Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 58,497
- 131,362
Wanabodi
Hii ni makala yangu kwenye gazeti la Mwananchi la leo.
Sisi Watanzania tuna utamaduni wa kuchangiana kwenye sherehe au misiba,
hivyo ili Tanzania tuweze kupata maendeleo ya kweli, maendeleo endelevu, Watanzania ni lazima tubadilike sio tusichangie sherehe au misiba, bali tubadilike na kuanza kuchangia pia afya, elimu na kuchangiana kuleta maendeleo ikiwemo, kuchangiana mitaji.
Kuna msemo wa Kiswahili usemao, chanda chema hivikwa pete, na mcheza kwao hutunzwa, hii ni makala ya kuwahimiza Watanzania, tuichangie Hospitali ya Benjamin William Mkapa, iliyopo Dodoma, kwa jinsi hospitali hii ilivyo ni mkombozi kwa baadhi ya magonjwa, sio tuu ni hospitali mkombozi mkuu wa upandikizaji figo kwa wagonjwa wa figo na upandikizaji wa uloto kwa wagonjwa wa selimundo, bali Tanzania ndio nchi pekee kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, kupandikisa uloto.
Hospitali hii kwa hapa nchini ndio hospital pekee inayotoa huduma hii nchini Tanzania, hivyo sio tuu ni hospitali tegemewa sana hapa nchini kwetu Tanzania, bali ni fursa kwa nchi yetu kuwa kitovu cha utalii wa kimatibabu, medical tourism, badala ya wagonjwa wa bara la Afrika kufurika nchini India kupata tiba za kibingwa, wafurike Tanzania kupata huduma hizo, na sio tuu kuwatibu watu bali pia kuinui pato la taifa.
Mimi ni mhanga wa ajali mbaya ya pikipiki, mjini Dodoma, nikapata tatizo la brachial plexus injury, kukatika mawasiliano kati ya ubongo na mkono, nikawahishwa hospitali ya Dodoma, flying doctors wakanihamishia Moi, nikapelekwa Hospital ya Mill Park nchini Afrika Kusini, hatimaye nikaenda kuponea India.
Huko kote, vifaa vya vya Moi na vile vya India, vifaa vyetu ni bora zaidi, tatizo letu lilikuwa ni ubingwa wa kufanya operesheni za ubongo, lakini sasa Tanzania tumepiga hatua kubwa, sio tuu kustahili pongezi, bali, juhudi hizo ziungwe mkono kwa watanzania wote, tuchangishane, kuwaokoa wenzetu, kwasababu huduma za kibingwa ni gharama kubwa kwa Watanzania wa kawaida.
Tofauti kati ya Tanzania na huko kote nilikopita kutibiwa, Tanzania mgonjwa anapokelewa hospitalini kama mgonjwa, mtu wa kuhurumiwa na kusaidiwa, kwa wenzetu mgonjwa anapokelewa kama mteja ni mfalme, watu wanakimbizana!. Japo mimi tatizo langu ni mkono, nilikuwa natembea mwenyewe, kufika india, unaletewa kiti, namweleza mhudumu naweza kutembea mwenyewe, anakugomea, wewe ni mgonjwa, sisi tuko hapa kwa ajili ya kukuhudumia, huna sababu ya kutembea, wakati mimi ndio kazi yangu, kaa tukupeleke!.
