Kwa wale ndugu zangu wanyamwezi na wasukuma toka Tabora na watu mliowahi kufika Tabora mtakubaliana na mimi ya kwamba tatizo la wehu,wendawazimu na vichaa kuwa wengi lipo muda mrefu na kila siku linazidi kuongezeka mpka imefika hatua imekuwa kero sasa.
Eneo kama stendi mkuu hapo Tabora mjini kuna wehu na vichaa wanashinda pale wanapigana mitii hadharani wako uchi wa mnyama,ukipita njianindo usiseme katika watu sita utakaopishana nao basi watatu ni wehu ukipita soko kuu ndo usiseme wehu na vichaa wamejaa alafu hawana ustarabu siku akili zao zikifyatuka wanafanya fujo wanarusha mawe ovyoo waharibu biashara za watu yaani hawa viumbe wenzetu wamekuwa ni tatizo sana si mjini si vijijini wapo wengi kama juzi nilikuwa urambo soko kuu kuna mwehu nilimuona anajisaidia hadharani .
Lakini yote tisa hebu tuelezane ni kwanini katika huu mkoa wetu kwanini wehu, wendawazimu na vichaa ni wengi inawezekana labda mi nimekulia Dar labda sifahamu lakini nimetembea mikoa mingi ila Tabora too much.