CCJ kuanza Charm offensive! - Ask your questions!

ninafurahi kwamba mgawanyo tunaoutaka ndio unaendelea kuwepo. Wale wanaoamini chadema, cuf au vyama vya upinzani vilivyopo ndiyo vinawakilisha matamanio yao na njozi zao wana haki kabisa ya kuendelea kuwemo humo na kuviimarisha; wale wanaoamini kuwa ccm ndiyo suluhisho la matatizo ya watanzania na kuwa ndio chama pekee chenye uwezo wa kutuletea maendeleo nao wana haki ya kuendelea kuunga mkono na kujiunga nacho. Lakini si haki kujaribu kuwataka watu wote wajiunge na upinzani wa zamani au chama tawala ati kwa sababu chama kipya hakieleweki, hakijulikani n.k n.k hakuna ratiba ya kuundwa chama ili kikubalike; hakuna masharti ya chama kiwe kimeundwa kwa muda gani ili kiwe kinavutia watu; chama ni itikadi na muundo. Hadi hivi sasa hakuna chama kwenye upinzani huu zamani chenye itikadi ya ccj, period. Sasa kutaka watu wa ccj au mashabiki wake kujiunga na vyama vya upinzani wa zamani ili mradi tu wasiwe na chama chao ni kujaribu kuweka mawazo huru ya watu kwenye chupa moja ya upinzani.

Naomba nipendekeze; wale mnaoamini chadema, cuf au vyama vya upinzani vya zamani kuwa ndio uchaguzi wenu endeleeni tu kwani ni sehemu ya demokrasia. Kama watu hamkubaliani kiitikadi, mtazamo au mapendekezo yenu ya kitaifa hamuwezi kuungana. Sielewi kwanini ccj wanatakiwa kujiunga na vyama vingine wakati hawakubaliani navyo kiitikadi, mtazamo au malengo! Hatuwezi kujiunga na vyama vingine ili "kuiondoa ccm madarakani"; muungano wa namna hiyo ni muungano dhaifu kwani unaundwa katika lengo la udhaifu. Huweji kuwa na lengo la kuondoa ccm madarakani kama msingi wa muungano!

Wale walioridhika na ccm waendelee hivyo hivyo na wale ambao tunataka kuleta pendekezo jipya kwa wapiga kura na watanzania, pendekezo lenye misingi ya historia yetu kama taifa basi tutafanya hivyo. Yawezekana tusifanye vizuri kama tunavyotaka kwenye uchaguzi huu lakini tunachotaka ni kuwa na sisi wenye mawazo tofauti na yale ya ccm au upinzani uliopo sasa tuwe na nafasi katika siasa za nchi yetu? je hili linawatisha sana hadi mtushauri tujiunga na watu ambao hatukubaliani nao kiitikadi, mfumo, mtazamo au usuluhishi wa matatizo ya kitaifa? Tuungane nao ili nani afurahi?

hii nimeipenda yup
 
Felister,
Mkuu wangu hata sijakufahamu kabisa unachozungumza. Kwanza hakuna mtu aliyedharau mtu isipokuwa tunazungumzia chombo hiki cha CCj.. Ni swala jingine kabisa kusema Mwanakijiji hawezi kitu pasipo kujua mapana ya Mwanakijiji, tofauti na kuznugmzia chombo cha usafiri ambacho lengo lake ni kuwachukua Watanzania wote na sio wanachama wake kufika ktk promise land. Na hata huo mfano unazungumzia huyo Mtume alisema yeye peke yake akiwa na maana kuwa ndiye pekee Muumini wa Mwenyezi Mungu na haikuwa na maana hapakuwepo na watu wengine wenye uwezo. Ni swala la kiimani zaidi ya uwezo na nguvu zake.

Ni muhimu sana swala hili tusilichukulie Unazi au ushabiki kwa sababu tunazungumzia Mustakabali wa nchi nzima na raia wake. Hili sio swala la wanaCCJ na waumini wake against the rest.. hatupiganii nani ataingia peponi kabla ya mwenzake ila swala zima linatuhusu sote inapofikia nani awe kiongozi wetu na chombo gani tukitumie. Sasa mkianza kufikiria kuna akina HAO against SISI wenye elimu na uwezo, ndipo mnapoweza kupoteza kabisa maana ya usajili wenu. CCJ ni chama kinachotakiwa kuwa wazi hakuna sababu kabisa ya kujificha ficha viongozi kisha mnatwambia kama hatuwezi tuwaachie wanaoweza hao wamejificha..

