Cancer inachukua maisha yangu

Cancer inachukua maisha yangu

Baada ya kusumbuka kwa takribani wiki tatu sasa, afya yangu ikiharibika kwa kasi huku mimi binafsi,vipimo na ushauri wa madoctor ukionyesha ni uchovu tu au tatizo la kawaida Jana nimekuja kufanya vipimo hapa Nairobi na inaonyesha nina cancer katika figo langu.

Ninarudi nyumbani kesho, nitajitahidi kuendelea na maisha yangu kama kawaida, lakini huu ni ukweli mbaya sana, cancer is haunting my life.

Pole sana mkuu nakubaliana nawe kabisa ni ukweli mbaya ila naamini kama vipimo vilifanyika vizuri na wakaweza kufanya diagnosis kujua ni stage ipi huo ugonjwa upo kwa sasa ni rahisi kupata tiba appropriate hivyo shaka ondoa kwani tiba zipo na utapona kabisa mkuu. Uwe na tumaini tu na pia mwamini Mungu yeye ni mponyaji wakati sie tunatibu.
 
Hivi dalili zake zikoje?

Sent from my BlackBerry 9700 using JamiiForums
 
Mkuu Sangarara,
Pole na changamoto.

Tafadhali zingatia haya:
1. Iwapo hujafanyiwa operation na kutolewa sample ikathibitishwa maabara si sahihi kusema una cancer. Hapo unakuwa na UVIMBE ambao biological nature yake haifahamiki, ila tu inahisiwa kuwa cancer.

2. Mgonjwa siku hizi yanageuzwa biashara. Usiingie kwenye mtego kununua products ambazo hazijawa scientifically objectively proven kutibu tatizo lako.

3. Don't jump from hospital to hospital or from doctor to doctor. Ingefaa zaidi uendelee na hospitali hiyohiyo waliyokudiagnose.

4. Don't give up. Fight on. Cancer nyingi hutibika kwa operation, radio au chemotherapy. Modern medicine inatoa options za kuboresha maisha ya wagonjwa wa cancer kwa kiwango cha juu sana.
 
Am very sorry brother what matter don't give up ana believe in Jesus you will be healed as god say if you ask anything in my name,i will do it John 14:14.
 
Baada ya kusumbuka kwa takribani wiki tatu sasa, afya yangu ikiharibika kwa kasi huku mimi binafsi,vipimo na ushauri wa madoctor ukionyesha ni uchovu tu au tatizo la kawaida Jana nimekuja kufanya vipimo hapa Nairobi na inaonyesha nina cancer katika figo langu.

Ninarudi nyumbani kesho, nitajitahidi kuendelea na maisha yangu kama kawaida, lakini huu ni ukweli mbaya sana, cancer is haunting my life.

Pole sana...zingatia tu masharti utakayopewa na daktari, hata hivyo m/mungu akujaalie uwe mwenye kupata tiba na upone!!!
 
sija give up, Lakini I know, taarifa hii haitanicha kama nilivyokuwa juzi, Mungu atanisamehe kwa makosa ya namna hii nitakayofanya katika vita hii.

Tunaamini u mpiganaji hodari! Utapigana na Utasimama! Pigana Mkuu wangu! Binafsi naheshimu dawa za Kiafrika! Usisite wala kutia hofu, Unaweza! Pigana! Tupo nyuma yako!
Kila la heri!
 
Pole sn mkuu ukiambiwa itolewe kabla haijavuka mipaka, uccte,
 
Sangarara polee sana. Nimependa ushauri wa wadau wengi waliotoa hapa, I really hope utaufanyia kazi. Nakuombea wepesi katika wakati ambao naamini ni mgumu katika maisha yako. Kila la kheri. Pamoja Saana.
 
Hakika ameyachukua madhaifu yetu YOTE. Na kwa kupigwa kwake sisi TUMEPONA. Mtegemee Mungu na uwe na imani kwamba ushapona. Kauli ya kusema cancer inachukua maisha yako ni kuukana ukuu wa Mungu. Kumbuka pia maneno huumba. Muombe Mungu ili aweze kukuelekeza mahali patakapokupatia suluhisho la tatizo hili. Muombe Mungu akupe watu na si watu tu ila watu muhimu watakaotumika ktk kulimaliza tatizo hili.

Mungu akupatie uponyaji wa haraka.
 
Pole sana Sangarara! Kama walivyosema wengi jaribu kupata 2nd and 3rd and 4th opinion. There is a 50/50 chance kuwa wameku misdiagnose. Usikate tamaa na jaribu za kienyeji hasa hizo ambazo kuna watu wamezitaja na hivo ushahidi upo. Hatua yako ya kuongea hapa ni mwanzo mzuri sana kwani kushare tatizo kunapunguza uzito wake! Nina uhakika baada ya kusoma comments zote hizi unajisikia unafuu tayari. Pole sana na mungu ni mwema pambana na utushirikishe tupo kwa ajili yako wakati wowote.
Mungu ni mwema na huzuni na sala zetu anaziona na kuzisikia. Amenm

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom