Companero,
Mkuu hata sijakuelewa kabisa..Ila nitatumia lugha rahisi zaidi kwa wote ili kila mtu anielewe pasipo kutumia dictionary sijui ya nani..
Navyojua mimi hakuna Maamuzi yoyote yasiyokuwa na goals zake iwe ni kutafuta Uhuru toka kwa mkoloni, kumwondoa mtawala raia ambaye ni dikteta na hata kuondoa chama au mfumo wa utawala uliopo.. Hizi zote zitatafsirika kutegemeana na MAZINGIRA yaliyopo wakati mhusika anazungumza. Hivyo ni goals zilizowekwa ndizo huzaa ideology, hata kama iwe Revolutionary in Political ndio foundation bado yale malengo ndiyo yatakayozaa ideology in practice.
Kwa hiyo nachoweza mimi kujiuliza leo ni yapi yalikuwa malengo ya kudai UHURU wetu (GOALS) pasipo kujali posiotion ya waasisi wetu wakati wakigombea Uhuru huo..Bila shaka tulipokuwa tukigombea Uhuru wakoloni walikuwa wakikataa changes kwa sababu wao ni watawala.. bila shaka walikataa changes zozote(conservative) na kina Nyerere wakaitwa Revolutionary...
Lakini baada ya sisi kuchukua Uhuru wetu we stand ktk position tofauti kabisa..a step forward hatupo tena pale pa kutawaliwa. Na hapo a revolutinary anaweza kupinga mabadiliko yoyote ya goals zilizowekwa as founding principals za Mapinduzi yao. Tunajikuta wengine tukiwa katika position kama ya yule mkoloni kukataa changes zozote goals zetu tulizoweka wakati tunautafuta Uhuru bila kujali kama wao huko nyuma walikuwa na mitihani wa revolutionary, reformist au Conservative.
Mkuu kumbuka maneno yangu siku zote kuwa WATU na MAZINGIRA mliyopo that's what count. Marekani walipokuwa wakipigania Uhuru, Waingereza walowezi walikuwepo Conservative, Reformist na pengine wengine Revolutionary chini ya utawala wa Malkia. Lakini Yankees na kina Abraham Lincorn walikuwa Revolutionary period. Baada ya Uhuru, madaraka kuwa mikononi mwa wananchi wenyewe everything changed.. now it's about themselves (Political revolutionaries) kuwa aidha Republican hao kina Abraham waliokuwa revolutionary, wengine kuibukia Demokratic, Fascist, Nationalist, Communist, na mengineyo mengi tu kwa kutazama mfumo wa Utawala ulotokana na Mapinduzi yale..
Kwa hiyo mimi, maadam ni Republican jukumu langu ni kulinda na kutunza goals zilizowekwa na waasisi wangu TANU in practice as a Conservative..Ni kweli sikubaliani na changes zozote zinazohusu kurudisha Ukabila, Udini, Kupotea kwa Lugha ya Kiswahili, Wageni kuja kuiba rasilimali zetu, Unyonyaji, Ukabaila, Ubwanyenye, kuuzwa ardhi, wazawa kuwa second class citizen, kuwa brain washed na corrupted..Hizi ni baadhi tu ya vitu ambavyo siku zote sintakubaliana navyo kisiasa...na kiuchumi siku zote nitaheshimu haki ya kila mtu kuendesha maisha yake kiuchumi kama navyotaka Uhuru wa taifa langu kuheshimika - Political freedom, social freedom, economic freedom = Total freedom.