Mzee Mwanakijiji,
Unaposema CCJ sio chama kilichanzishwa na wana CCM hapa mkuu utakuwa unatufunga kamba tu ama kujilaghai mwenyewe. Huwezi kutumia majina ya watu waliopo leo hii kushindana na CCM ktk nchi hii. Ukweli huu lazima mmuukubali. Hayo majina ya kina Mpendazoe mtashindwa vibaya sana kwa sababu Nitarudia tena Watanzania tu Wajinga na Malimbukeni. Itachukua zaidi ya majina haya kuwapeni hata nafasi ya kushinda majimbo na laukama nia yenu ni nzuri basi bila shaka mtakubaliana nami kwamba ipo kila haja ya kukusanya nguvu zetu wote wanaopenda mabadiliko kupambana na utawala wa CCM..To me tatizo sio Kikwete, na fact zipo kwamba kafanya mengi mazuri (policies) kuliko mabaya isipokuwa kashindwa kusimamia utawala wake...Kosa moja kubwa la JK - he is a WEAK president.. Hili kosa moja tu linaondoshaa kabisa sifa zake zote za kushika ajira yake...
 
mzee mwanakijiji,
mkuu wangu mawazo yako ni ya kibinafsi.. Yaani unaonyesha wazi kwamba unachoamini wewe hata kama ni kinyume basi sawa tu hali wakati huo huo unatumainia ushindi pasipo kuunganisha nguvu... Hii haiingii akilini hata kidogo. Maelezo yako kwa ujumla hayana tofauti na ile hotuba ya jk alipowaambia wafanyakazi kwamba - haitaji kura zao.. Jambo ambalo limetupa picha kwamba jk anafikiri anaweza kushinda pasipo kura za wafanyakazi. Fikra hizi tu zinaweza kumgharimu sana kinyume na matajario yake.

Mkuu mara zote kauli ya mtu ndio humfunga ktk matendo yake, hivyo unaposema ccj hawana sababu ya kuungana na vyama vingine kwa sababu za kiitikadi, malengo na kadhalika inanipa wasiwasi mkubwa zaidi kwa sababu nimeisoma katiba ya ccj na hakuna jipya.. Ccj imeundwa kutokana na matokeo ya uongozi mbovu aambao wote hawa wameutumikia kwa zaidi ya miaka 26 muda mrefu zaidi ya utawala mzima wa nyerere. Hawa watu walikuwa viongozi ngazi za juu kwa miaka yote 26 wasione sababu ama umuhimu wa upinzani kwamiaka yote 26 ila tu baada ya kuingia jk ndipo tunawaona wakisimama.
Kifupi hawa naweza kuwaita ni wana mapinduzi, ccj ni chama kinachotaka kupindua ccm kwa amani lakini ni kizazi kile kile kilichotufikisha hapa tulipo leo. Mabaya yote wanayoyaona leo ccm ni mabaya ambayo vyamavingine vimeyaona miaka zaidi ya 15 iliyopita wakati wao hawaoni makosa haya. Leo ujio wao uyaone makosa yote ya upinzani kisha basi badala ya wao kuyarekeebisha ili ushindi upatikane wanachukua jukumu hilo wao wenyewe kwa matumaini kwamba sisi wananchi tutawaamini kwa sababu tu wanatumia jina la mwalimu nyerere.

Hapana mkuu wangu... Ccj wakiwa viongozi ndani ya ccm wamepiga kura nyingi sana dhidi ya miradi ambayo imetuingiza ktk hasara. Walikuwa moja ya sababu kubwa ya bunge letu kupitisha sheria ambazo zimetufikisha hapa. Walikuwa wajumbe wa mkutano ulopitisha azimio la zanzibar na kuliua azimio la arusha hali wakidai azimio hilo halikufa. Na wakayapokea mafisadi ndani ya chama wakijua fika kwamba chama kinapoteza mrengol lakini hawakutoka. Sasa iweje leo hawa watu waje hapa kutuhakikishia ushindi hali wakijitenga na kutohitaji nguvu ya wanamapinduzi wengine waliowatangulia.