Hospitali yetu ya Benjamin Mkapa (BMH) imefikia uwezo huo wa kubadilika na kuwa kitovu cha utalii wa kimatibabu mjini Dodoma, ikiwa na mipango ya kuanzisha kijiji cha utalii wa kimatibabu katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Mipango hiyo iko katika mkakati kabambe wa miaka 10 wa hospitali hiyo unaolenga kuimarisha huduma maalum za afya, utafiti na mafunzo. Hospitali pia inaanzisha mfuko maalum wa kusaidia upandikizaji wa uloto kwa watoto wanaougua ugonjwa wa seli mundu na huduma za upandikizaji wa figo kwa watu wenye uhitaji kwa kushirikiana na Mfuko wa Kitaifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Mpango huo unalenga kukusanya bilioni 7/- ndani ya miaka miwili, huku bilioni 4/- zikiwa tayari zimekusanywa. Mkurugenzi Mtendaji wa BMH, Profesa Abel Makubi, alifichua mipango hiyo wiki hii alipokuwa akiwapa wahariri wa Jukwaa la Wahariri, taarifa jijini Dar es Salaam kabla ya sherehe za miaka 10 za hospitali hiyo zilizopangwa kufanyika Julai mwaka huu.
Profesa Makubi amesema mafanikio ya hospitali katika muongo mmoja uliopita yameiweka katika nafasi ya kupanua utalii wa kimatibabu, na kuvutia wagonjwa kutoka nchi jirani wanaotafuta matibabu maalum.
Alisema BMH kwa sasa ina wafanyakazi 1,073 ikilinganishwa na wafanyakazi 20 pekee wakati hospitali hiyo ilipoanzishwa Oktoba 13, 2015. Kulingana naye, hospitali hiyo sasa inahudumia takriban watu milioni 10 kutoka mikoa minane kote nchini.
Profesa Makubi aliongeza kuwa hospitali imeendelea kuvutia wagonjwa wa kimataifa kupitia huduma za utalii wa kimatibabu. "Chini ya utalii wa kimatibabu, tumewatibu wagonjwa 2,897 kutoka Burundi, 526 kutoka Comoro na mgonjwa mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), pamoja na wagonjwa wengine wa kigeni," alisema.
Akielezea kwa undani kuhusu upandikizaji wa uloto kwa watoto wenye ugonjwa wa seli mundu, Mkurugenzi Msaidizi na Mtaalamu wa Hematology, Dkt. Stella Mangae, amesema Upandikizaji uloto (Bone Marrow Transplant) ni utaratibu wa kitiba ambapo uloto ulioharibika au kuugua hubadilishwa na kuwekwa uloto wenye afya kutoka kwa mchangiaji. Upandikizaji huu hutibu magonjwa ya Selimundu (Sickle Cell Anemia), Kansa ya Damu (Leukemia) na Matatizo ya Kinga ya Mwili na Magonjwa ya Kurithi
Amesema hadi sasa BMH imeishawatibu wagonjwa 30, ambapo 12 wamepona kikamilifu na kuendelea na maisha ya kawaida, ikiwa ni pamoja na kurudi shuleni. Alisema wagonjwa wawili wamelazwa kwa sasa, akiwemo mmoja kutoka DRC.
Dkt. Mangae alikiri gharama kubwa ya upandikizaji wa uloto lakini akaipongeza serikali kwa kufidia gharama za matibabu zinazofikia milioni 75 kwa kila mgonjwa.
Ili kupunguza mzigo kwa wananchi, serikali na wadau mbalimbali tujitolee kushiriki harambee hii ya hospitali ya BMH kwa kuchangia chochote ulichonacho kuanzia shilingi 1,000, kama Watanzania tuna utamaduni wa kuchangia sherehe kama harusi, lazima sasa tubadilike na kuchangia harambee za Afya na Elimu.
Jinsi ya kuchangia kwa watu wa kawaida, Michango inaweza kutumwa kupitia:
Namba ya Malipo (Control Number): 986930000001
Jina: BMH Organ Tanzania, kwa mitandao yote ya simu.
Kwa upande wa taasisi, michango itumwe akaunti namba : 102501000407
Benki Kuu ya Tanzania
Jina: BMH Organ Tanzania
Hospitali ya BMH ni chanda chema, chanda chema huvikwa pete, tuivike pete kwa kuichangia, kama ilivyo kwa mcheza kwao hutunzwa, tuitunze BMH kwa kuichangia, itutunze!.
