ninafurahi kwamba mgawanyo tunaoutaka ndio unaendelea kuwepo. Wale wanaoamini chadema, cuf au vyama vya upinzani vilivyopo ndiyo vinawakilisha matamanio yao na njozi zao wana haki kabisa ya kuendelea kuwemo humo na kuviimarisha; wale wanaoamini kuwa ccm ndiyo suluhisho la matatizo ya watanzania na kuwa ndio chama pekee chenye uwezo wa kutuletea maendeleo nao wana haki ya kuendelea kuunga mkono na kujiunga nacho. Lakini si haki kujaribu kuwataka watu wote wajiunge na upinzani wa zamani au chama tawala ati kwa sababu chama kipya hakieleweki, hakijulikani n.k n.k hakuna ratiba ya kuundwa chama ili kikubalike; hakuna masharti ya chama kiwe kimeundwa kwa muda gani ili kiwe kinavutia watu; chama ni itikadi na muundo. Hadi hivi sasa hakuna chama kwenye upinzani huu zamani chenye itikadi ya ccj, period. Sasa kutaka watu wa ccj au mashabiki wake kujiunga na vyama vya upinzani wa zamani ili mradi tu wasiwe na chama chao ni kujaribu kuweka mawazo huru ya watu kwenye chupa moja ya upinzani.
Naomba nipendekeze; wale mnaoamini chadema, cuf au vyama vya upinzani vya zamani kuwa ndio uchaguzi wenu endeleeni tu kwani ni sehemu ya demokrasia. Kama watu hamkubaliani kiitikadi, mtazamo au mapendekezo yenu ya kitaifa hamuwezi kuungana. Sielewi kwanini ccj wanatakiwa kujiunga na vyama vingine wakati hawakubaliani navyo kiitikadi, mtazamo au malengo! Hatuwezi kujiunga na vyama vingine ili "kuiondoa ccm madarakani"; muungano wa namna hiyo ni muungano dhaifu kwani unaundwa katika lengo la udhaifu. Huweji kuwa na lengo la kuondoa ccm madarakani kama msingi wa muungano!
Wale walioridhika na ccm waendelee hivyo hivyo na wale ambao tunataka kuleta pendekezo jipya kwa wapiga kura na watanzania, pendekezo lenye misingi ya historia yetu kama taifa basi tutafanya hivyo. Yawezekana tusifanye vizuri kama tunavyotaka kwenye uchaguzi huu lakini tunachotaka ni kuwa na sisi wenye mawazo tofauti na yale ya ccm au upinzani uliopo sasa tuwe na nafasi katika siasa za nchi yetu? je hili linawatisha sana hadi mtushauri tujiunga na watu ambao hatukubaliani nao kiitikadi, mfumo, mtazamo au usuluhishi wa matatizo ya kitaifa? Tuungane nao ili nani afurahi?
hii nimeipenda yup