Mkuu wangu nimekwambia wazi kabisa kwamba hata zimbabwe ambao walikuwa na uhasama mkubwa wa kikabila na chuki ya jadi. Iliwachukua kuungana kwa nguvu zao kuweza kumshinda kaburu ian smith. Huko south pamojana upinzani mkubwa wa kiitikadi baina ya anc na pac walikuja unganisha nguvu zao kumlazimisha kaburu kuachana na apartheid. Uhuru wa msumbiji na kadhalika, hizi zote ndizo hekima za mwalimu nyerere alizotuonyesha ama kutuachia kwamba ni lazima tuondoe tofauti zetu tunapomkabiri adui mmoja. Maswala mengine ya kiitikadi yatafuata baada ya ushindi na kubomoa nguzo au kuta za berlin (katiba, sheria na taratibu za kiutawala).

Kinyume cha kufanya hivyo ni kukataa wazi hekima za mwalimu lakini bado mkitumia jina lake kwa faida yenu..ikiwa ushindi ni lazima basi shurti mkubali ukweli kwamba umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu.. Mkikataa haya binafsi sioni sababu kabisa ya chama hiki ccj kutumia jina la mwalimu hali msingi mkubwa wa itikadi yoyote ni kuwaunganisha watu dhidi ya utawala dhalimu.

kwani cjj ina nini mpaka ulazimishe iungane na upinzani mwingine? Mbona cuf,chadema,nccr,tlp, ...n.k hujaomba viungane kwa nini usiaze na hivyo.?pili kama wanaona itikadi tofauti kwa nini waungane? Kwani shwala ni kutoa ccm tu au kuna zaidi ya hili ambalo ndio inatofautisha vyama?
 
Kwa kweli mwanakijiji kwangu mimi umekiwakilisha vyema cjj ktk mjadara huu
 
Felister,
Mkuu wangu hata sijakufahamu kabisa unachozungumza. Kwanza hakuna mtu aliyedharau mtu isipokuwa tunazungumzia chombo hiki cha CCj.. Ni swala jingine kabisa kusema Mwanakijiji hawezi kitu pasipo kujua mapana ya Mwanakijiji, tofauti na kuznugmzia chombo cha usafiri ambacho lengo lake ni kuwachukua Watanzania wote na sio wanachama wake kufika ktk promise land. Na hata huo mfano unazungumzia huyo Mtume alisema yeye peke yake akiwa na maana kuwa ndiye pekee Muumini wa Mwenyezi Mungu na haikuwa na maana hapakuwepo na watu wengine wenye uwezo. Ni swala la kiimani zaidi ya uwezo na nguvu zake.

Ni muhimu sana swala hili tusilichukulie Unazi au ushabiki kwa sababu tunazungumzia Mustakabali wa nchi nzima na raia wake. Hili sio swala la wanaCCJ na waumini wake against the rest.. hatupiganii nani ataingia peponi kabla ya mwenzake ila swala zima linatuhusu sote inapofikia nani awe kiongozi wetu na chombo gani tukitumie. Sasa mkianza kufikiria kuna akina HAO against SISI wenye elimu na uwezo, ndipo mnapoweza kupoteza kabisa maana ya usajili wenu. CCJ ni chama kinachotakiwa kuwa wazi hakuna sababu kabisa ya kujificha ficha viongozi kisha mnatwambia kama hatuwezi tuwaachie wanaoweza hao wamejificha..

Mzee Mwanakijiji,
Unaposema CCJ sio chama kilichanzishwa na wana CCM hapa mkuu utakuwa unatufunga kamba tu ama kujilaghai mwenyewe. Huwezi kutumia majina ya watu waliopo leo hii kushindana na CCM ktk nchi hii. Ukweli huu lazima mmuukubali. Hayo majina ya kina Mpendazoe mtashindwa vibaya sana kwa sababu Nitarudia tena Watanzania tu Wajinga na Malimbukeni. Itachukua zaidi ya majina haya kuwapeni hata nafasi ya kushinda majimbo na laukama nia yenu ni nzuri basi bila shaka mtakubaliana nami kwamba ipo kila haja ya kukusanya nguvu zetu wote wanaopenda mabadiliko kupambana na utawala wa CCM..To me tatizo sio Kikwete, na fact zipo kwamba kafanya mengi mazuri (policies) kuliko mabaya isipokuwa kashindwa kusimamia utawala wake...Kosa moja kubwa la JK - he is a WEAK president.. Hili kosa moja tu linaondoshaa kabisa sifa zake zote za kushika ajira yake...

Mkandara, kwanini CCJ iungane na vyama vingine? Na ni chama gani ambacho kinafaa CCJ kuungana nacho na kwanini?
 
