Tunahitaji kujua lugha nyingi na za kimataifa kadiri inavyowezekana. Hapa tunazungumzia English kwa sababu ndiyo lugha iliyoachwa na mtawala wa mwisho wa kikoloni wa nchi yetu, Uingereza. Mtawala wa mwisho angelikuwa mjerumani tungekuwa tunazungumzia kijerumani. Lugha ya kigeni katika mazingira yote ni rahisi kuijua ikifundishwa mashuleni kutoka chini kabisa. Hakuna anayesema Kiswahili hakiitajiki. Kiswahili nacho kifundishwe watu wakielewa kwa ufasaha siyo wale wa siku hizi wanaiga kiswahili cha Kenya ambapo WANAUME wanawaita WABABA na WANAWAKE wanawaita WAMAMA. Ni aibu tupu.. Labda kama msamihati wa Kiswahili sasa umekuwa. Kiswahili ni rahisi kuendelea nacho kwa sababu tunaishi nacho mitaani na kinafundishwa mashuleni. English itumike kama lugha ya kufundishia mashuleni kutoka Chekechea mpaka Vyuo vya elimu ya juu ndiyo tutaielewa vizuri na watoto na wajukuu wa nchi yetu wataielewa vizuri.