Paskali
Hii ni makala yangu kwenye gazeti la Mwananchi la leo.
Sisi Watanzania tuna utamaduni wa kuchangiana kwenye sherehe au misiba,
hivyo ili Tanzania tuweze kupata maendeleo ya kweli, maendeleo endelevu, Watanzania ni lazima tubadilike sio tusichangie sherehe au misiba, bali tubadilike na kuanza kuchangia pia afya, elimu na kuchangiana kuleta maendeleo ikiwemo, kuchangiana mitaji.
Kuna msemo wa Kiswahili usemao, chanda chema hivikwa pete, na mcheza kwao hutunzwa, hii ni makala ya kuwahimiza Watanzania, tuichangie Hospitali ya Benjamin William Mkapa, iliyopo Dodoma, kwa jinsi hospitali hii ilivyo ni mkombozi kwa baadhi ya magonjwa, sio tuu ni hospitali mkombozi mkuu wa upandikizaji figo kwa wagonjwa wa figo na upandikizaji wa uloto kwa wagonjwa wa selimundo, bali Tanzania ndio nchi pekee kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, kupandikisa uloto.
Hospitali hii kwa hapa nchini ndio hospital pekee inayotoa huduma hii nchini Tanzania, hivyo sio tuu ni hospitali tegemewa sana hapa nchini kwetu Tanzania, bali ni fursa kwa nchi yetu kuwa kitovu cha utalii wa kimatibabu, medical tourism, badala ya wagonjwa wa bara la Afrika kufurika nchini India kupata tiba za kibingwa, wafurike Tanzania kupata huduma hizo, na sio tuu kuwatibu watu bali pia kuinui pato la taifa.
Mimi ni mhanga wa ajali mbaya ya pikipiki, mjini Dodoma, nikapata tatizo la brachial plexus injury, kukatika mawasiliano kati ya ubongo na mkono, nikawahishwa hospitali ya Dodoma, flying doctors wakanihamishia Moi, nikapelekwa Hospital ya Mill Park nchini Afrika Kusini, hatimaye nikaenda kuponea India.
Huko kote, vifaa vya vya Moi na vile vya India, vifaa vyetu ni bora zaidi, tatizo letu lilikuwa ni ubingwa wa kufanya operesheni za ubongo, lakini sasa Tanzania tumepiga hatua kubwa, sio tuu kustahili pongezi, bali, juhudi hizo ziungwe mkono kwa watanzania wote, tuchangishane, kuwaokoa wenzetu, kwasababu huduma za kibingwa ni gharama kubwa kwa Watanzania wa kawaida.
Tofauti kati ya Tanzania na huko kote nilikopita kutibiwa, Tanzania mgonjwa anapokelewa hospitalini kama mgonjwa, mtu wa kuhurumiwa na kusaidiwa, kwa wenzetu mgonjwa anapokelewa kama mteja ni mfalme, watu wanakimbizana!. Japo mimi tatizo langu ni mkono, nilikuwa natembea mwenyewe, kufika india, unaletewa kiti, namweleza mhudumu naweza kutembea mwenyewe, anakugomea, wewe ni mgonjwa, sisi tuko hapa kwa ajili ya kukuhudumia, huna sababu ya kutembea, wakati mimi ndio kazi yangu, kaa tukupeleke!.
Hospitali yetu ya Benjamin Mkapa (BMH) imefikia uwezo huo wa kubadilika na kuwa kitovu cha utalii wa kimatibabu mjini Dodoma, ikiwa na mipango ya kuanzisha kijiji cha utalii wa kimatibabu katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM).
Mipango hiyo iko katika mkakati kabambe wa miaka 10 wa hospitali hiyo unaolenga kuimarisha huduma maalum za afya, utafiti na mafunzo. Hospitali pia inaanzisha mfuko maalum wa kusaidia upandikizaji wa uloto kwa watoto wanaougua ugonjwa wa seli mundu na huduma za upandikizaji wa figo kwa watu wenye uhitaji kwa kushirikiana na Mfuko wa Kitaifa wa Bima ya Afya (NHIF).