Mkandara, kwanini CCJ iungane na vyama vingine? Na ni chama gani ambacho kinafaa CCJ kuungana nacho na kwanini?
Thank You!
Nimependa sana mwanzo huu wa kufahamishana badala ya kubishana. Kwanza kabla sijajibu swali lako naomba kusema machache kuhusiana na tumaini jipya la wananchi. Kama nilivyokwisha sema hapo awali Ni muhimu sana kuzingatia vitu viwili WATU na MAZINGIRA ktk kila ubunifu wa suluhisho la la kutatua matatizo yaliyopo. Kwa maelezo yako CCJ imekuja na Itikadi mpya mabyo wao wanaiona inafaa na pinzani ya chama kilichopo madarakani.
Yawezekana uko right kabisa lakini sivyo wananchi wanachoamini. WATU yaani sisi wananchi tunajua kwa uhakika kwamba UONGOZI bora ndio tatizo kubwa la maendeleo yetu. NI kutokana na Uongozi uliopo ndio wamebadilisha dira ya Taifa. Dira ambayo baba wa taifa na waasisi wa chama walituahidi kufika hiyo nchi ya Kufikirika. Uongozi mbaya umeshindwa kufuata Itikadi au wanaweza kuibadilisha.

Sasa maadam fikra za wananchi wengi ni kuwepo kwa viongozi wabaya, viongozi ambao walibadilisha mengi ikiwa ni pamoja na miiko na maadili ya uongozi kwa faida yao wenyewe ndio walioharibu Itikadi nzima ya chama CCM... Na kama unakumbuka JK alipoingia madakani hata yeye na Lowassa walisema kwamba wamerithi mapungufu mengi toka Utawala wa Mkapa na Mkapa kwa Mwinyi ili mradi kila mmoja wao kuepa ukweli kwamba jukumu ni lao kuyaondoa matatizo waliyorithi. Hivyo, watu hawa wapiga kura wanachojua ni kwamba Uongozi wa CCM ni mbaya..Na chama ni watu.

Pili, Katika mazingira tulokuwa nayo leo haiwezekani kupata mapinduzi ya kweli kwa kutumia siasa za miundo ya Kiitikadi. wananchi wapiga kura hawajui kabisa hizi habari za Itikadi kwa sababu ya njaa kali. Akili zao zimefungwa kwa njaa na umaskini hivyo kutengeneza mazingira magumu sana kisiasa hasa kwa vyama vya Upinzani..Katiba na taratibu zote za uchaguzi ni mbaya kiasi kwamba mwanya uliopo ni mdogo sana kwa vyama vingi kuweza kupata Ushindi..

Mkuu wangu wananchi hatutajali kama ni CCJ iliyounganisha nguvu zake na Chadema au CUF..Ujumbe huu ni kwa vyama vyote vya Upinzani kutengeneza mazingira ya ushindi bila kutumia porojo za siasa isipokuwa kutengeneza mazingira ya kisayansi. Na hakuna uwezekano wowote kwa vyama hivi kushinda pasipo kuunganisha nguvu zao. CCJ mkiwa wa kwanza kunyoosha mkono, sii vibaya hata kama Itikadi yenu kisiasa ina tofauti kubwa na wengineo. Mkuu majuzi tu Conservative ya Uingereza imeungana na Demokratic (The far left) kumwangusha Labour (kati kushoto). Hivi vyama vinapingana kiitikadi kuliko Conservatives na labour lakini kwa sababu walitaka kumwondoa Gordon Brown, na wakajua mazingira yanayoweza kuleta mgawanyo wa kura, wakatazama uwezekano wa kisayansi kulingana na mazingira yao ndipo walipoitisha uchaguzi kabla ya kusubiri miaka miwili ijayo, Upepo unaweza kugeuka.

Sisi hapa TZ hatuna maswala ya mseto. JK akishinda uchaguzi he takes all hata kama Bunge mtagawana na CCM. Kwa hali yoyote ile najua fika wabunge wengi wa CCM hawatarudi 2010, lakini CCM sio wajinga hivyo, nao wamejiandaa kuwaondoa wale wasio uzika mapema kwa kuweka kura za wanachama wao. Hivyo Wabunge wasioweza kurudi watachujwa mapema ktk uchaguzi wa mwanzo na ukitazama huko Mikoani CCM bado ndio jina kubwa. Ukimuondoa mtu wasiyempenda ukamweka mwingine tayari CCM itaanzisha Uhai mpya na ushindani utakuwa baina yenu na huyu CCM mpya anayependwa na wanachama mikoani. Kwa Tanzania na mazingira yake ni kazi kubwa kuishinda CCM kama mapungufu sio ya mgombea.

