Sizungumzii ubora wa majengo yanayojengwa Nairobi au Kenya kijumla
Na wala sizungumzii kuhusu kubomolewa nyumba Morogoro Road kuanzia Kimara hadi Kibamba wala jengo la Tanesco, la hasha
Hapa nazungumzia hatuna sheria za maana za kukomesha ujenzi wa makazi holela kama haya yaliyopo Manzese, Tandale, Mwananyamala, Mbagala, Tandika, Keko n.k
Ni vile kila mtu akipata pesa ananunua kiwanja anajenga bila kufuata utaratibu wowote wa mipango miji, hili nchini kwetu ni tatizo
Hali ni tofauti na Kenya, penye ukweli lazima tuseme hizo slums wako nazo wana hali ngumu kweli kuliko hizi sehemu zetu za uswazi... Nyumba zilizopo uswazi kwetu ni bora kuliko zilizopo kwenye slums zao
Ila ukitoka nje ya hizo slums hukuti typical character za akina Manzese, Tandale, Tandika na Keko zaidi ya kukuta Estates na Gated Community za maana
Issue ya makazi kwao nyang'au ziko serious sana
Sent using
Jamii Forums mobile app