Hyo lilikuwepo...ila kwa sasa wame catch up kiasi...mombasa kuna wakati ilikuwa imesimama sana kw ajili ya zile tabia vijana kutojituma...ila sai vijana wengi wanajituma angalau kufikia malengo yao..bali mila na tamaduni zetu hatuwezi zitelekeza...mombasa ni mji wa anasa bana pwani mwa kenya...
friend-wise vijana wa kimombasa mpo vizuri sana kuliko wa kutoka jamii zingine za kenya.
nitakupa story moja. miaka kadhaa iliyopita ikiwa ndio mara yangu ya kwanza kufika nairobi, nilikuwa napata shida sana na maisha ya upweke. nazungumzia ule upweke wa kutojichangaya na watu.
nikirudi tu toka job najifungia kwa nyumba mpaka mida jioni.....yaani nilikuwa ziwezi ku interact na watu kutokana na ile selfish lifestyle ya watu wa nairobi.no greetings no story.
basi after three months nikapata "beshte" wangu mmoja hivi mkikuyu aliyezaliwa mombasa, kusomea mombasa na kukulia mombasa. he was very friendly to me. hata kiswahili chake ni typical mombasa accent.
yeye ndio mtu pekee aliyenitembeza karibia night club zote za nairobi, tulikuwa tunakula bata sana siku za weekend. he used to take me as his brother.
alisomea masuala ya computer, too bad alikuwa hana job. last year but one(2016) nikamwambia njoo dar es salaam tuone vile tutafanya kuhusu profession yako.
kwa sasa yupo hapa dar akipiga kazi katika organization moja ambayo nilimtafutia job.
urafiki wetu umekuwa ni kama ndugu. amepata manzi wa kitz, next year inshallah watafunga ndoa.
pia ako na talent ya uigizaji... nikamu introduce kwa wadau wa industry ya bongomuvi. he is catching up in acting, hopefully one day atakuja kuwa star wa movie za kibongo.
ningeweza kukutajia jina lake but haitakuwa poa.bila shaka utakuwa unamfahamu.