Kwa hiyo mkuu wangu swala kubwa la wananchi...ni kuwaondoa CCM madarakani. haihusiani kabisa na Itikadi, malengo wala katiba yao.. Asilimia 80 ya Watanzania hawajali hizi siasa za Itikadi ikiwa tatizo kubwa nchini ni utekelezaji. Na kazi kubwa ya vyama vya Upinzani inatakiwa kujihusisha zaidi na kubuni mbinu za kuuondoa Uongozi uliopo (CCM) na sio kuvumbua Itikadi mpya ambazo haziwezi kufanya kazi hadi siku wameshika madaraka. Na kibaya zaidi tupo ktk taifa la Wajinga na Malimbukeni wenye njaa kali ambao madai yetu makubwa ni - What have You done for me lately! Hii kiswahili mingi ya itikadi na malengo haiwagusi kabisa..

Hii ndio sababu ya CCJ kuanzisha mwamko mpya wa kutunga Muungano wa vyama vya Upinzani. Mkianza na hatua hii hata kujaribu kuungana na wengine kuunda jeshi kubwa mtakuwa mmeanzisha kitu kipya na hakika mtawajua wale wanaotaka kusimama nanyi ktk mapambano na wale wanaojitenga wakitaka madaraka na ruzuku za bunge kwa maniufaa yao binafsi.. Wewe kama Mwanakijiji utawaanika wote hapa na magazetini ili wananchi tusiwape kura zetu..Tunajua fika CCM ina mapandikizi yake ndani ya vyama vyote vya kisiasa na huu ndio wakati wa kuwanasua na kuwatupa nje..Huu ndio wakati pekee wa kufanya mapinduzi ya haki. Nyoosheni mikono yenu msiwe kama Chadema na CUF tulowambia mwaka 2005 wakashindwa kufanya hivyo kisha kwa ujinga wao wakaja taka kuungana baada ya kushindwa uchaguzi mkuu. It was a stupid move, na rahisi kwa CCM kuwavuruga.
 
Mkandara, Kwanini hadi hivi sasa (kabla ya ujio wa CCJ) vyama vya upinzani havijaweza kuungana na kupata huo ushindi?
 
Rudi ukurasa wa kwanza na wa pili...............

Naona wewe na jmushi hamuoni umuhimu wa cross-checking na triangulation. Rejea posti #33 ya Mwanakijiji. Jibu lake linadhihirisha kuwa sio mwanachama mwanzilishi 'absolutely'! Pia tembelea posti zake za zamani kuhusu CJJ. Kisha angalia falsafa zake na uzilinganishe na falsafa mchanyato anazodai kuwa ni za CJJ - tangu lini chama kikawa na mirengo miwili. How can you talk left and walk right or talk right and walk left?
 
Naona wewe na jmushi hamuoni umuhimu wa cross-checking na triangulation. Rejea posti #33 ya Mwanakijiji. Jibu lake linadhihirisha kuwa sio mwanachama mwanzilishi 'absolutely'! Pia tembelea posti zake za zamani kuhusu CJJ. Kisha angalia falsafa zake na uzilinganishe na falsafa mchanyato anazodai kuwa ni za CJJ - tangu lini chama kikawa na mirengo miwili. How can you talk left and walk right or talk right and walk left?

usipoangalia utamiss mengi kweli;.. nenda nyuma kidogo ya "zamani"..
 
I really have no clue!

attachment.php
 
absolutely!
Kama wewe MM ni among founders! !! inabidi nikitupie macho - wacha tuvute subira inawezekana neema ikawa imefunuliwa kwa watanzania - Chama Mbadala kuzaliwa - kilichosubiriwa kwa miongo mingi kitakacholeta tumaini jipya la ukombozi wa kweli.
Sisi wengine ni akina Tomaso, tutasubiri tuone dalili kwanza.
 
usipoangalia utamiss mengi kweli;.. nenda nyuma kidogo ya "zamani"..

Mkuu acha mazingaombwe. Mimi ni msomaji mzuri wa posti zako, kuanzia mashairi mpaka uchambuzi. Mtazamo wako wa kisiasa naweza hata kuuandikia wasifu - hili la CCJ ni bango tu la kutimiza uliyoshindwa kuyatimiza kupitia vyama vingine. Hebu jibu maswali haya kama u mwana-CCJ:

1. Wanachama waanzilishi wa CCJ wapo wangapi?
2. Ulipata kadi ya CCJ lini, wapi na ni namba ngapi?
 
I will not dare to speculate what this means..