Mpango huo unalenga kukusanya bilioni 7/- ndani ya miaka miwili, huku bilioni 4/- zikiwa tayari zimekusanywa. Mkurugenzi Mtendaji wa BMH, Profesa Abel Makubi, alifichua mipango hiyo wiki hii alipokuwa akiwapa wahariri wa Jukwaa la Wahariri, taarifa jijini Dar es Salaam kabla ya sherehe za miaka 10 za hospitali hiyo zilizopangwa kufanyika Julai mwaka huu.
Profesa Makubi amesema mafanikio ya hospitali katika muongo mmoja uliopita yameiweka katika nafasi ya kupanua utalii wa kimatibabu, na kuvutia wagonjwa kutoka nchi jirani wanaotafuta matibabu maalum.
Alisema BMH kwa sasa ina wafanyakazi 1,073 ikilinganishwa na wafanyakazi 20 pekee wakati hospitali hiyo ilipoanzishwa Oktoba 13, 2015. Kulingana naye, hospitali hiyo sasa inahudumia takriban watu milioni 10 kutoka mikoa minane kote nchini.
Profesa Makubi aliongeza kuwa hospitali imeendelea kuvutia wagonjwa wa kimataifa kupitia huduma za utalii wa kimatibabu. "Chini ya utalii wa kimatibabu, tumewatibu wagonjwa 2,897 kutoka Burundi, 526 kutoka Comoro na mgonjwa mmoja kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), pamoja na wagonjwa wengine wa kigeni," alisema.
Akielezea kwa undani kuhusu upandikizaji wa uloto kwa watoto wenye ugonjwa wa seli mundu, Mkurugenzi Msaidizi na Mtaalamu wa Hematology, Dkt. Stella Mangae, amesema Upandikizaji uloto (Bone Marrow Transplant) ni utaratibu wa kitiba ambapo uloto ulioharibika au kuugua hubadilishwa na kuwekwa uloto wenye afya kutoka kwa mchangiaji. Upandikizaji huu hutibu magonjwa ya Selimundu (Sickle Cell Anemia), Kansa ya Damu (Leukemia) na Matatizo ya Kinga ya Mwili na Magonjwa ya Kurithi
Amesema hadi sasa BMH imeishawatibu wagonjwa 30, ambapo 12 wamepona kikamilifu na kuendelea na maisha ya kawaida, ikiwa ni pamoja na kurudi shuleni. Alisema wagonjwa wawili wamelazwa kwa sasa, akiwemo mmoja kutoka DRC.
Dkt. Mangae alikiri gharama kubwa ya upandikizaji wa uloto lakini akaipongeza serikali kwa kufidia gharama za matibabu zinazofikia milioni 75 kwa kila mgonjwa.
Ili kupunguza mzigo kwa wananchi, serikali na wadau mbalimbali tujitolee kushiriki harambee hii ya hospitali ya BMH kwa kuchangia chochote ulichonacho kuanzia shilingi 1,000, kama Watanzania tuna utamaduni wa kuchangia sherehe kama harusi, lazima sasa tubadilike na kuchangia harambee za Afya na Elimu.
Jinsi ya kuchangia kwa watu wa kawaida, Michango inaweza kutumwa kupitia:
Namba ya Malipo (Control Number): 986930000001
Jina: BMH Organ Tanzania, kwa mitandao yote ya simu.
Kwa upande wa taasisi, michango itumwe akaunti namba : 102501000407
Benki Kuu ya Tanzania
Jina: BMH Organ Tanzania
Hospitali ya BMH ni chanda chema, chanda chema huvikwa pete, tuivike pete kwa kuichangia, kama ilivyo kwa mcheza kwao hutunzwa, tuitunze BMH kwa kuichangia, itutunze!.
Paskali