye ndio tatizo..Ni mtazamo tu!

Umefikiria sana hapa! Halafu hujaeleweka
 
kaazi kwelikweli, hofu kubwa kwa wananchi wenye upeo ni kwa nini mpaka sasa hao big fish wanashindwa kujiytokeza hadharani, wanachopima ni nini? mimi wanannipa shaka sana viongozi hao kama kweli wataweza kuiendesha hii nchi wakati hata confidence ya kujitokeza adharani ni mpaka wapimie kwnza
 
Too emotional brother "sentamental"!
And the problem of this is you react instead of responding

Acha upuuzi,wengine wapuuzi hamfatilii mjadala inavyotakiwa,mnarukia rukia tu issue,go ef n c where it cums from quit being a moron....eti emotional,kama unataka hoja kwa hoja nieleze where exactly you can justify yur crap.
 
Acha upuuzi,wengine wapuuzi hamfatilii mjadala inavyotakiwa,mnarukia rukia tu issue,go ef n c where it cums from quit being a moron....eti emotional,kama unataka hoja kwa hoja nieleze where exactly you can justify yur crap.

Nyamaza wewe
 
Mbona ni jambo la kwaida kwa watu kuhama vyama,hata keshokutwa waloko CCJ watahama kwenda vyama vingine...hata kwenye dini watu huhama kila leo,sembuze vyama vya siasa...hata Mawaziri wa Kikwete huhamishwa toka Wizara moja kwenda nyingine,sembuse wanachama wa chama cha siasa..Halafu ukija kukagua hao watu wanaohamahama toka chama kimoja kwenda vingine wengi wao huwa ni vimeo,Believe me..We furahia hivyo vimeo..Ha ha ha! Watu credible huwa hawahami vyama,teh teh teh..Kila shemu kuna matatizo hakuna mahali mabko kuko purely salama,matatizo hayakimbiwi,ukiona mtu anakimbia ujue yeye ndio tatizo..Ni mtazamo tu!

Credibility ya mtu hupimwa na nini?

Kama kuna watu wanaendelea kubaki kwenye chama kilichogubikwa na kashfa, rushwa, na kila aina ya uozo, sidhani kama hao wana sifa ya kuitwa CREDIBLE, bali ni OPPORTUNISTS.
 
Back
Top Bottom