Kwa vile hoja zangu zilikuwa mbili, yaani either X or Y. hoja zenyewe ni hizi, Swali la kwanza ni X swali la pili ni Y.
Mzee Mwanakijiji, let me be frank and open,
1. Kwanza: CCJ is for real, and its more that what we see and hear mpaka mtu wa calibre ya Mzee Mwanakijiji kujiunga. Ili nijiridhishe, its for real, natamani kuijua 'the motive behind Mzee Mwanakijiji ndani ya CCJ'.
2. Pili inawezekana kabisa Mzee Mwanakijiji ukawa uko Kazini[/B], na hii piga debe yote ikawa ni sehemu tuu ya majukumu tuu ya kazi

Its just thinking aloud!,


kwa vile vile sijaona jibu lako la swali la kwanza,
then don't speculate, utakuwa ni uko kazini, endelea na kazi nzuri CCJ.
 
Mkuu acha mazingaombwe. Mimi ni msomaji mzuri wa posti zako, kuanzia mashairi mpaka uchambuzi. Mtazamo wako wa kisiasa naweza hata kuuandikia wasifu - hili la CCJ ni bango tu la kutimiza uliyoshindwa kuyatimiza kupitia vyama vingine. Hebu jibu maswali haya kama u mwana-CCJ:

1. Wanachama waanzilishi wa CCJ wapo wangapi?
2. Ulipata kadi ya CCJ lini, wapi na ni namba ngapi?
Companero, nadhani haya ni mambo ya ndani sana kuyaweka hadharani, hata kama ningekuwa ni mimi, nisingejibu, ila kuwa mshabiki/mwanachama muanzilishi, sio lazima uwe ulipata kadi ya uanachama, namba ngapi, lini na wapi. Inavyosikika wale makamanda ndio wanachama waanzilishi huku bado kadi zao za CCM wamezishikilia wakisikilizia hatima ya usajili wa CCJ.
Agostino Lyatonga Mrema, aliwahi kuulizwa kwenye kipindi cha Kiti Moto enzi zile, kuwa mbona hajawahi kuonekana akiikabidhi kadi yake ya CCM, popote?, hakujibu, alipandisha tuu jazba. Sasa unategemea Mwanakijiji ajibu nini kwenye hili?.

Kwa maoni yangu, CCJ bado ni ghost party mpaka hapo kitakapopata usajili wa kudumu, wanachama wake hawa waanzilishi, wana vyama vyao na wengine wana kazi zao, tusubiri wapate usajili wa kudumu, tuwaone wakirudisha kadi za vyama vyao, japo wengi huendelea na kazi zao.
 
Kilicho bora kabisa kwa WaTanzania kwa sasa ni CCM. CCJ mtaanzia wapi ili kuubadili mtazamo huu? Zingatieni pia kwamba vyombo vyote vya DOLA ni "mali" ya CCM na Serikali yake. Mliwaona juzi wakuu wa vyombo hivi walivyokuwa wamempamba JK siku ile anahutubia wazee wa Dar. CCJ mtafanyaje kuyabadili haya?
 
Mwanakiji,

Post nyingi za Mkandara zimetohoa majibu ya maswali na maswali ya majibu.......... Nina kiswali vijidogo tu..
  • Ok, siasa ni sayansi au sayansi ni siasa? kwa mtazamo wa CCJ.....
  • kuna sehemu umesema kuwa ccj kimeanzia chini, wapi na kwa vipi?
  • Yapi mahitaji halisi ya mtz ambayo yameisukuma ccj kuundwa?
  • Kwenye chaguzi za US na UK huwa wanazingatia itikadi au polices?
  • Ni wapi Africa ambapo CCJ imetest itikadi zake ikaona inawork out?
  • inasemekana kuwa uwepo wa CCJ unatokana na richmond....... kwa kuwa wengi kutoka ccm watakuja ccj na wengi wao ndo wale waliokuwemo kwenye hio songombingo, je ccj itatofautishaje hawa na ikiwezekana kuadhibiti hasa ukizingatia mnataka demokrasia ili hali mkajikuta aliyesilimishwa anakuwa askofu?
asante
 
Back
Top Bottom